Hawa nao ni Adamu na Eva!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,139
Hawa nao ni Adamu na Eva! NDOA, TALAKA NA KUOLEWA TENA
UTANGULIZI

Ndoa ilianzishwa (instituted) na Mungu. Mungu aliumba mke kwa ajili ya Adamu kwa kuwa Mungu aliona “Haikuwa vema” kwa Adamu kuwa peke yake.
Mungu alimuumba mke (Eva) kuwa msaidizi (suitable helper) wa Adamu kutawala dunia, kulea familia na kumuabudu Mungu.
(Mwanzo 2:18, 42)

Ndoa ni mke mmoja na mume mmoja (monogamous).

Mungu alimuumba Eva peke yake kwa ajili ya Adamu na si Eva na Jane, Ingawa Mungu alikuwa na uwezo wa kuumba wanawake wengi kadri anavyoweza ila alimuumba Eva peke yake kwa ajili ya Adamu.
Agano la kale kulikuwa na polygamist na matokeo yake hakukuwa na amani.
(Mwanzo 2:22)

Ndoa ni mke na mume. Biblia haizungumzii kuumbwa kwa Adamu na James au Eva na Linda na kufanya ndoa bali Adamu na Eva.
(Mwanzo 2:22, 1:28)

ndoa inahusisha Mume kuondoka kwa wazazi ili kuanza familia yake kama mke na mume na pia kuna kuwa na taarifa kwa jamii (public recognition) kwamba fulani na fulani ni mke na mume hata kama formalities au tamaduni hutofautiana.

Ndoa inawafunga mke na mume hadi kifo.
Marko 10:9

1Wakorintho 7:39
Warumi 7:2-3

Ndoa inahusisha wajibu wa kila mmoja katika mahusiano kwa mke kutii (submissive) na Mume kumpenda mke wa kujitoa sadaka (sacrificial love)

Efeso 5:22-24, 25-28)


Ndoa huhusisha mume kuwa kichwa cha nyumba au mke kama Kristo alivyo kichwa cha kanisa
Efeso 5:23

1Wakorintho 11:3

Ndoa ni suala zito ni uamuzi wa pili kwa uzito duniani (kwanza ni wokovu na pili ni ndoa) hivyo si kuingia tu kwa kadri unavyijisikia kwani barabara unayoingia ni dead end hakuna kutoka hadi kifo.

Dunia imejaa udanganyifu wa kila aina kuhusiana na suala la ndoa jambo la msingi ni kujua kweli na kweli itakuweka huru.


Unapoingia kwenye ndoa unahitaji kuwa makini, mbele ya safari kujitetea eti nilikuwa bado nina akili ya kitoto, au nilidhani atabadilika au sikuwa na akili timamu au sikujua kama itakuwa hivi haitakusaidia kwani ukiingia ni hadi kifo kitakapowatenganisha hivyo kama hujaoa au kuolewa please be extra carefull siyo unabeba bora liende then kesho unasema “I made a terrible mistake” naweza kuachana naye! hakuna kitu kama hicho.

Ubarikiwe!
 
Can you explain Jacob (Mungu alimpenda hadi kumuita Israel) then? Alioa mtu na dada yake (toka nitoke baba mmoja mama mmoja), alizaa na maids wa wake zake wote na (of all the people) mke wa mwanae but still he is still considered kuwa ni baba wa imani.
 
Mtoboa siri! ngoja nikasali kwanza nikirudi nakujibu swali lako. Ila atakayewahi ajibu mimi nitamalizia!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom