Mbilimbili
Senior Member
- Mar 17, 2012
- 172
- 19
Habari wana jamvi, natumaini mmeshinda vyema. Iko hivi kuna dada mmoja simfaham kiundani, tumefahamiana kwenye mitandao ya kijamii. Yeye anasema yupo Senegal kwenye kambi ya wakimbizi, ila anachotaka kunifanyia naona sivyo. Amenieleza wazazi wake walifariki kutokana na vurugu zilizokuwapo Sudan, kwa hiyo wameacha donge nono la U$D 4.5M kwenye account yao iliyopo London. Sasa kinachonipa wasiwasi ni kwamba amenipa details zote za kufanya Transfer ya hiyo hela, iingizwe kwenye account yangu. Naomba mawazo yenu wadau, sababu nadhani wanataka kuniingiza na mimi kwenye huu mtandao wa kishetani.