Hatimaye Masauni - UvCCM Ang'atuka

Naona kuna utata katika habari ya kwenye gazeti la mwananchi (hard paper vc online). ninaomba kunukuu sentensi zifuatazo kisha tujiulize ukweli ni upi:

Mwananchi online: "Habari zinasema kuwa Masauni alitakiwa na katibu wa CCM, Yusuf Makamba ajiuzulu kwa hiari yake, lakini aligoma na kujitetea dhidi ya kashfa inayomkabili ya kughushi umri wakati anagombea nafasi hiyo mwaka 2008"

Mwananchi hard Paper lililo mtaani: "Habari zinasema kuwa Masauni alijiuzulu saa mbili usiku baada ya kubanwa na katibu wa CCM, Yusuf Makamba ajiuzulu kwa hiari yake dhidi ya kashfa inayomkabili ya kughushi umri wakati anagombea nafasi hiyo mwaka 2008.

Swali: ukweli ni upi?

Habari ya kwanza imewekwa jana usiku 9.52 pm, bila shaka ilinyofolewa kutoka kwenye computer kabla ya kuwekwa kwenye page. Baadaye habari ilipofanyiwa update (ya masauni kujiuzulu) ndiyo ikawekwa kwenye page na kupelekwa mtamboni!
 
Mie nimeshangaa haswa,nakumbuka back 1997 nikiwa Ngaza Secondary huyu mdada alikuwa pale Nyegezi Social (SAUTI) akisoma na alikuwa kama kwenye mid 20's,kama mpaka sasa bado ni kijana,basi tena.
Shyrose ni mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM akitokea UWT(umoja wa wanawake tz),UVCCM pia wana mjumbe wao kwenye baraza kuu la UWT,ni utaratibu wao CCM.
 
ANOTHER BLUNDER YA JK.
Kuna blunders nyingi zilitajwa katika thread fulani, napenda na hii iongezwe kwani JK ndiye alimkingia kifua Masauni
Vyombo vya ushauri vinafanya kazi kweli? au JK ndiye hashauriki.
Kuna siku tutaamka na kuambiwa tuondoke TZ maana imeshauzwa sisi bila kujua!
 
Mie nimeshangaa haswa,nakumbuka back 1997 nikiwa Ngaza Secondary huyu mdada alikuwa pale Nyegezi Social (SAUTI) akisoma na alikuwa kama kwenye mid 20's,kama mpaka sasa bado ni kijana,basi tena.

Ni kweli alikuwa Nyegezi( NSTI wakati huo). Haikuwa 1997 bali 1990. Alikuwa anasoma diploma ya Journalism. ShyRose sasa hivi atakuwa amenusa 40 au zaidi.
 
Nasikia hiyo yote ni influencee ya mtoto wa Rais, kwa kuwa anasauti ambayo inatokana na kuwa mtoto wa presidaa na yeye ndio ameshinikiza hao jamaa watoke. humo namo kuna makundi na hii yote ni sababu ya Ubara na Uzanzibar. Nimesikia kwenye magazeti yaliyokuwa yakisomwa leo asubuhi na kituo cha radio cha magic fm
 
Ridhiwani uko wapi hebu chukua mikoba ya Masauni......!

Ridhiwani......................? aghaaaaaaaaaaaaaaaaa achana na huyu dogo hamna kitu pale."Like father like son" Wapo vijana kibao safi kama Nape.
 
Wakuu,

1.Kama Masauni na vijana wa zanzibar wameona kuwa wanaonewa basi wachane na CCM sababu mie sioni sababu ya mtu kumng'ang'ania mtu ambaye hakutaki na hakupendi.

2.Kuna jambo mnamiss hapa,Riz ni nguvu ya Mzee wake na siku zote Muungwana amekuwa akiamini kwa nguvu ya kupata habari za kiinteligensia,hivyo kupandikiza watu kila sehemu kunamsaidia sana hivyo msishangae kuwa hayo ni maagizo kwa ajili ya uchaguzi mkuu..

3.Kama kweli Muungwana hausiki na hili jambo basi amrudishe kwenye uongozi tena,si alimweka yeye?

4.CCJ bado inahitaji vijana waadilifu kwa ajili ya kuunda jumuiya ya vijana waadilifu wa CCJ .hivyo anaweza jiunga nao.

5.Kama anasema wanampiga majungu si awataje?mie huwa sipendi kuishi kwa speculation bila kujua ukweli..Aseme
 
CCJ tunasema "Wera wera sitoi bila heraaaaaaaaaa na tuko furuuuuuuuuuuu" Tendwa acha uma##$$ wako tupe usajili wetu tuwangoe hawa mafisadi.Waachae wagombane sisi tunaimarisha chama tubebe nchi.
 
ANOTHER BLUNDER YA JK.
Kuna blunders nyingi zilitajwa katika thread fulani, napenda na hii iongezwe kwani JK ndiye alimkingia kifua Masauni
Vyombo vya ushauri vinafanya kazi kweli? au JK ndiye hashauriki.
Kuna siku tutaamka na kuambiwa tuondoke TZ maana imeshauzwa sisi bila kujua!

Mkuu, sina mbavu!
 
Nikivaa hayo maguo ya kijani,MUNGU atanilaani !

Laiti idadi ya watu mnaosema hivyo ingefikia dazeni 10 hivi!!

2005 niliongea na washikaji kibao, ila baada ya uchaguzi kila mmoja akanipa mshindo nyuma kuwa hakuona mtu mwingine wa kuchagua zaidi ya JK. Baada ya hotuba ya juzi wakaanza kunambia kuwa wanajuatia uamuzi wao. Pia FL1 naye alikuwa anajuta.

Naona tunalaani hayo mambo kabla neema ya khanga, T-shirt na pilau haijatutembelea. Tuna miaka zaidi ya 100 kufika nchi ya ahadi labda Musa wetu ajitokeze kimiujiza (kuptia CCJ????)!!
 
Kwa hiyo Malisa atakaimu uenyekiti? Nasikia wazee wao wa CC wanakutana leo pamoja na mengine ku-deliberate juu ya hali hii. FMES uko wapi? Tunakumiss sana kwenye suala hili.
 
Kwa hiyo Malisa atakaimu uenyekiti? Nasikia wazee wao wa CC wanakutana leo pamoja na mengine ku-deliberate juu ya hali hii. FMES uko wapi? Tunakumiss sana kwenye suala hili.

FMES nimempoteza kwa muda sasa.Nitawasilina naye baadaye kujua nini kimemsibu ila mkulu yupo..

Nitawapa nyeti baadaye kuhusiana na Hili
 


Haya ni makubwa sasa, Ningependa kuwaambieni kitu, wanompiga vita masauni na kumnyooshea vidole ningependa kuwauliza ndani ya UVCCM je kila mmoja wenu nae atupe umri wake wa kweli basi maaana najua fika ndani ya UVCCM ni wachache sana wenye umri mdogo kwani hii sheria nayo hajazingatiwa ukitizama ni vijana wachache sana katika nchi hii ndio wako UVCCM na wenye umri mdogo na wengi wao ni umri mkubwa sasa pia UVCCM nanyi hili mkalijadiri na umri uwe mwisho 35.

nimeona matukio mengi ya viongozi wa UVCCM ndio wanao jiuzulu lakin cha ajabu Masaun anachia ngazi kwa kosa la Umri je hao Viongozi wakuuwa CCM wano kutwa na kashafa nyingi na bado wako wanang'ang;ania madaraka ndani ya CCM au NEC je mbona hawaachii ngazi?

CCM kuna tatizo na inapaswa wakaechini wajichunguze sana na kwa makini wasije jisahau wakadhani hao viongozi wao ndio CCM hata kidogo wasije jidanganya yatakuja wakuta tu huko mbeleni.

Nilisha wambieni UVCCM ni hawana hata kauli mbiu NAPE alisema saaana na waka mdharau hao hao UVCCM hata kumuunga mkono wao wakapiga kimya hizo pesa za mafisadi na zinawachanganya sana na hamtokuja iongoza hii nchi amini nawambieni ninyi viongozi wa UVCCM mliopo kwasasa simameni na mjisimamie msingojee kuambiwa na mfanye jinsi hao wakubwa zenu watakavyo mtaburuzwa mpaka lini


Mafisadi ni wenzao na Masauni hakuwa mwenzao ndio maana kwa kosa dogo tu la kufoji umri mamemtupa nje lakini waliofoji nyakaraka na kuiba fedha ya walipa kodi kwa kuumia Kagoda, mikataba ya jengo la vijana ni wenzao
 
Hii ni dalili ya another Kikwete kuongoza hicho kijichama duh
 
Naomba kuuliza tu kwani kijana kwa mujibu wa UV SISI M ni miaka mingapi? na huyo Shy rose ni kijana? Ni swali tu!

Ni mzee kwelikweli huyu dada....alicheza 'REDE' mwaka 1969....sasa jumlisha mwenyewe umri wake maana hiyo rede huchezwa na vischana vya 6-15 years
 
Masauni hakuwa chaguo la JK wala Ridhiwani. Hawa baba na mwanae walimtaka Beno Malisa, rafika wa karibu wa Ridhiwani, ili wawe wanatawala wao kupitia mgongoni. Baada ya kampeni kali kati ya kundi lao na la Hussein Bashe, ndipo ikafanyika 'compromise' na kuwaweka Malisa na Bashe wagombee u-Makamu na Masauni wa waZenji wenzake wawili wagombee Uenyekiti.

Kwenye mkutano wa uchaguzi kule Dodoma kampeni kali zilikuwa kati ya Malisa na Bashe, na waliteka wajumbe wengi. Ilikuwa wazi kuwa atakayechaguliwa kati ya Malisa na Bashe basi atakuwa anaungwa mkono na wajumbe wengi na atakuwa na nguvu kuliko Mwenyekiti wake.
Hata kwenye uongozi wake imeonekana wazi kuwa Malisa na Ridhiwani wanam-sideline 'Mwenyekiti' Masauni kwenye events, mfano ile ya Arusha.

Hivyo Masauni alichaguliwa kwa matumaini kuwa atasema 'asante Mzee Kikwete' na atakuwa 'yes man' kwa Ridhiwani. Hilo ameligomea, hivyo wameibua hoja ya umri, ambayo kwa UVCCM wengi wapunguza umri wao ili wapate madaraka ndani ya UVCCM.
Na kama kawaida yaonekana Mzee JK na Ridhiwani wanamtumia Mzee Makamba kuleta fitina...

Au kama vp turudishe ASP, vijana wawe ASPYL (ASP Youth League), na Bara iendelee na UVCCM ya Vikwete...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom