Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,013
- 144,371
Wanaccm msiposhughulikia mambo haya, hakika chama chenu kitashindwa vibaya 2015 na hata chaguzi zingine.
(1)Raisi kuwa mwenyekiti wa chama Taifa.
Hili ni tatizo kubwa sana, kwani inakuwa vigumu kwa chama kuisimamia serikali hata pale inapoboronga kwa mfano hali ilivyo sasa.
(2)Utaratibu kuwa raisi aliyepo lazima atumikie vipindi 2 vya miaka mitano mitano.
Hakika huu ni utaratibu mbovu sana kwani hata kama ataonekana kupwaya au kuvurunda ktk kipindi cha kwanza shariti apewe kipindi cha pili na ukimpinga chama kinakujia juu.Kigezo kiwe ni uwezo ni si kubebana na athari yake hata nyie sasa mnaiona.
(3)Individuals kuwa muhimu kuliko hata chama.
Inasikitisha sana ccm ya leo iko radhi kubeba watu wachache kwa gharama ya chama kizima.Mtu amefanya madhambi ya wazi ila atalindwa kwa nguvu zote bila kujali athari kwa chama.Kulindana ni cancer ianayotafuna taswira ya chama chenu mbele ya macho ya umma.
(4)CCM ya leo kutokujali na kupuuza shida za maskini walio wengi na kujali matajiri kuanzia kwenye chama chenyewe na nchi nzima kwa ujumla.
(5)Wanaccm wenyewe kushindwa kukemeana,kukosoana na kuelzena ukweli pale mnapokosea na badala yake mmewaachia wapinzani hakika watazidi kupanda chati.
(5)Ahadi za miaka nenda rudi zisizotekelezwa.
(6)Wanaccm kumuona raisi kama mungu mtu asiyestahili kukosolewa na badala yake kujipendekeza kwake mkitarajia kupewa vyeo.Mkosoeni siyo kujipendekeza anakiathiri chama.
(7)Viongozi na wanaccm kutokusoma alama za nyakati.
Athari yake mnashindwa kujua nini umma wa watanzania unataka kwa sasa na mmebaki kuhubiri siasa za kizamani za amani na utulivu.Watanzania wa leo wanajua hata wapinzani wanaamini na kuthamini uwepo wa amani na utulivu.
(8)Rushwa wakati wa uchaguzi.
Hii ni wakati wa uteuzi wa wagombea ndani ya chama na kwa wapiga kura kwa ujumla.Kumbukeni sasa hivi vyombo vya habari vinaendesha elimu ya uraia isiyo rasimi na watanzania wanaelimika na kujua athari ya rushwa hasa kwenye uchaguzi.
(9)Siasa za makundi na ufalume wa kupeana madaraka unaojipenyeza kwa kasi ndani ya chama chenu.
Hapa sihitaji kutoa ufafanuzi wenyewe mnayajua haya.
Huu ni ushauri wa bure kwenu.
(1)Raisi kuwa mwenyekiti wa chama Taifa.
Hili ni tatizo kubwa sana, kwani inakuwa vigumu kwa chama kuisimamia serikali hata pale inapoboronga kwa mfano hali ilivyo sasa.
(2)Utaratibu kuwa raisi aliyepo lazima atumikie vipindi 2 vya miaka mitano mitano.
Hakika huu ni utaratibu mbovu sana kwani hata kama ataonekana kupwaya au kuvurunda ktk kipindi cha kwanza shariti apewe kipindi cha pili na ukimpinga chama kinakujia juu.Kigezo kiwe ni uwezo ni si kubebana na athari yake hata nyie sasa mnaiona.
(3)Individuals kuwa muhimu kuliko hata chama.
Inasikitisha sana ccm ya leo iko radhi kubeba watu wachache kwa gharama ya chama kizima.Mtu amefanya madhambi ya wazi ila atalindwa kwa nguvu zote bila kujali athari kwa chama.Kulindana ni cancer ianayotafuna taswira ya chama chenu mbele ya macho ya umma.
(4)CCM ya leo kutokujali na kupuuza shida za maskini walio wengi na kujali matajiri kuanzia kwenye chama chenyewe na nchi nzima kwa ujumla.
(5)Wanaccm wenyewe kushindwa kukemeana,kukosoana na kuelzena ukweli pale mnapokosea na badala yake mmewaachia wapinzani hakika watazidi kupanda chati.
(5)Ahadi za miaka nenda rudi zisizotekelezwa.
(6)Wanaccm kumuona raisi kama mungu mtu asiyestahili kukosolewa na badala yake kujipendekeza kwake mkitarajia kupewa vyeo.Mkosoeni siyo kujipendekeza anakiathiri chama.
(7)Viongozi na wanaccm kutokusoma alama za nyakati.
Athari yake mnashindwa kujua nini umma wa watanzania unataka kwa sasa na mmebaki kuhubiri siasa za kizamani za amani na utulivu.Watanzania wa leo wanajua hata wapinzani wanaamini na kuthamini uwepo wa amani na utulivu.
(8)Rushwa wakati wa uchaguzi.
Hii ni wakati wa uteuzi wa wagombea ndani ya chama na kwa wapiga kura kwa ujumla.Kumbukeni sasa hivi vyombo vya habari vinaendesha elimu ya uraia isiyo rasimi na watanzania wanaelimika na kujua athari ya rushwa hasa kwenye uchaguzi.
(9)Siasa za makundi na ufalume wa kupeana madaraka unaojipenyeza kwa kasi ndani ya chama chenu.
Hapa sihitaji kutoa ufafanuzi wenyewe mnayajua haya.
Huu ni ushauri wa bure kwenu.