Karelis ni mchezaji mwenyekipaji kikubwa sana na kamuacha mbali samatta.ila tatizo la karelis si mzuri kwenye kukaba, na hicho ndicho kinachomfanya kocha ampange samatta sana kuliko karelis.Ila kwa sasa inaonekana kocha anataka kutengeneza combination ya karelis na samatta.itakuwa bonge la combination.
Karelis anaonekana ni mzoefu zaidi kuliko Samatta, na pia amezoea sana hiyo ligi, na ana nguvu kuliko Samatta ila Samatta ana kipaji kikubwa sana kuliko huyo Karelis halafu anacheza kwa ajili ya timu. Naona yeye ndio anampatia pasi Karelis, lakini sioni Karelis akitoa pasi nzuri kwa Samatta. Kama ulivyosema combination ya wawili hawa itakuwa matata sana ambapo Samatta analazimika kuwa mpishi kwa ajili ya Karelis