Kiduduye
Member
- Jul 25, 2012
- 10
- 7
Hapo ndo mtakapojua kuwa soka la bongo la majungu, kukomoana, fitina na chuki. Hivi mtu na akili yako kweli unadiriki kufanya ujinga kama huu aliofanyiwa Ngasa? hilo suala dunia nzima hakuna lipo tz tu, na kwa hali hii soka letu halitasogea milele. Mtu kama Geofrey kaburu mtu mwenye heshima zake hawezi kujiaibisha kiasi hiki umewahi kuona wapi mchezaji anauzwa tu kama nyanya au vitunguu vilivyo sokoni. Jambo la msingi ni kwamba pande zote 3 zinatakiwa zikae zikubaliane hapa namaanisha kwamba azam, simba na mrisho ngasa mwenyewe wafikie makubaliano na usajiri wake lakini cha ajabu viongozi wanafanya mkomoeni. Km leo mlisikia michezo ya clouds fm yule katibu wa azam anaongea kama kaladhimisha vile nadhani kisa ni mrisho ngassa kuibusu logo ya yanga, sawa kimichezo ngassa kafanya kosa lakini walitakiwa wamuonye au apewe adhabu kulingana na vifungu vya sheria. Ulishawahi kusikia wapi duniani eti mtu anauzwa kwa mkopo wa pesa kiasi kweli jamani mm naona kuna njama fulani hapa inafanyika ili kumuharibu ngassa kisaikolojia, hata kama ningekuwa ni ndo mchezaji nisingekubali kamwe kulazimishwa kufanya maamuzi hayo cha msingi kama mmeona ngassa hamumtaki tena mnavunja mkataba na mnamlipa pesa yake anakuwa huru kucheza timu yoyote anayoitaka, siyo kwamba eti kisa anaipenda yanga ndo akatae hapana hata kama angekuwa kapelekwa yanga kwa staili kama hii sidhani kama angekubali. Jambo la msingi hapa wadau ni kusapoti vitu vinavyoeleweka na sio unafiki tu eti kisa unaipenda simba ndo usapoti ujinga nakataa katakata. Azam muacheni ngassa afanye maamuzi yeye kama yeye, si mmesikia leo Daniel Agger liverpool wamekubali ofa ya west ham pn mil 19 lakini mchezaji kagoma huo ndo msimamo. Big up kwa wanangu mliogoma kupelekwa kwa mkopo Shamte ally, ramadhani chombo redondo huo ndo ushujaa mohamed banka. Nitashangaa sana kama ngassa akikubali kuchezea simba.