Hawataki kuhama: Wamang'ati wajiandaa kupambana na Polisi

Companero

Platinum Member
Jul 12, 2008
5,604
1,704
Wabarbaig watangaza vita

Na Novatus Makunga

20th December 2009

headline_bullet.jpg
Atakayesogelea eneo lao kuligawa kukiona
headline_bullet.jpg
Wasema JK alishawapa mashamba hayo

Barbaig.jpg

Makundi ya jamii ya wafugaji wa kibarbaig yakiibuka kutoka msituni tayari kupambana na atakayevamia eneo lao.

Wafugaji wa kabila la Wabarbaig katika kijiji cha Mogitu na vijiji vya jirani, wametangaza vita kupambana na yeyote atakayeingia katika eneo hilo kwa lengo la kuligawa upya.
Kama njia ya kujilinda na kujihami, wafugaji hao wamejipanga kwenye makundi na kujificha katika moja ya mlima kijijini hapo kupambana na atakayethubutu kuingia kwa ajili ya zoezi la kuligawa upya eneo wanalodai lilishatengwa kwa ajili ya malisho ya mifugo.
Sakata hilo linatokana na mashamba yaliyokuwa yakimilikiwa na Shirika la Chakula na Kilimo (Nafco), yaliyopo eneo la Basotu ambayo mwaka 2006 serikali iliyaachia kwa ajili ya kugawiwa kwa wananchi.

Wananchi hao ambao pia wanatoka katika vijiji vya Ming’enyi na Gidagamu wanapinga kile kinachoonekana kutaka kumegwa kwa eneo lililotengwa kwa ajili ya ufugaji ili kuwapatia maeneo wananchi walioondolewa katika mlima Hanang.

Nipashe imeshuhudia maelfu kwa maelfu ya Wabarbaig wazee kwa vijana waliogawanyika katika makundi ya watu wasiozidi 200 kila moja likiwa na kiongozi wake, wakiwa na silaha za jadi yaani mikuki, pinde na sime wakiibuka katika mlima Kujo.

Taarifa zilizopatikana katika eneo hilo lililopo umbali wa kilomita takribani 50 kutoka katika mji wa Katesh ambao ndiyo makao makuu ya Wilaya ya Hanang, zilisema kuwa Jumatatu iliyopita wafugaji hao waliwakurupusha maofisa waliokwenda katika eneo hilo kwa ajili ya zoezi la upimaji.

Kamanda wa Polisi mkoani Manyara, Parmena Sumario, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo alisema walilazimika siku ya pili yake kumkamata Mwenyekiti wa kijiji cha Mogitu, Israel Dawi na watu wengine 16 ambao inawashikilia.

Kiongozi wa kimila kwa upande wa vijana, Mangi Gidagurenda, alisema kuwa hadi kufikia juzi ni siku ya nne wanalala nje ya nyumba zao kwa lengo la kulinda ardhi yao isichukuliwe na wapo tayari kwa mapambano na polisi.

“Mimi hapa nilipo ni miongoni mwa wanaotafutwa na polisi kukamatwa lakini tumejizatiti kupambana nao mpaka mtu wa mwisho kamwe hatutakubali kuonewa na kunyang’anywa ardhi yetu,” alisema.

Alishangazwa na hatua ya polisi kuwakamata wenzao wanaotetea haki akiwemo mwenyekiti wa kijiji cha Mogitu na kueleza kuwa wanajiandaa kuandamana hadi polisi wilayani Hanang kujua kulikoni.

Kijana wa Kibarbaig, Herje Giter, alisema anashangazwa na uongozi wa Wilaya ya Hanang kuingilia upya suala la ugawaji wa eneo hilo ambao ulishakamilika na maeneo kutengwa kwa shughuli za ukulima na ufugaji.

“Mheshimiwa Jakaya Kikwete alishatoa mashamba hayo kwa nia nzuri kwa wananchi sasa hawa viongozi wanataka kuharibu nia nzuri ya mheshimiwa Rais,” alisema Giter.
Gidambusa Mwarja, alisema kuwa wananchi wa maeneo hayo walishazoea kuwekwa mahabusu katika magereza tangu mwanzo mwa miaka 80 wakati serikali ilipowapokonya mashamba hayo na kuanzisha mradi wa Nafco kwa hiyo hawatashindwa kutumia nguvu ili kuhakikisha ardhi yao haimegwi.

"Tumejiandaa kwa lolote litakalojitokeza na wote tayari tumeshaandika urithi wa mali zetu kwani mwanaume lazima afe na mali yake na sisi ardhi ni mali yetu lazima tuipiganie," alisema.

Alidai kuwa kuwepo kwa watu kutoka mlima Hanang kunatumiwa tu kuwahalalisha wafanyabiashara na watu kutoka maeneo mbalimbali kwani wanadai wengi walishagawiwa na kuyauza maeneo hayo.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Hanang alipopigiwa simu ili kutoa ufafanuzi alikuwa mbogo.
“Watafuteni hao hao waliowaleta huku na kuwapa taarifa za huo mgogoro mimi siko tayari kuzungumzia ujinga huo nina kazi nyingi,” alisema Ligubi na kukata simu.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Hanang alivyofuatwa ofisini kwake alikataa kutoa ufafanuzi kwa madai hatakuwa tayari kuzungumza mpaka atakapokuwa na Mkuu wa Wilaya Lugubi.

Mkuu wa mkoa wa Manyara, Henry Shekifu, alisema kuwa yupo katika mkutano Mwanza hata hivyo katika vikao vilivyopita vilivyowashirikisha pia viongozi wa vijiji hivyo walikubaliana kuwa sehemu ya eneo lililotengwa kwa mifugo limegwe kwa ajili ya wananchi.
“Kwa kweli hali ni mbaya mimi nitapita kwenda kuzungumza na hao wananchi lakini nashangaa kama hata wenyeviti wa vijiji wanaongoza hali hiyo wakati nao tulikubaliana katika vikao,” alisema Shekifu.

Katika mpango wa awali chini ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo kapteni mstaafu John Ngatuni, halmashauri ilipitisha mgawo wa kutenga ekari 500 kwa ajili ya kuhifadhi kwa matumizi mbalimbali yakiwemo ya uwekezaji na kugawa ekari 6000 kwa wakulima na kiasi kingine kama hicho kwa wafugaji.

CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

http://www.ippmedia.com/


0 Maoni | Kuwa wa kwanza kutoa maoni
 
Labda hii ndiyo lugha mafisadi wanaweza kuielewa.Now, kama kila Mtanzania angekuwa na spirit hii katika kulinda maslahi yake, na kupiga kura kwa interests zake na za nchi, labda tungekuwa mbali.
 
Wabarbaig watangaza vita

Na Novatus Makunga

20th December 2009

headline_bullet.jpg
Atakayesogelea eneo lao kuligawa kukiona
headline_bullet.jpg
Wasema JK alishawapa mashamba hayo

Barbaig.jpg

Makundi ya jamii ya wafugaji wa kibarbaig yakiibuka kutoka msituni tayari kupambana na atakayevamia eneo lao.

Wafugaji wa kabila la Wabarbaig katika kijiji cha Mogitu na vijiji vya jirani, wametangaza vita kupambana na yeyote atakayeingia katika eneo hilo kwa lengo la kuligawa upya.
Kama njia ya kujilinda na kujihami, wafugaji hao wamejipanga kwenye makundi na kujificha katika moja ya mlima kijijini hapo kupambana na atakayethubutu kuingia kwa ajili ya zoezi la kuligawa upya eneo wanalodai lilishatengwa kwa ajili ya malisho ya mifugo.
Sakata hilo linatokana na mashamba yaliyokuwa yakimilikiwa na Shirika la Chakula na Kilimo (Nafco), yaliyopo eneo la Basotu ambayo mwaka 2006 serikali iliyaachia kwa ajili ya kugawiwa kwa wananchi.

Wananchi hao ambao pia wanatoka katika vijiji vya Ming’enyi na Gidagamu wanapinga kile kinachoonekana kutaka kumegwa kwa eneo lililotengwa kwa ajili ya ufugaji ili kuwapatia maeneo wananchi walioondolewa katika mlima Hanang.

Nipashe imeshuhudia maelfu kwa maelfu ya Wabarbaig wazee kwa vijana waliogawanyika katika makundi ya watu wasiozidi 200 kila moja likiwa na kiongozi wake, wakiwa na silaha za jadi yaani mikuki, pinde na sime wakiibuka katika mlima Kujo.

Taarifa zilizopatikana katika eneo hilo lililopo umbali wa kilomita takribani 50 kutoka katika mji wa Katesh ambao ndiyo makao makuu ya Wilaya ya Hanang, zilisema kuwa Jumatatu iliyopita wafugaji hao waliwakurupusha maofisa waliokwenda katika eneo hilo kwa ajili ya zoezi la upimaji.

Kamanda wa Polisi mkoani Manyara, Parmena Sumario, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo alisema walilazimika siku ya pili yake kumkamata Mwenyekiti wa kijiji cha Mogitu, Israel Dawi na watu wengine 16 ambao inawashikilia.

Kiongozi wa kimila kwa upande wa vijana, Mangi Gidagurenda, alisema kuwa hadi kufikia juzi ni siku ya nne wanalala nje ya nyumba zao kwa lengo la kulinda ardhi yao isichukuliwe na wapo tayari kwa mapambano na polisi.

“Mimi hapa nilipo ni miongoni mwa wanaotafutwa na polisi kukamatwa lakini tumejizatiti kupambana nao mpaka mtu wa mwisho kamwe hatutakubali kuonewa na kunyang’anywa ardhi yetu,” alisema.

Alishangazwa na hatua ya polisi kuwakamata wenzao wanaotetea haki akiwemo mwenyekiti wa kijiji cha Mogitu na kueleza kuwa wanajiandaa kuandamana hadi polisi wilayani Hanang kujua kulikoni.

Kijana wa Kibarbaig, Herje Giter, alisema anashangazwa na uongozi wa Wilaya ya Hanang kuingilia upya suala la ugawaji wa eneo hilo ambao ulishakamilika na maeneo kutengwa kwa shughuli za ukulima na ufugaji.

“Mheshimiwa Jakaya Kikwete alishatoa mashamba hayo kwa nia nzuri kwa wananchi sasa hawa viongozi wanataka kuharibu nia nzuri ya mheshimiwa Rais,” alisema Giter.
Gidambusa Mwarja, alisema kuwa wananchi wa maeneo hayo walishazoea kuwekwa mahabusu katika magereza tangu mwanzo mwa miaka 80 wakati serikali ilipowapokonya mashamba hayo na kuanzisha mradi wa Nafco kwa hiyo hawatashindwa kutumia nguvu ili kuhakikisha ardhi yao haimegwi.

"Tumejiandaa kwa lolote litakalojitokeza na wote tayari tumeshaandika urithi wa mali zetu kwani mwanaume lazima afe na mali yake na sisi ardhi ni mali yetu lazima tuipiganie," alisema.

Alidai kuwa kuwepo kwa watu kutoka mlima Hanang kunatumiwa tu kuwahalalisha wafanyabiashara na watu kutoka maeneo mbalimbali kwani wanadai wengi walishagawiwa na kuyauza maeneo hayo.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Hanang alipopigiwa simu ili kutoa ufafanuzi alikuwa mbogo.
“Watafuteni hao hao waliowaleta huku na kuwapa taarifa za huo mgogoro mimi siko tayari kuzungumzia ujinga huo nina kazi nyingi,” alisema Ligubi na kukata simu.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Hanang alivyofuatwa ofisini kwake alikataa kutoa ufafanuzi kwa madai hatakuwa tayari kuzungumza mpaka atakapokuwa na Mkuu wa Wilaya Lugubi.

Mkuu wa mkoa wa Manyara, Henry Shekifu, alisema kuwa yupo katika mkutano Mwanza hata hivyo katika vikao vilivyopita vilivyowashirikisha pia viongozi wa vijiji hivyo walikubaliana kuwa sehemu ya eneo lililotengwa kwa mifugo limegwe kwa ajili ya wananchi.
“Kwa kweli hali ni mbaya mimi nitapita kwenda kuzungumza na hao wananchi lakini nashangaa kama hata wenyeviti wa vijiji wanaongoza hali hiyo wakati nao tulikubaliana katika vikao,” alisema Shekifu.

Katika mpango wa awali chini ya aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo kapteni mstaafu John Ngatuni, halmashauri ilipitisha mgawo wa kutenga ekari 500 kwa ajili ya kuhifadhi kwa matumizi mbalimbali yakiwemo ya uwekezaji na kugawa ekari 6000 kwa wakulima na kiasi kingine kama hicho kwa wafugaji.

CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

http://www.ippmedia.com/


0 Maoni | Kuwa wa kwanza kutoa maoni





Madhara ya kutosoma na kutambua wajibu wao kama raia wa nchi. Sheria inasema ardhi ni mali ya serikali na rais ni mdhamini mkuu,hivyo matumizi yake yanaweza kubadilishwa wakati wowote,after all wanaogaiwa ardhi hiyo ni watanzania wenzao kama huo si upumbavu ni nini? wanawaza ng'ombe tu badala ya kuuza wakawa matajiri na kubaki na mifugo michache wamekalia ujinga wacha wanyang'anywe.
 
Companero;vita vimezuka ama vimetangazwa?Na ni kivipi hiyo ni Guerilla war?
 
Madhara ya kutosoma na kutambua wajibu wao kama raia wa nchi. Sheria inasema ardhi ni mali ya serikali na rais ni mdhamini mkuu,hivyo matumizi yake yanaweza kubadilishwa wakati wowote,after all wanaogaiwa ardhi hiyo ni watanzania wenzao kama huo si upumbavu ni nini? wanawaza ng'ombe tu badala ya kuuza wakawa matajiri na kubaki na mifugo michache wamekalia ujinga wacha wanyang'anywe.

Hiyo sheria yenyewe ni ya kidhalili na haina tofauti na ukoloni.

Kati ya sheria zinazozuia maendeleo Tanzania kwa sana ni hii sheria ya yenye nature ya eminent domain.

Serikali yenyewe haieleweki, upande mmoja inaonyesha kujiondoa katika eminent domain like laws kwa kuwarudishia watu majumba yaliyotaifishwa, upande mwingine inawaingilia indigenous people bila proper compensation, lazima kuwe na zali ukizingatia watu wenyewe moto chini hao.

Halafu tunalalamika hatuna uwekezaji, na eminent domain kama za Eva Morales zote hizi? Kwa nini wawekezaji wasiende Kenya kwenye sheria ya ardhi iliyo more investor friendly? Angalau wakenya wamechagua kuwa mabepari na hilo linajulikana.Hata "bwana" amesema atawatapika wale wenye uvuguvugu.
 
Madhara ya kutosoma na kutambua wajibu wao kama raia wa nchi. Sheria inasema ardhi ni mali ya serikali na rais ni mdhamini mkuu,hivyo matumizi yake yanaweza kubadilishwa wakati wowote,after all wanaogaiwa ardhi hiyo ni watanzania wenzao kama huo si upumbavu ni nini? wanawaza ng'ombe tu badala ya kuuza wakawa matajiri na kubaki na mifugo michache wamekalia ujinga wacha wanyang'anywe.

Na hiyo mikuki yao sidhani kama wataweza mudu AK47 zikiingia. Hawa jamaa wana utani mmbaya hekari 6000 warande tu na n'gombe.

Wana haki ya kuendendekeza mila zao za ajabu lakini not to the tune of 6000 acres. Hila sio ardhi tena akapewe muarabu kama ni hivyo bora waichezee tu hawa wazawa.
 
Na hiyo mikuki yao sidhani kama wataweza mudu AK47 zikiingia. Hawa jamaa wana utani mmbaya hekari 6000 warande tu na n'gombe.

Wana haki ya kuendendekeza mila zao za ajabu lakini not to the tune of 6000 acres. Hila sio ardhi tena akapewe muarabu kama ni hivyo bora waichezee tu hawa wazawa.


JC:

Mi naona ipitishwe sheria ya kuanzisha tribal areas or reservations hili watu wanaopenda kubakia kwenye jadi zao wabakie huko.
 
Kama ni kweli basi katika vita hivi kuna ulazima wa serikali kukomesha mapigano haya kila sehemu huko Hanang
 
JC:

Mi naona ipitishwe sheria ya kuanzisha tribal areas or reservations hili watu wanaopenda kubakia kwenye jadi zao wabakie huko.

Mkuu

huko si ndio kule tunakosema kuwaendekeza na ndoto zao za upuuzi. Solution ni kuwafanya waelewe times have changed. Siku hizi kuna sheria za nchi ambazo zina apply kwenye ardhi. Sheria ambazo zita affect traditions zao kama wanavyotoka.

Lakini ukweli wenyewe its impractical in our times mfano angalia in the amazon na haya mambo ya madini na mafuta. Whenever land has other economical benefits ni lazima itumiwe ku maximize the welfare of the whole. Na hawa wenzano tena ni settlers ambao inabidi wasogezwe. Hiwe hawa wanaotaka ya kuzurura it dosent make sense.

Sasa angalia na eskimos hau hata huku kwetu UK everyday protesters wanagombana na developers kuhusu kuchukua ardhi ukweli wenyewe there is a demand for new housing therefore open land is needed.

Itakua hawa jamaa ni lazima wabadilike tu; kwani its not about their lifestyle but reality of life. its impossible for them to contine like that for two more generations even in Tanzania.

Kwa hivyo kuwasaidia ni namna moja tu lazima wa accept reality that is; our Laws and who has the final say kwenye ardhi ya nchi. Hila serikali itafute mbinu ya kubadilisha mawazo ya hawa watu taratibu taratibu.
 
Labda hii ndiyo lugha mafisadi wanaweza kuielewa.Now, kama kila Mtanzania angekuwa na spirit hii katika kulinda maslahi yake, na kupiga kura kwa interests zake na za nchi, labda tungekuwa mbali.
Nimejifunza kuwa haya mambo madogo madogo yanayoendelea huwa yanabeba alama ya kubwa ambalo madogo yanalitengeneza kama tutaendelea kuyadharau. We better watch out!
 
Companero;vita vimezuka ama vimetangazwa?Na ni kivipi hiyo ni Guerilla war?

Watu wanapolala msituni kama Mau Mau. Tena kwenye makundi madogomadogo yaliyojificha na silaha za kumshutukiza adui. Basi ujue vita ya msituni imeshazuka.
 
Haya matamshi yakishakaa vichwani mwa watu mhh...:mad:

Pale itakapoonekana hayo(kwenye kichwa cha habari) yatanufaisha/yatatatua mgogoro uliopo-haitakuwa vigumu wengine wakafuata mfano huo. Hatutaki kwenda huko.

I miss JFVILLE:D
 
Juma Contena na Zakumi tunawajua kuwa ninyi mna chuki binafsi na jamii za wafugaji. Hizi ndio chuki zinazosababisha haya matatizo yote. Mnaona sawa wawekezaji wa jatrofa kupewa ekari zetu laki 6 ila taabu kwa Wabarbaig kubaki na ekari zao elfu 6! Alafu Zakumi unadai waandaliwe eneo la kuwahifadhi wa na jadi zao, sasa hiyo ina tofauti gani na kuwaacha waishi maisha yao ya transhumansi huko Hanang? Ninyi kama mmeshindwa kuishi kwa kufuga na kulima huku endeleeni tu kubeba maboksi huko! Ardhi ni mali ya Umma!
 
Watu wanapolala msituni kama Mau Mau. Tena kwenye makundi madogomadogo yaliyojificha na silaha za kumshutukiza adui. Basi ujue vita ya msituni imeshazuka.

Mkuu ni kweli kuhusu characteristic ya makundi madogo madogo na yenye kumshtukiza adui,lakini Guerilla warfare siyo lazima viwe vita vya msituni,Ambush and raid/Fight and run away to fight another day ndiyo nguzo ya guerilla tactics,inaweza ikawa urban na still a guerilla warfare...Kwahiyo sidhani kama vita vya msituni ndio guerilla war....May be the other way round,i stand to be corretcted.
 
Mkuu ni kweli kuhusu characteristic ya makundi madogo madogo na yenye kumshtukiza adui,lakini Guerilla warfare siyo lazima viwe vita vya msituni,Ambush and raid/Fight and run away to fight another day ndiyo nguzo ya guerilla tactics,inaweza ikawa urban na still a guerilla warfare...Kwahiyo sidhani kama vita vya msituni ndio guerilla war....May be the other way round,i stand to be corretcted.
Sifa kuu ya guerilla war (vita ya msituni) ni kupiganwa kwa kushtukiza au kuvizia. Haingalii ni wapi vita inapiganwa: mjini au msituni. Ikiwa na tabia ya kuvizia inakuwa guerilla war hata kama inapiganwa mjini, kinyume na conventional war. Kumbe hicho wanachotaka kukifanya wabarbaig ni guerilla war kwa sababu wamejificha wakivizia adui yao wamshukie kwa nguvu ghafla.
 
Sifa kuu ya guerilla war (vita ya msituni) ni kupiganwa kwa kushtukiza au kuvizia. Haingalii ni wapi vita inapiganwa: mjini au msituni. Ikiwa na tabia ya kuvizia inakuwa guerilla war hata kama inapiganwa mjini, kinyume na conventional war. Kumbe hicho wanachotaka kukifanya wabarbaig ni guerilla war kwa sababu wamejificha wakivizia adui yao wamshukie kwa nguvu ghafla.

Kinachofanya guerilla war iitwe guerilla war ni msitu ama tactics?Ina maana kwamba hiyo ya wabarbaig ni guerilla war kwasababu ni "vita ya msituni?"
Ndio maana nikauliza endapo ni kweli vita vya msituni si lazima viwe guerilla warfare and vice versa.
 
Wafugaji hawa wana haki ya kupewa (in fact kurudishiwa) maana walinyang'anywa na serikali enzi zile za nafco

Kama serikali lazima ifahamu kuwa wafuagaji wanahaitaji ardhi kubwa kwakuwa mifugo yao ni makundi makubwa na yanayotambaa na kutembea (ufugaji wa kienyeji)

Bado mahitaji ya nyama ni makubwa na soko lake ni ndani na nje kuwabughuzi hawa wafuagaji ni kuonyesha kuwa hatuthamini mchango wao mkubwa kabisa katika pato la Taifa.
 
Mkuu

huko si ndio kule tunakosema kuwaendekeza na ndoto zao za upuuzi. Solution ni kuwafanya waelewe times have changed. Siku hizi kuna sheria za nchi ambazo zina apply kwenye ardhi. Sheria ambazo zita affect traditions zao kama wanavyotoka.

Lakini ukweli wenyewe its impractical in our times mfano angalia in the amazon na haya mambo ya madini na mafuta. Whenever land has other economical benefits ni lazima itumiwe ku maximize the welfare of the whole. Na hawa wenzano tena ni settlers ambao inabidi wasogezwe. Hiwe hawa wanaotaka ya kuzurura it dosent make sense.

Sasa angalia na eskimos hau hata huku kwetu UK everyday protesters wanagombana na developers kuhusu kuchukua ardhi ukweli wenyewe there is a demand for new housing therefore open land is needed.

Itakua hawa jamaa ni lazima wabadilike tu; kwani its not about their lifestyle but reality of life. its impossible for them to contine like that for two more generations even in Tanzania.

Kwa hivyo kuwasaidia ni namna moja tu lazima wa accept reality that is; our Laws and who has the final say kwenye ardhi ya nchi. Hila serikali itafute mbinu ya kubadilisha mawazo ya hawa watu taratibu taratibu.

Labda tumuulize Sanctus Msimbe na TPN wao wangelishughulikia vipi jambo hili ukizingatia wametoka wkenye kongamnao linalohusu Vipaumbele vya Kitaifa katika kujenga Uchumi Imara.

Ni vipi tunaposema waende na wakati, tunaweza kuwaelimisha wakaondokana na mila na jadi zao na kuwafanya waendane na mkao wetu tunaodai ni wa kisasa na kimaendeleo?
 
JMushi1 hiyo ni tafsiri yangu, nilikuwa natafuta neno la kiswahil na lililonijia ndio hilo la vita ya msituni - utakuwa umenisaidia sana kama utaleta tafsiri rasmi ya 'guerilla war'.
 
Back
Top Bottom