ALU-MASOLI
Member
- Mar 2, 2010
- 57
- 1
:argue:
Wanajamii wenzangu, je haya majibu yanasadifu kile kilichokuwa kikidaiwa na walengwa wa lile lalamiko?
Wanajamii wenzangu, je haya majibu yanasadifu kile kilichokuwa kikidaiwa na walengwa wa lile lalamiko?
CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
UFAFANUZI KUHUSU FURSA KWA WANAFUNZI KUPIGA
KURA CHUONI WAKATI WA LIKIZO
UFAFANUZI KUHUSU FURSA KWA WANAFUNZI KUPIGA
KURA CHUONI WAKATI WA LIKIZO
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kinapenda kufafanua kwamba, ingawa tangu tarehe 24 Julai mwaka huu wanachuo walio wengi wamekuwa mapumzikoni, hakuna kampasi
yoyotote ya Chuo Kikuu iliyofungwa. Shughuli zote muhimu za Chuo, zikiwemo
ufundishaji wa makundi kadhaa ya wanafunzi wa shahada za kwanza, utafiti, huduma
za maktaba, utoaji wa ushauri wa kitaaluma na shughuli mbalimbali zinazohusiana na
mafunzo ya uzamili na uzamivu zimekuwa zikiendelea muda wote. Kwa kifupi, Chuo
kimeendelea kutoa huduma kwa wadau wake wote.
Kwa hiyo ni wazi kwamba siku ya uchaguzi, yaani tarehe 31 Oktoba 2010, vituo vya
kupigia kura vilivyopo ndani ya kampasi za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam vitawapokea
na kuwahudumia watu wote wenye stahili ya kupiga kura hapo bila usumbufu wowote.
Watakaohudumiwa kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na Tume ya Uchaguzi ni
pamoja na wanafunzi, wafanyakazi waliojiandikisha Chuoni na wananchi kutoka
maeneo yanayozunguka kampasi za Chuo.
yoyotote ya Chuo Kikuu iliyofungwa. Shughuli zote muhimu za Chuo, zikiwemo
ufundishaji wa makundi kadhaa ya wanafunzi wa shahada za kwanza, utafiti, huduma
za maktaba, utoaji wa ushauri wa kitaaluma na shughuli mbalimbali zinazohusiana na
mafunzo ya uzamili na uzamivu zimekuwa zikiendelea muda wote. Kwa kifupi, Chuo
kimeendelea kutoa huduma kwa wadau wake wote.
Kwa hiyo ni wazi kwamba siku ya uchaguzi, yaani tarehe 31 Oktoba 2010, vituo vya
kupigia kura vilivyopo ndani ya kampasi za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam vitawapokea
na kuwahudumia watu wote wenye stahili ya kupiga kura hapo bila usumbufu wowote.
Watakaohudumiwa kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na Tume ya Uchaguzi ni
pamoja na wanafunzi, wafanyakazi waliojiandikisha Chuoni na wananchi kutoka
maeneo yanayozunguka kampasi za Chuo.
IMETOLEWA NA OFISI YA UHUSIANO
CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
13 Oktoba, 2010
CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
13 Oktoba, 2010