Hawa Ndio Mawaziri wa JK; Waziri Mwinyi asema kwa sasa Madaktari bingwa si muhimu!!!

Anaweza kuwa amekosea kujieleza, lakini kimsingi tunahitaji uwiano wa madaktari bingwa na madaktari wa ngazi za chini

Katika nchi ambayo dispensary nyingi za vijijini hazina hata maBwana Afya, kuwekeza kwenye madaktari bingwa pekee hakuna maana kwa sababu watu wengi mno wanakufa kwa maradhi ya kawaida ambayo yangesaidiwa kwa kuwepo madaktari wa ngazi ya chini.

Pia, bila ya kuwepo kwa madktari wa ngazi ya chini, wagonjwa hawataweza kuandikiwa kuonana na daktari bingwa, hivyo huduma ya hawa madaktari bingwa itakuwa kwa wachache zaidi

Kwa hiyo hapa ni suala la uwiano. Tunahitaji kusomesha madaktari wa ngazi ya chini wa ngapi kwa kila daktari bingwa mmoja?
 
mwinyi ni daktar bingwa aliyesomea ugiriki..unfortunantly he z not accustomed with local figures(fees..etc)bt he knwz kusomesha dr bingwa its too expensive bcoz yeye ni dr bingwa..

Empty headed.......yaaan ye kasoma halafu kwa wengine ndo iwe expensive????? Kama hiyo hela ingekuwa inafundisha mtu kuja kushona kandambili sawa.........mtu daktari bingwa uanategemea asome kwa ada ya chini?????? Isn't life the most expensive thing????? Na unaunga mkono ....eti ya kasomea Ugiriki.....sooooo??????


Hiyo red unamaanisha nini??? Kwani mshara wake upo kwa currency gani??????
 
huyu waziri yupo tayari kupeleka mtoto,mke au mzazi wake kwenye hospitali isiyo na daktari bingwa? Labda kupima malaria..... Sasa wananchi watakua wanaenda kwenye mahospitali kupima urefu, uzito, BP na malaria tu? katika jitihada za serikali kuhalalisha msimamo wake dhidi migomo ya madaktari na walimu , wanaishia kuongeza msuguano kati yao na wanataaluma...
 
Ukisomesha daktari bingwa inabidi umpe vifaa bingwa ili afanye kazi bingwa. Ukisomesha daktari bingwa bila kumpa vifaa bingwa matokeo ni migomo tu. By the way, kurugenzi ya mafunzo wizara ya afya ndiyo inayotengeneza vipaumbele vya mafunzo, kurugenzi hiyo inaongozwa na madaktari.

Pro diaspora.....ndo mawazo yenu haya huwa uzalendo kwenu ni zero........sequential events
 
Ukisomesha daktari bingwa inabidi umpe vifaa bingwa ili afanye kazi bingwa. Ukisomesha daktari bingwa bila kumpa vifaa bingwa matokeo ni migomo tu. By the way, kurugenzi ya mafunzo wizara ya afya ndiyo inayotengeneza vipaumbele vya mafunzo, kurugenzi hiyo inaongozwa na madaktari.

Pro diaspora.....ndo mawazo yenu haya huwa uzalendo kwenu ni zero........sequential events

Mkuu OLESAIDIMU katika nilichoandika hapo ni kipi kilichokosa uzalendo? Au nini ambacho siyo cha ukweli. Ingekuwa vizuri kama tungejenga tabia ya kudeal na hoja badala ya kudeal na majina na maisha ya watu.
 
Last edited by a moderator:
Dr. Mwinyi is out of touch, Baba alikuwa waziri, baadae Rais, nae anabebwa kulipa fadhila za Mzee. Hizi fikra za Mh waziri wa Afya ni sawa na zile za Mh Mponda kuleta Bajaja ambulancy kwa $10000 each na kuzipeleka vijijini.
Kujuana, Takrima na Fadhila zinaliangamiza Taifa letu
 
Mkuu neurosurgery ni superspecialization, hufanywa kwa miaka miwili, isipokuwa anaefanya neurosurgery tayari anakuwa ni specialist, so labda ujumlishe miaka mitatu ya specialization na miwili ya superspecialization ndio inakuwa mitano. Mwinyi alizungumzia specialization, hakuna ya miaka mitano mkuu


Kuwa neurosurgeon ni kuwa mpasuaji wa ubongo na spinal cord, sasa mtu huyu akiamua ku specialize kwenye ubongo au spinal cord pekee ndio superspecialization{fellowship}.

It does not mean that this is super specialization of surgery
 
Sio kosa lake, kwani toka lini wizara ya afya na ustawi wa jamii (Tanzania bara) ikawa ya muungano?
 
Ndugu yangu unashangaa nini? kwani wao na familia zao wanatibiwa hapa bongo? siwanatibiwa INDIA na Ulaya? Kwani madaktari si walisha waeleza kuwa maofisa wa serikali wanalzimisha kupewa rufaa ya kwenda kutibiwa nje hata kwa ugonjwa unaoweza kutibika hapa bongo?wewe unadhani kinachofanya viongozi wakuu wa bongo wawe wanawarithisha na kuwakingia kifua watoto wao akiwemo MWINYI mwenyewe kushika nyadhifa serikalini nini,si ni kutaka kuepukana na huduma dhaifu za jamii zilizosababishwa na uongozi mbaya wa wazazi wao? Nenda shule za kata kama utamkuta hata mtoto wa wa afisa mtendaji wa kijiji,kama hizo ni shule bora watoto wao si ungewaona?
THANKS
































Sasa napata sababu kwa nini serikali haishtuki hata madaktari wakigoma, na pia napata maana ya kauli ya Mizengo Pinda ya Liwalo na Liwe.

Waziri mwenye dhamana ya afya Hussein Mwinyi akihojiwa BBC leo asubuhi na mtangazaji wa kipindi cha haba na haba Noel Mwakalindile ambaye alitaka kujua kauli ya serikali juu ya upungufu wa madaktari bingwa, waziri akasema kwa sasa focus yao kubwa ni kusomesha wataalamu wa afya wa ngazi ya cheti na diploma kwa kuwa wao ndio wanahitajika zaidi. Amesema kusomesha daktari bingwa ni gharama kubwa kwani daktari bingwa anasoma miaka minne mpaka mitano. Kwanza huu ni uzushi, vyuo vyote tanzania madaktari bingwa wa fani zote wanasoma kwa miaka mitatu tu, isipokuwa KCMC ambako wanasoma kwa miaka minne. Hakuna hata chuo kimoja ambacho daktari bingwa anasoma kwa miaka mitano. Hii inanipa wasiwasi kuona kuwa waziri wetu hajui hata madaktari bingwa wanasoma miaka mingapi, Je waziri wa aina hii anawezaje kutuambia anajua gharama ya kumsomesha huyu daktari bingwa?

Hivi kweli huduma bora za afya Tanzania zitaimarika kwa kusomesha maafisa tabibu? Hii serikali inayojali afya ya watu wake inawezaje kweli kuona gharama kusomesha madaktari bingwa na badala yake kusomesha maafisa tabibu. Au inatumia ujinga wa watanzania kwamba mtu yeyote anaevaa koti jeupe ni daktari na hivyo wananchi watajua serikali yao imewapelekea madaktari wakati ni maafisa tabibu ambao tiba yao ni ya huduma ya kwanza?

Nchini kenya kwa sasa madaktari bingwa wako katika ngazi ya hospitali ya wilaya, na wanamkakati wa kuhakikisha kwamba kila mtu anatibiwa na daktari bingwa ili apate tiba ya uhakika na hivyo afya yake kuboreka. Kwetu hata hospitali za rufaa hazina madaktari bingwa wa kutosha achana na hospitali za mikoa ambazo zenye bahati zina bingwa mmoja tu, na tunawaza kuongeza maafisa tabibu. Hivi kwa nini nchi hii badala ya kwenda mbele tunarudi nyuma?

No wonder mwaka jana walipunguza budget ya kusomesha madaktari bingwa na hata wale waliopata udahili walikosa udhamini, nilijua serikali haina pesa kumbe kwa mtazamo wao daktari bingwa si muhimu. Namuomba Hussein Mwinyi akiumwa awe wa kwanza kwenda kwa afisa tabibu kutibiwa aone kama hatapewa ppf injection hata kama ana malaria. Waziri Mwinyi ufikiri kwanza kabla ya kukejeli watanzania.

Naomba kuwakilisha.
 
Hivi mpaka leo hamuamini kua serikali hii ya CCM haipokwa ajili ya wananchi bali ni
kwa ajili yake yenyewe???
hata ikifanya jambo lolote, ni kwa ajili ya kuwazuga wananchi tu ili wazidi kuiweka
madarakani.
waziri gai bwana hata sauti kukaza anashindwa.........!unaatu.
 
nilishasema mimi zamaniiiii, ukiwa mjinga na mpiga domo sana kwa ccm unafaa sana kuwa kiongozi. Kwa hili usishangae mzee ni kawaida sana kwa magamba kupuuza wataalamu. Kwani umesahahu prof Maghembe alipokuwa waziri wa elemu aliposema wanafunzi wa vyuo vikuu wanaotaka computer eti wanatafuta anasa!!!!!!!!!
 
Mkuu OLESAIDIMU katika nilichoandika hapo ni kipi kilichokosa uzalendo? Au nini ambacho siyo cha ukweli. Ingekuwa vizuri kama tungejenga tabia ya kudeal na hoja badala ya kudeal na majina na maisha ya watu.....

Were you pro-his explanation opposed or you were just a neutral observer mkuu.Well you sound offended let me say m sorry for that but as you say let us deal with the issues of which are not hanging in vacuum.

The doers must be along the actions letting these issues on their own makes it difficult to deal with these matters.Tukiwahusisha watendaji na matendo inakuwa mwanzo mzuri wa watu kuwa responsible na matendo na matamshi yao na hiki kimekuwa kichaka kikubwa sana cha watu kujificha kwa kisingizio cha "tujadili mada na sio mtu"

Well we can do that lakini ukweli ni kwamba waanzishaji wa mada, waathirika wa mada husika ni watu hao tunaoshauriwa tusiwahusishe in one way or another.

It is true that we are to follow rules and principles but sometimes exceptions should be considered.

Vivuli vyetu vitatufuata tu, tujiandae kuwa navyo
.
 
Empty headed.......yaaan ye kasoma halafu kwa wengine ndo iwe expensive????? Kama hiyo hela ingekuwa inafundisha mtu kuja kushona kandambili sawa.........mtu daktari bingwa uanategemea asome kwa ada ya chini?????? Isn't life the most expensive thing????? Na unaunga mkono ....eti ya kasomea Ugiriki.....sooooo??????


Hiyo red unamaanisha nini??? Kwani mshara wake upo kwa currency gani??????
hayupo kwenye dunia ambayo we upo...
 
inatisha sana mim naona viongozi wote wakubwa wangenyimwa kutibiwa nje wangeona faida ya madaktari bingwa
 
mzanzibar aliyeshika wizara isiyo ya muungano.

Sio kosa lake hawa wapemba wana matatizo sana na watatuharibia nchi. Huyu bwana kwanza kasoma masomo ya kuunga unga si unajua tena mtoto wa mkubwa . Huko alikotokea na udaktari wake uchwara akaja kuomba kazi Muhimbili wakamtolea nje kaenda kwa Kairuki kwa kushikwa mtoto wa mkubwa maana baba yake ndiye aliyetoa kibali cha Kairuki kuufungua hospital private enzi zile kwwa hiyo wakawa wanalipa fadhira. Udaktari wakuunga kauacha katumbukia siasa . Mtoto kapewa vyeo lukuku si hajabu ndie kiongozi mkuu ajaye . tunategemea nini kwa mpemba kama huyu. Walalamishi hawa watu hawana maana . Kwa hiyo akiongelea mabingwa kutokuwa na muhimu najua ni upeo wake wa kufikiri.
Jamani watu wengine kuwa mawaziri msidhani ni sababu ya bongo kuchemka ni watoto wa mafisadi wnabebwa
 
Huyu kaenda mbali na ukweli, madaktari bingwa wasipotakiwa upasuaji utafanywa na kina nani cuz naona wao ndo wanazifanya sana hizi....ni waTZ wangapi wana uwezo au link za kupelekwa nje ya nchi kutibiwa....inawezekana ile hoja ya Mh Ndugai kwamba kuna waheshimiwa wanachanganyikiwa kwa viroba na msuba ikawa na mashiko kwa kauli kama hizi
 
Lakini tuliwachagua wenyewe tena kwa mbwembwe na ushabiki .....ccm ni no one...nani wa kulaumiwa?
 
Back
Top Bottom