Hatimaye nguvu ya umma wa wachangiaji washinda sakata la mifuko ya pension

mkuu hawa jamaa usiwape kauli za kuwasamehe kirahisirahisi hivyo. wameshatunyanyasa mno hawa, sehemu za migodini kule Mara binadamu na mifugo tunadhurika na makemikali ya migodini, tukiwaambia wanaanza kutudhihaki. in-short hawa magamba wameshatusulubu vya kutosha hasa hizi awamu za pili, tatu na nne. yaani ni wadhulumaji na wanyang'anyi wa mchana kweupe. wanajijari wao tu na washikaji zao. hawa sio watu wa kusamehe kirahisi. tuwatoe kwanza madarakani halafu ndio tufikirie kuwasamehe.

Nyerere alishawahi sema kwamba katika hawamu zilizopita wamefanya ya kijinga na ya maana,sasa inabidi hawamu inayokuja(jk/mkapa) watoe mabaya na waendeleze mema! Sasa cha kushangaza hawamu hii inafanya ya kijinga tu,dawa yao 2015!! Hawa Jamaa sijui wanafikiri watatawala milele? Kulikua na Kina Hitler,kina Kuku wazabanga,Gaddafi,Al-Capone,wako wapi?
 
Huwenda kalipata hicho cheo kwa kufunua malinda! Hela yetu inauma-Watulipe tusepe!
Dah! umenchekesha sana,alipata cheo baada ya kufunua malinda???!!!!!! ila yawezekana ni kweli make kalikuwa kamekomalia kwelikweli!!!
 
Huwenda kalipata hicho cheo kwa kufunua malinda! Hela yetu inauma-Watulipe tusepe!
Na hilo ndilo tatizo kubwa tulilonalo. Wanawake wengi waliopewa nyadhifa kubwa hawakupewa kwa sababu wanao uwezo wa kumudu majukumu ya nyadhifa zao. Tazama fisadi Makinda anavyokinajisi kiti cha uspika. Nimesikia vituko vya RC wa Tanga Lt Galawa juzi nikapata kizunguzungu. Nimewasikia wengine leo wanalia kuwa ipitishwe sheria itakayowezesha kuwa na uwakilishi wa 50% kwa wanawake na wanaume bungeni.
 
Hatuna Serikali wa Bunge, wote ni wasanii 2 hawa. ilikuwaje ukapelekwa bungeni na ulipitaje mswaada kandamizi bungeni? Ikifika wakati wa kuomba kura wajibu haya maswali, wezi wakubwa hawa

Bob G unaongelea bunge lipi? Hili hili la mafisadi, walevi na wavutaji wa sigara mbali mbali?
 
Wale waliokuwa wanaleta threads zao ndeefu za kutukashifu tuliokuwa tunapinga hii sheria wajitokeze waseme sasa. Siyo kila kitu kinachofanyika huko nje wewe unacopy tu! Na huyu Irene Isaka wa SSRA alitukosea heshima sana Wafanyakazi kwa kutuambia tunalilia hiyo 10% wakati 90% tunayopata tumeshindwaje kuitumia vizuri. Shame on you!
 
Hii kitu naisubiria kwa hamu, ifutwe kabisa maana ni wizi wa waziwazi...
 
hifadhi za jamii za nchi zilizoendelea tofauti na huku kwetu,cha kushangaza ssra wanacopy nje wanakuja kupaste huku kwetu,tena wanapaste vipengele vinavyomnyonya mtanzania(withdrawal benefits) huku wakivi-delete vile vinavyomfaidisha mtanzania(unemployment benefits) huu ni ujinga,sheria sio msaafu wala biblia kusema kwamba haibadiliki,wamefanya kosa tumewasamehe ila msije kurudia ujinga huu tena!!
hii ilikuwa ni mbinu chafu ya kuendela kumuachia r1 channce ya kuchezea hela za migongo yetu tulizowekeza kwa miaka kadhaa. Hii noma sana hawa watu wanatumia nafasi yao vibaya dhidi ya maslahi ya umma wa tanzania
 
Hivi huyo Irene Isaka ana wazazi na ndugu wa Tanzania hapa?kweli?hana utu wala uzalendo kwa wananchi wenzake(kama yeye ni Mtanzania)..... Anatumiwa kukandamiza jasho la walalahoi woote hawa?sidhani huyu dada amepewa nini?au ndio vyeo vya chup+++ sasa analipa fadhila kwa kufanya chochote watakavyoambiwa wakubwa wanataka
 
Huyu Irene mnamsakama bure tuu nafasi yenyewe kaipata kwa hisani apa wa kumlaumu ni JK aliwezaje sign kitu cha dhuluma kama icho
 
Unajua hawa wezi wanajisahaulishaga kwakuwa wao wana mapesa mengi. Katika waTZ kusave kamshahara ni jambo gumu sana kutokana na ukali wa maisha na mikopo mbalimbali. Hii compulsory saving kwa maana ya pension ilikuwa ndo inatutoa. Waliofuta hawana njaa, wenye njaa hawana mamlaka. kaaaazi kweli kweli
 
Nimesoma hotuba ya kambi ya upinzani wizara ya kazi. Wameeleza kwa ufasaha jumla ya mikopo iliyochukuliwa na mingine kudhaminiwa na serikali toka mifuko ya hifadhi ya jamii ambayo imepelekea mifuko hii kuelekea kufilisika baada ya serikali kushindwa kulipa mikopo hiyo. Kwa upande mwingine, naibu kiongozi wa upinzani bungeni ambaye pia ni mwenyekiti wa POAC, kamati ambayo mifuko hii iko chini yake, amekuwa akipigia upatu fedha yetu hii ichotwe tena ikawekezwe huko kwenye mradi wa umeme wa maka ya mawe Kiwira. Hivi yeye kama mwenyekiti wa kamati hiyo nyeti hakuyajua hayo matatizo yaliyoelezwa na waziri wake kivuli yaliyopelekea kakausha hii mifuko yetu? Huyu ndiye anataka kuwa rais wetu? Mungu apishie mbali.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom