Sangarara
JF-Expert Member
- Sep 29, 2011
- 13,100
- 5,649
Wapaka rangi pamoja na wanaowasafisha wanaume kwenye salon wote mi siwafagilii. Haina maana kuwa situmii huduma yao...natumia ila kwa uangalifu bila kuchangia vifaa.
Kinachonishangaza nimeshashuhudia wamama wanaweka miguu kwenye mapaja ya hawa jamaa infront of their husbands...hasa hawa wanaopita kwenye mabaa kutoa hiyo huduma. Mimi siwezi aisee...ntafanya hivyo salon nikijua mume wangu hanioni. Lol....na najijua kuwa mi mgumu hivyo mpaka rangi ataishia ku massage miguu hapati kitu.
Same kwa mume wangu...kuna siku nilimsindikiza akakate nywele...nilichokifanya nilibaki kwenye gari kwa kuwa sitaweza kuvumilia kuona wadada wana mscrub...wadada wa salon walipotoka nje wakakuta nimejaa kwenye gari...nadhani walishangaa kwa nini sikushuka..wale wako kibiashara zaidi kama wauza baa...ukinogewa wanakugeuza buzi.
Hata masalon ya kike ambayo wahudumu ni wanaume ...wanapenda sana kutega wake za watu, wakikuona umekuja na usafiri wa maana wanatamani kukugeuza sugar mummy...nshawasoma sana.
Kikubwa ni kutokuwa na mazoea na hao wote...wewe ni mteja na unalipia service...hakuna story za sijuhi unakaa wapi? Unafanya kazi gani? Sipendi mazoea kabisa yasiyokuwa na sababu.
Ili kujiepusha na vishawishi ni ku stay away from opposite sex. Hakuna dawa zaidi ya hiyo.
Ukubwa dawa!! na Macamera man je? nawakumbuka taratibu.