- Kususia FUTARI za kisiasa na za Wamarekani.
VIONGOZI wa dini ya Kiislamu wamejifungia katika Msikiti wa Mtambani wakiandaa tamko muhimu katika historia ya Uislamu nchini.
Shur aya Maimamu imekuwa ikipitia kwa makini kila sentensi na aya zinazokusudia kuwaunganisha Waislamu dhidi ya wale wanaotia vikwazo kwa maendeleo ya dini hiyo na Waisalmu nchini.
Habari toka ndani ya Shura hiyo zinaeleza kwamba maimamu wamevutiwa sana na yule msichana ambaye watu wa umri wa babu zake, baba zake, kaka zake na vijana wenzake wote wanamtongoza kwa siri au bayana lakini yeye kang'gang'ana na silaha moja tu: 'SIDANGANYIKI!' Kwa kuwa Waislamu nchini wamekuwa wakihadaiwa na kila kiongozi anayeingia madarakani masheikh wanataka kuhamasisha Waislamu nchi nzima kukataa katakata tabia ya kudanganywa kama watoto.
Wanadai yapo madai yao na ahadi zilizotolewa na msururu wa viongozi kwamba hiki au kile kitafanywa lakini hakuna kilichofanywa. Kwa sababu hii watawataka Waislamu kutokuwakubali wale ambao kwa namna moja au nyingine wamechangia Waislamu kudanganywa na kuendelea kuchukuliwa kama raia wa daraja la pili katika nchi ambayo babu na nyanya zao ndio waliojitolea kuwa mstari wa mbele kudai uhuru wake.
Haikufahamika kama maimamu hao wakialikwa safari hii na wakubwa wa serikali KULA FUTARI pale IKULU kama watakubali au la. Kwa mujibu wa redio mbao maimamu hao wanadhamira ya kuwatolea nje wale wote watakaojaribu kuwaalika kufuturu ili kujiongezea pointi za kisiasa huku wakiwanyang'anya Waislamu hata kile kidogo walichonacho.