HATIMAYE John Tendwa akubali kukutana na CHADEMA

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Tendwa sasa anywea kwa Chadema


Na Khamis Mkotya


HATIMAYE Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa amekubali kukutana na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), baada ya kuwapo mvutano baina yake na chama hicho.

Hatua hiyo inalenga kumaliza tofauti zilizopo baina ya msajili na chama hicho kikuu cha upinzani nchini.

Jitihada za kutafuta suluhu hiyo inafanywa na Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Dk. Emanuel Makaidi, ambaye ameingilia kati uhasama huo.

Akizungumza na Mtanzania jijini Dar es Salaam jana, Dk. Makaidi alisema anasikitishwa na uhusiano tete uliopo baina ya vyombo hivyo viwili.

Dk. Makaidi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha NLD, alisema amefungua mlango wa kutafuta suluhu baina ya msajili na chama hicho kwa faida ya taifa.

Chadema ilisitisha uhusiano na ofisi ya msajili na kulazimika kutangaza mgogoro na kiongozi huyo kutokana na kuchukizwa na kauli yake ya kutishia kukifuta chama hicho.

Msajili alitishia kufanya hivyo kwa madai kuwa chama hicho ndicho kilichosababisha mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa Channel tena, Daud Mwangosi.

Dk. Makaidi alisema licha ya kuanzisha jitihada hizo kwa muda sasa, lakini jitihada zake zimegonga mwamba baada ya kushindwa kukutana na viongozi wa juu wa Chadema.

Dk. Makaidi alisema uwamuzi wa kutafuta suluhu hiyo ulifikiwa katika mkutano wa wadau wa siasa ulioitishwa hivi karibuni na Tendwa, ambapo Chadema haikuhudhuria.

"Chadema na msajili wa vyama wote ni wadau wa siasa, kwa hivyo misimamo yao hii ikiendelea itakuwa haina tija kwa taifa zaidi ya kuendeleza chuki na uhasama.

"Chadema kususia shughuli za mtu aliyewasajili, hii si sawa na pia msajili kutishia kukifuta chama tena chama kikuu cha upinzani alichokisajili mwenyewe pia nayo si sawa.

"Kwa kutambua hilo, ndipo tunapotafuta suluhu. Tunataka wakutane wazungumze na kujadili waone namna ya kumaliza tofauti zao badala ya kila mmoja kubaki na msimamo wake.

"Pamoja na kwamba nimeshindwa kukutana na viongozi wa Chadema, lakini nataka wananchi wajue zipo jitihada zinazofanywa za kurejesha wao," alisema.

Hata hivyo Dk. Makaidi alisema tayari msajili huyo amekwisharidhia kukutana na viongozi wa chama hicho ili kumaliza tofauti zao, baada ya kufanyika kazi kubwa.

"Oktoba 16 nilikwenda kwa msajili, pamoja na kumweleza kushindwa kwangu kukutana na viongozi wa Chadema, nilimwomba msajili afanye kila analoweza akutane na viongozi wa Chadema.

"Awali msajili alipinga wazo langu akisema kuwa atawezaje kuwaita watu ambao hawamtambui. Lakini nafurahi baada ya ushawishi mkubwa hatimaye msajili alikubali.

"Wapo watu wanaoweza kubeza na wengine wakaona kama Chadema wanabembelezwa. Hapana, katika hali kama hii ni vigumu kuiepuka Chadema katika mazungumzo.

"Kwanza Chadema ndiyo official opposition (kambi rasmi ya upinzani) bungeni. Pia ni chama kikuu cha upinzani nchini, hakuna namna ya kuikwepa.

"Napenda kutumia fursa hii kuwaomba viongozi wa Chadema wakiitwa na msajili wakubali ombi la msajili ili kumaliza tofauti zilizopo. Kuendelea kubaki na msimamo haitusaidii kama taifa," alisema.

Akizungumza na Mtanzania kwa njia ya simu, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika, hawezi kuzungumzia suala hilo kwa sasa.



Mnyika alisema chama chake kilikwishapeleka barua Ikulu kulalamika namna kinavyohujumiwa na kueleza kuwa wanachosubiri kwa sasa ni majibu ya barua hiyo na si vinginevyo.


Source: Mtanzania



 
Nilijua tu. Ameona dhouruba kali ya M4C ambayo ilikuwa inamnyima usingizi, hasa akifikira baada ya muda wake atakuwa raia tu wa kawaida!
 
Nilijua tu. Ameona dhouruba kali ya M4C ambayo ilikuwa inamnyima usingizi, hasa akifikira baada ya muda wake atakuwa raia tu wa kawaida!

Huyu mjamaa ameanza kuuhofia ukada wake wa chama cha magamba! Huwa nashangaa kwa nini hjataki kuwa neutral , Haiduru angekuwa anakaa kimya kama vile yule aliyemtangulia, George Liundi. Wakati wa vuirugu za kisiasa kati ya serikali na NCCR, na baadaye CUF, Liundi alikuwa haropoki na kupayuka ovyo kama huyu mjamaa!
 
Safi sana Dr. Makaidi wewe yaelekea unasoma ramani za upepo utokako na kule unakoelekea. Big up kwani busara ya U-DR wako imejidhihilisha bayana bila chenga. Mimi binafsi nawashauri wapiganaji wangu wakubali ushauri huo, kumbuka mkono ukigusa mavi huwa haukatwi bali huoshwa kwa maji.
 
tungelikuwa na madaktari wa hivi hata kule ccm basi tanzania ingekuwa mbali sana ...Dr.umekuwa mkweli sana!
 
aiseee babaangu hiyo barua yetu imekwenda ikuli gani hiiii ya magogoni au ikulu nyingine??? manake ikulu ya magogoni siiamini hata kidogo wanaweza sema imepotei barua yetu
 
Mbinu za magamba kuidhibiti cdm zinazidi kugundulika na kufeli sijui hili la udini walilolipandikiza lazima ifikapo 2015 litakuwa limekwishawamaliza
 
Maigizo haya wawapelekee wasiojua kiswahili.
Tendwa amechemka sana, afute kwanza kauli yake ya kutishia kuifuta chadema, kauli inayoonyesha chuki ya moja kwa moja.

Amempanga mzee makaidi kanakwamba asomeke ni mpatanishi, kinachopaswa ni kumhukumu huyu joni tendwa kwa kuyatumia madaraka yake vibaya. Chadema mkiitwa na huyu kibabu mwambieni afute kwanza tishio lake, manake mkienda kabla hajafuta kauli mnaweza kujikuta mnakabidhiwa barua ya kufutwa rasmi.
 
Anyway taarifa inaonesha suluhu bado iko mbali.

Nadhani ilipaswa kuwa hivi; kwa vile Tendwa alilianzisha basi na awe yeye wa kwanza kuitikia wito wa mpatanishi kwa kuiandikia barua rasmi CHADEMA au kutangaza kama alivyofanya awali kuwa anawaomba CHADEMA wakutane ili kujadili na kutatua tofauti zilizopo.

Ila pamoja na hayo tutaendelea kuwa makini naye maana kaonesha udhaifu mkubwa sana kama binadamu na kama Msajili. Atapewa ushrikiano ili mambo yarudi kwenye normalized status. PERIOD.
 
Hatimaye Tendwa akubali kukutana na CDM? Ni lini Tendwa alisema hataki au hawezi kuktana na CDM?
 
Ni vema viongozi wa CDM wakakutana na Msajili pamoja na yote itakuwa pia nafasi kwa CDM kumuweka sawa kwa kumpa darasa hata hiyo barua iliyotumwa magogoni apate copy.
 
Mkuu nadhani hiyo heading haipo sawa! Hapo wakukubali kuongea na mwenzie ni cdm na sio Tendwa maana wao ndio waliositisha ushirikiano! Sijawahi kusikia Tendwa amekataa kuongea na cdm!
 
hakuna kukutana na huyo kilaza!dawa ni ang'oke tu kwenye hiko kiti cha usajili anachokiona ka mtaji!
 
Akanushe upuuzi aliouongea kwenye media ile ile aliyotumia,na aache mambo ya ukada wake kwa CCM
 
Ni vyema viongozi wangu wakakubali kukutana nae hili kumaliza hili tatizo.

Sisi sote ni ndugu!

Na tendwa aache mchezo wa vitisho vya kitoto!
 
Tendwa kama msajili wa nyama vya siasa nchini alipotoka na kuongozwa na jazba na ukada wake kuropoka yale aliyoropoka. Hivyo hawezi kukwepa kubebeshwa lawama hizi za kutoelewana na chama kikuu cha upinzani nchini. <br>La msingi ni yeye kukubali ukweli usiopingika kuwa alipotoka na kukurupuka na kuropoka. Kwa maana nyingine ni kwamba yeye Tendwa anatakiwa kufutwa ile kauli yake ya kutishia kukifuta CHADEMA. short of that nawasihi Chadema kutokubali kukaa meza moja na huyu kada wa waziwazi wa MAGAMBA-period!!!!
 
Back
Top Bottom