Ledio
Member
- Jun 15, 2011
- 30
- 2
Napenda kutoa kilio changu kwa waziri wa Ofisi ya Rais, Menejiment ya utumishi wa Uma, juu ya mambo wanayotendewa watumishi walioko katika Halmashauri za wilaya. Huwa sipendi kuropoka na nalisema hili kwa ushahidi kwa kuwa sasa nina experience zaidi ya 10yrs nikiwa mtumishi katika Halmashauri hizi. Wakuu Idara katika Halmashauri zetu wamekuwa Miungu watu na pindi mnapofanya ziara katika Halmashauri huwa hampendi kusikiliza watumishi wengine hivyo hampati picha halisi ya manyanyaso wanayopata watumishi hao.