The Intelligent
JF-Expert Member
- Dec 27, 2013
- 2,459
- 818
kuna jamaa angu mhaya alikua anaoa basi rafiki yetu mkurya akaenda pale kwenye kiti cha bwana harusi akakaa anagoma kutoka mpaka pesa itolewe
Kwanini?
kuna jamaa angu mhaya alikua anaoa basi rafiki yetu mkurya akaenda pale kwenye kiti cha bwana harusi akakaa anagoma kutoka mpaka pesa itolewe
kuna jamaa angu mhaya alikua anaoa basi rafiki yetu mkurya akaenda pale kwenye kiti cha bwana harusi akakaa anagoma kutoka mpaka pesa itolewe
Wakurya ni wajukuu wa wahaya, kwa hiyo hata iwe vipi babu / bibi hawezi mdharau mjukuu. Na mjukuu hawezi chukizwa na utani wa babu/bibi.
aaah karibu blaaza sukari ya warembo...mutu ya puturu.............. mutu ya minara kokonati oiliiUnamkuta mtu kakaa katika kundi la watu, mara baada ya wewe kufika sehemu hiyo anakupokea kwa maneno kibao ya utani, na kati ya hayo maneno mengine ni ya kukudhalilisha mbele za watu. Kisa? Kwa sababu tu yeye anapenda kutania! Anafanya hivyo bila hata ya kuelewa kuwa una uhusiano gani na watu wengine katika kundi hilo, kwa maana si kila utani unafaaa wakati wote mbele za watu wote.
Wasukuma wana watani wangapi jamani...!? Pwani, Morogoro, Dodoma na Sasa Rukwa wote ni watani wa Wasukuma? Tunaomba chati inayoonyesha, kabila lipi lina taniana na lipi. Kwenye chati hiyo nitajua watani wangu wa ziada maana kijijini kwetu Kusadikika tunajulikana kwa kutania na akina Anduje Ngoswe Kibanga. Pia nilisikia Mgaramao na nao wanatatizwa na idadi ya makabila wanayotaniana nayo.Utani wa Wafipa na Wasukuma ni hatari
Duh! Wakurya nao wamebananishwa...Ha ha haa! Wakivamiwa na kundi lote hilo panakalika kweli. Ha ha aa!Wahehe vs wakirya
Waha vs wakurya
Wahaya vs wakurya
Wanyaturu vs wakurya
Wanyiramba vs wakurya
Nawazaga ilitokeaje wasukuma wakawa na utani na wagogo na wazaramo na watu wote wa iringa? Kwanza wako mbalimbali kweli!!Nadhani ilikuja tu automatically. Starting point ni kujua haya mambo yalianza lini. Hii ya wahaya na waha sio common sana lakini nasikia enzi hizo wazungu walipokuja Kigoma wakauliza "What tribe you?" wakasema "Baha". Walipoenda Bukoba wakauliza "Are you also Baha?" wakajibu "Yeah". Kwa hiyo ile "ya" ikaongezwa mwisho kuwa "Bahaya".
haaa ase mi sijajua sa si wako mbali sana imekuwaje ?Mi naupendaga sana utani wa wachaga na wafipa!
mhhh watu kumsifia nyerere vitu ambavyo hakufanya hamjambo ,utani ulikuwepu kabla nyerere hajazaliwa kenya pia makabila mengi yanautani nako ni nyerere hahahahaNafikiri ilikuwa ni strategical moves ya Nyerere kuwaunganisha watanzania na ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana.
Kwani umewahi kusikia makabila ya jirani zetu waKenya ama kule Rwanda wakitaniana??
nakwambiaDuh! Wakurya nao wamebananishwa...Ha ha haa! Wakivamiwa na kundi lote hilo panakalika kweli. Ha ha aa!
Wakurya shida.Mleta mada hii unatakiwa ujue makabila na asili, mila na tamaduni zao ndipo uje kuuliza la Wakurya na wahaya. Pili napenda nikusahihishe kidogo, ni kwamba wahaya na Wanyambo wanataniana na Wakerewe, Wajita, Wajaluo na Wakurya amabao katika wakurya kuna vikabila au koo kama Wasimbiti, wangorome, Wasweta, Waruri, Wazanaki, Wakabwa, wakiroba, Wakwaya, Waikoma, Wanata, Waisenye, Waikizu etc Vile Vile Wahaya na Wanyambo wanataniana na Waha wa Kigoma
Ukishajua hivyo ndipo uje na swali lako
Prof Gwasa (RIP) wa UDSM alitoa andiko zuri sana kuhusu mada hii. Andiko lilichukua jina LA "Utani Complex". Ukitaka kujua zaidi kuhusu suala la utani kati ya makabila basis tafunta andiko hili.Wakuu,
Nimezaliwa katika kizazi hiki cha dotcom na nikaikuta Tanzania ikiwa hai, ndani ya jamii ya nchi yetu hii nikakuta kuna muingiliano mkubwa wenye bashasha miongoni mwa wananchi. Ndani ya mipaka ya nchi hii ikajengwa hulka na tamaduni za kuondoleana utofauti kwa misingi ya dini, jinsia ukabila, ukanda n.k. Kinachonifanya kutafakari ni juu ya suala la Utani wa Makabila.
Nawasilisha na naomba kusaidiwa kujuzwa ili niweze kufahamu juu ya hili, mniwie radhi iwapo nitakuwa nimeikosea jamii yetu kwa kuweka hoja hii mbele yenu.
- Je, ni nini kilikuwa chanzo cha kuanzisha utani wa kikabila (Mfano Wanyamwezi na Wagogo - WATANI)
- Je, ni hali tuliyoirithi toka kwa wakoloni ama ilianza punde tulipopata uhuru?
- Nani muanzilishi wa kutambulisha kabila hili ni watani wa kabila fulani?
- Je, hali hiyo ya utani bado ipo mpaka leo na ikiwa hai au imebaki kuparurana tu?
- Kwa wale mliokula chumvi nyingi, hali ya utani wa makabila ilijenga au lah!
----
BAADHI YA MICHANGO YA WANA-JF
CHANZO CHA UTANI WA WAHEHE NA WANGONI
Wangoni ndio kabila ambalo ni watani wa jadi wa Wahehe, moja ya sababu ambazo hutajwa kuwa sababu ya utani huu ni kuwa katika vita za kikabila zilizokuwa zikiendelea kabla ya ujio wa wakoloni, Wahehe na Wangoni waliwahi kupigana na hakukupatikana mshindi, na kuanzia hapo walianza utani kila moja akitamba kuwa bora kuliko mwenzie.
Utani wa makabila haya mawili ni utani wenye heshima watu wa rika moja ndio ambao hutaniana, hauhusishi matusi kama ulivyo utani wa baadhi ya makabila. Na utani huu hugeuka nyenzo muhimu ya kusaidiana wakati wa misiba ambapo watani husaidia kukusanya michango na kufanya kazi ambazo zinawapunguzia mzigo wafiwa.
Wanataniana sana. Wajaluo na Wakalenjin, Waluo na waluhya nkNafikiri ilikuwa ni strategical moves ya Nyerere kuwaunganisha watanzania na ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana.
Kwani umewahi kusikia makabila ya jirani zetu waKenya ama kule Rwanda wakitaniana??
Ha ha ha ha ha yote ni sawa la msingi wanaishi vizuri1. Nasikia Wazaramo walikuwa Wagogo zamani. Kulipotokea shida ya Chumvi, wakaamuwa kuwatuma wenzao waende Pwani kununua Chumvi na kuileta Dodoma. Jamaa walipofika Pwani wakaamua kubaki huko Milele. Kwa maana nyingine kwa Kiswahili cha kisasa ungesema "Walizamia" na hii ndiyo mwanzo wa jina la WAZARAMO yaani Walizaramia.
2. Wagogo zamani walikuwa Wazaramo. Kulipotokea Msiba huko pwani, wakaamua kuwatuma wenzao waende Dodoma kununua Mbuzi kwa ajili ya Arobaini. Jamaa wakaenda Dodoma na kufika huko, wakala zile hela za kununulia mbuzi na hawakurudi. Wazee wa pwani wakakaa na kuwaombea Albadiri (laana) na Wagogo hadi leo wana matatizo ya macho (Matonya and Comp.)
Sasa sijui kipi kina ukweli. Ila hawa jamaa wamekuwa watani hadi kesho.