EMT, baada ya kutuhabarisha, ulitakiwa utu update. CC hajapanga ajenda za NEC, hivyo NEC haijakutana leo, itakutana kesho.
HATMA ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba inatarajiwa kujulikana kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho kinachoanza leo. Kikao hicho kinaanza asubuhi hii mjini hapa, huku kukiwa na taarifa kuwa sekretarieti yake huenda ikavunjwa. Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya ndani ya CCM, zinadai kuwa uamuzi huo unachukuliwa ikiwa ni hatua ya chama hicho kujivua gamba linaloonekana kuchuja mbele ya umma.
Chanzo chetu cha habari kilidai kuwa, baada ya kuvunjwa sekretarieti, Makamba ambaye ndiye mwenyekiti wa sekretarieti hiyo, atawasilisha taarifa ya kuomba kustaafu. Hatua hiyo inamwezesha Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kuteua sekretarieti nyingine ambayo itakiongoza hadi mkutano mkuu unatarajiwa kufanyika mwakani.
Zaidi: Hatma ya Makamba CCM kujulikana leo