Hodi humu ndani
mie sio mwenyeji sana, ni mgeni kiasi
Nimekuja na shida yangu tafadhali naomba msaada wenu
Mie ni dada wa makamo, niko nje ya nchi kwa masomo.Tangu nifike hapa nimekuwa mtu wa kujiepusha sana na mambo ya mapenzi na kujitahidi kujikita zaidi kwenye masomo nisije nikakosa degree yangu na kurudi bongo kwa aibu au nikaamua kubaki huku kwa kukwepa aibu ya kushindwa.Namshukuru Mungu nimeweza kuruka viunzi vingi vya mapenzi.Well, tatizo limekuja siku za karibuni kukutana na kaka mmoja anayetokea moja ya nchi zilizo kusini mwa Afrika.mwanzoni alipoanza kunifuatilia kimapenzi nilisikia kichekesho kwa sababu kaka huyu macho kumchuzi,(makengeza) kwa hiyo nilikuwa nasikia kucheka kila mara anaposisitizia azma yake ya kuwa na mie.Cha ajabu jinsi siku zinavyokwenda naanza kumwonea huruma(sina hakika kama ni huruma au ni mapenzi)natamani kumwona mara kwa mara. asiponitakia goodnite najisikia vibaya.Akikaa siku nzima bila kunipigia nasononeka. In short mie nisipoona yale macho basi hujisikia vibaya mwenzenu na kila nikimuona kamoyom kangu kananidunda lakini najipa moyo kwamba ninachojihisi ni huruma sio mapenzi.sasa wadau ninawezaje kujua hasa nini kilicho moyoni mwangu.Weekend hii kaniofa twende movie lakini nasita mana sina uhakika na feelings zangu mwenyewe.ushauri tafadhali kabla sijachemka dada yenu.
mie sio mwenyeji sana, ni mgeni kiasi
Nimekuja na shida yangu tafadhali naomba msaada wenu
Mie ni dada wa makamo, niko nje ya nchi kwa masomo.Tangu nifike hapa nimekuwa mtu wa kujiepusha sana na mambo ya mapenzi na kujitahidi kujikita zaidi kwenye masomo nisije nikakosa degree yangu na kurudi bongo kwa aibu au nikaamua kubaki huku kwa kukwepa aibu ya kushindwa.Namshukuru Mungu nimeweza kuruka viunzi vingi vya mapenzi.Well, tatizo limekuja siku za karibuni kukutana na kaka mmoja anayetokea moja ya nchi zilizo kusini mwa Afrika.mwanzoni alipoanza kunifuatilia kimapenzi nilisikia kichekesho kwa sababu kaka huyu macho kumchuzi,(makengeza) kwa hiyo nilikuwa nasikia kucheka kila mara anaposisitizia azma yake ya kuwa na mie.Cha ajabu jinsi siku zinavyokwenda naanza kumwonea huruma(sina hakika kama ni huruma au ni mapenzi)natamani kumwona mara kwa mara. asiponitakia goodnite najisikia vibaya.Akikaa siku nzima bila kunipigia nasononeka. In short mie nisipoona yale macho basi hujisikia vibaya mwenzenu na kila nikimuona kamoyom kangu kananidunda lakini najipa moyo kwamba ninachojihisi ni huruma sio mapenzi.sasa wadau ninawezaje kujua hasa nini kilicho moyoni mwangu.Weekend hii kaniofa twende movie lakini nasita mana sina uhakika na feelings zangu mwenyewe.ushauri tafadhali kabla sijachemka dada yenu.