Mkuu Mungi, tatizo ni yeye au waliotunga hiyo sheria?? unajua kuna sheria nyingine zikitekelezwa tutakuwa wakimbizi??
Nafikiri hana kosa. Wenye makosa ni wabunge tuliowatuma watuwakilishe kuipitisha hiyo sheria mbovu na kandamizi. Sasa unaweza kuelewa ni kwa nini kila kona ya nchi ni ufisadi na mikataba mibovu
Watanzania tunashuhudia kulewa kwa madaraka kwa chombo hiki ambacho kimeshindwa kudhibiti ubadhirifu uliokithiri katika mifuko ya hifadhi ya jamii na badala yake kuwageukia wachangiaji na kutaka kuwadhiti bila hata kuwajua. Hivi mnajua tofauti ya wachangiaji wa mifuko hii? Mfano mdogo tu hivi hii sheria ilifikiria athari yake kwa makundi mbalimbali yaliyotofauti?
Mimi nina mkataba wa kazi wa miaka miwili kuishia Dec 2012.
Baada ya hapo sina kazi nilitegemea nichukue mchango wangu unisaidiekatika kujikimu mpaka nitakapopata kazi nyingine au nijiajiri mwenywe kwa kuwekeza pesa hii. Unaposema nisubiri nifikie umri wa miaka 55 unampango gani wa kunihudumia na kujikimu?
Je, unaniahidi kazi kwa miaka iliyobaki hadi miaka 55?
Huu ni mfano mmoja tu katika mingi ya kuonesha kuwa mmekurupuka katika sharia hii na kwa bahati mbaya wabunge wetu waliishia kurebisha spelling na semantics badala ya content na construction ya sheria yenyewe.
Tumewasikia mkianza kunywea kwa wafanyakazi wa migodii lakini jueni wao ni 'tip of iceberg
Katika hili sina wasiwasi kuwa serikali msipolishughulikia kwa haraka na kusitisha sheria hii kwa ujumla wake mtakuwa mnachezea ukomo wa uvumilivu wetu ambao nadiriki kusema hamuujui
Watanzania tunashuhudia kulewa kwa madaraka kwa chombo hiki ambacho kimeshindwa kudhibiti ubadhirifu uliokithiri katika mifuko ya hifadhi ya jamii na badala yake kuwageukia wachangiaji na kutaka kuwadhiti bila hata kuwajua. Hivi mnajua tofauti ya wachangiaji wa mifuko hii? Mfano mdogo tu hivi hii sheria ilifikiria athari yake kwa makundi mbalimbali yaliyotofauti?
Mimi nina mkataba wa kazi wa miaka miwili kuishia Dec 2012.
Baada ya hapo sina kazi nilitegemea nichukue mchango wangu unisaidiekatika kujikimu mpaka nitakapopata kazi nyingine au nijiajiri mwenywe kwa kuwekeza pesa hii. Unaposema nisubiri nifikie umri wa miaka 55 unampango gani wa kunihudumia na kujikimu?
Je, unaniahidi kazi kwa miaka iliyobaki hadi miaka 55?
Huu ni mfano mmoja tu katika mingi ya kuonesha kuwa mmekurupuka katika sharia hii na kwa bahati mbaya wabunge wetu waliishia kurebisha spelling na semantics badala ya content na construction ya sheria yenyewe.
Tumewasikia mkianza kunywea kwa wafanyakazi wa migodii lakini jueni wao ni 'tip of iceberg
Katika hili sina wasiwasi kuwa serikali msipolishughulikia kwa haraka na kusitisha sheria hii kwa ujumla wake mtakuwa mnachezea ukomo wa uvumilivu wetu ambao nadiriki kusema hamuujui
Huu ni ufedhuli na kiburi cha hali ya juu.Mlaaniwe wote mnaotaka kuangamiza maisha ya watanzania.
Tatizo Irene alikuwa wa kwanza kujishebedua kwenye vyombo vya habari!
Mtu mmoja wa SSRA akiuawa ndiyo serikali itajua kuwa wafanyakazi hawana utani
Tuingie maporini tu sasa
Mkuu mimi naona tunawaonea SSRA, Kwani wao wanatakeleza sheria iliyotungwa na wawakilishi wetu! Tuwe makini kuachagua wabunge, Tukiendelea kuchagua watu wanapitisha na kuunga mkono 100/100 matokeo yake ndiyo haya Mkuu!
Serikali ya chama Tawala CHUKUA CHAKO MAPEMA
Wakuu,
Hivi huyu mama Irene Isaka wa SSRA ni nani? Ametokea wapi? Amesoma wapi na kasomea nini? Asante.
Huyo Irene ana kiherehere
Si yeye ndo alisema tumeshindwa kumanage 90% ya hela yetu hiyo 10% itatusaidia nini?
kasahau kama bado kuna 35% PAYE kwenye hiyo 90% anayoisema...
Katika kile kinachoonekana kama kelele za mpita njia hazimzuii mwenye nyumba kulala Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii-SSRA imesema haishtushwi na kelele zinazopigwa na wafanyakazi kote nchini kuhusu sheria mpya inayopiga marufuku wafanyakazi kuchukua stahiki zao wanapostaafu hadi wafikishe miaka 55 na badala ya ke imesema tayari sheria hiyo mpya imeanza kutumika tangu Julai 20.
Taarifa iliyotolewa jana jijini Dar es Salaam na kitengo cha Mawasiliano na Uhamasishaji cha SSRA, imefafanua kuwa sheria hiyo imeshaanza kutumika na maombi mapya ya kujitoa yamesitishwa kwa kipindi cha miezi sita hadi muongozo mwingine utakapotolewa.
Ilibainisha kuwa lengo la kusitisha maombi ya kujitoa uanachama ni mamlaka na mifuko ya hifadhi ya jamii kutoa elimu kwa wadau ambao ndio wanachama wa sekta hiyo.
Taarifa hiyo ilisema wamesitisha fao la kujitoa si kwa sababu ya serikali au mifuko ya hifadhi kufilisika kama baadhi ya watu wanavyodai bali inalenga kuboresha maslahi ya wanachama.
Tunapenda kuwahakikishia wanachama kuwa mifuko ya hifadhi ya jamii ni thabiti na michango yote ya wanachama iko salama.
Tunawaomba wanachama na wadau wote wa sekta ya Hifadhi ya Jamii kuwa na utulivu mchakato huu ukiwa unaendelea kwa lengo la kulinda na kutetea maslahi ya wanachama, ilisema.
Source:Tanzania Daima
tetsi hakuna ila hisia zinaonesha mishale kuwa hapa lazima kuna njama tena kali. Ufujaji wa mifuko ya jamii huenda kikawa chanzo . Kwanza hata wale wastaafu tujiulize wamepata hela zao maana kipindi fulani kulikuwa na manung'uniko kuwa mifuko imefilisiwa na rz1 kwa mkono wa baba yake sasa sijui hisia kama ni za kwlei au la.ndugu wana jf kuna dhana mbalimbali zimeibuka juu ya sababu ya mabadiliko ya sheria ya mafao ya kujitoa,dhana hizi ni
1.inasemekana nssf na ppf wanajiandaa kuwachotea ccm fedha za kampeni 2015
2.inasemekana baada ya serikali kukopa fedha nyingi kwenye haya mashirika yaani nssf na ppf sasa yanaelekea kufilisika.wadau km kuna yeyote ana tetesi zaidi aziweke ili zitusaidie kuwaeleza watz wengi zaidi.
Nawasilisha
Huyo Irene ana kiherehere
Si yeye ndo alisema tumeshindwa kumanage 90% ya hela yetu hiyo 10% itatusaidia nini?
kasahau kama bado kuna 35% PAYE kwenye hiyo 90% anayoisema...
Na ingine 8% ya Bodi ya Mikopo! Du nitakufa na mtu