Hatimaye BAVICHA yapata Katibu Mkuu, ni Deo Munishi

Nilikuwa nakuona umeelimika lakini kwa sentensi hiyo nimekupuuza sana.
Mkuu wangu nisome vizuri. Nachoamini mimi sio lazima kifanyike nchini isipokuwa unatazama WATU na MAZINGIRA yaliyopo. Binafsi ningependa kuona utawala usiojali kabila, jinsia, wala dini lakini mnaambiwa kwa siasa za Tanzania hili haliwezekani na muhimu sana kutazama vitu hivi (Watu na Mazingira) kwa sababu ndivyo wananchi wote wanategemea kuona uuwiano ktk maswala yote ya kitaifa...

Sasa Kama Chadema wanaelewa hivyo, na hakika kutojali hali hiyo ndiko kumepelekea wao kuonekana chama cha Kidini na kikabila (mimi sioni) kwa nini bado wanaendelea na mfumo huu ambao unawapotezea umaarufu zaidi?.Na haya niliyajua baada ya kukutana na Kitila akanambia swala la Udini na Ukabila nchini ni very sensitive na Politically lazima kulitazama kwa makini sana tofauti na kuchagua mtu yeyote kulingana na uwezo wake wa kuongoza..

Kama Chadema wangekuwa chama tawala nadhani wangeweza kuunda mfumo wa kiutawala ambao hautazami dini, kabila, Utanganyika -Uzanzibar lakini hawawezi kufanya wanayoyafanya chini ya WATU wanaofiiria kwamba Udini na Ukabila upo ndani ya Chadema ktk utoaji ajira. Kwa hiyo usitazame sana maoni yangu kama yangu mimi, bali natazama WATU na MAZINGIRA waliyopo Chadema na kutoa hoja zangu.
 
Mheshimiwa heshima mbele, wakati mwingine inabidi mkubali kuwa propaganda zinazoenezwa kuwa CHADEMA ni chama cha kichaga zinaweza kuwaathiri, na kwa mantiki hiyo basi, mkaangalia jinsi ya kuyagawa madaraka kwa njia ambazo hazitosababisha hizo Propaganda kupata nguvu. Hebu chukulia akawepo Mchaga anagombea dhidi ya Kabila lingine na wote wana vigezo sawa, ila mchaga anakubalika zaidi miongoni mwa wapiga kura chamani, huoni kwamba mtu wa kabila lingine kwa makusudi ama kwa kupotoshwa anaweza kulalamika kwamba ameshindwa uchaguzi kwa sababu ya ukabila?

Huoni kwamba pendekezo lako lina mtizamo wa kikabila kwa kuwa mchaga atanyimwa haki yake ya kuchaguliwa kwa merit?una suggest kwamba propaganda ya ukabila iuliwe kwa suluhu yenye fabric ya ukabila?wenye kupima wamekuelewa
 
Tatizo lako wewe unawaza tu ukabaila, maana wewe ni mkabila. Mawazo ya watu wanaowaza mbali huwaza mabadiliko na maendeleo.
Hili sio tatizo lake ni Watanzania wengi kwa Ujumla wanatazama dini na makabila ya viongozi. Humu JF kila siku wanazungumzia Baraza la mawaziri, Bunge, na kadhalika ndizo siasa za Bongo na Chadema at this particular period wameshikwa pabaya ni lazima waepuke mtazamo wa watu hasa baada ya CCM kuwasingizia kuwa na Ukabila la Udini.
1. Je, Utaweza vipi kujitetea ikiwa kweli viongozi wake wengi ni Wachagga.
2. Je, Ukabila utazungumziwa wakati gani? inapotokea kitu gani?...naomba msaada wenu.
Jamani tuwe makini na sii kuunga mkono kila kitu wakati tunajua kabisa CCM wameisha pandikiza mbegu za ukabila na Udini..
Kuna kosa gani ama tutapungukiwa kipi kumchagua mtu mwenye uwezo toka makabila mengine?
 
Polepole ukabila unaingia nchini kama fikra dhaifu kama hizi bado zipo vichwani mwetu. Waliopiga kura walikuwa Wachagga tu? Mbona sielewi Mzee!
 
Hiyo ya cdm ni chama cha kichaga ni single iliyochuja na imedoda tafuteni nyingine.
 
Dah.... unajua uongo ukizungumzwa sana mwisho wake hua kweli vile - Makosa yale yale yanarudiwa na Chadema kila siku. Nasema siku zote WATU na MAZINGIRA kuwa kigezo cha maazimio yoyote..Chadema leo ilipo haitakiwi kabisa kufanya makosa kama haya pamoja na kwamba mimi naamini kabila, dini, Utaifa (Zanzibar - Tanganyika) wala jinsia siii sababu hata kidogo lakini nilisomeshwa na Mwalimu Kitila ya kwamba ktk siasa za Tanzania (ktk kujenga Utaifa), kabila na dini vinahitajika kutazamwa sambamba na CV ya mhusika...Sasa ikiwa hivyo ndivyo na Chadema wanaelewa fika kwamba wanashukiwa Udini na Ukabila kwa nini wanaendeleza kufanya makosa yale yale..

Pole sana kwa ufinyu wa mawazo! Hivi mpaka leo hujapata ufaham kwa nini wachaga wako kila mahali, na kwa uhalali?!

Acha mawazo mgando na fikra finyu tena potofu za udini, na ukabila!

Nakushauri ufanye kazi kwa bidii, soma upate kufahamu na Mungu akusaidie kupunguza na kuiondoa "inferiority complex" uliyonayo!
 
Mkuu Ibrah,

simaanishi kwamba tuwanyime madaraka, bali swali langu limekusudiwa kuwapa CDM picha ya ni jinsi gani propaganda zinaweza kuibuka, na kwa kufanya hivyo basi waandae mbinu ama namna watakavyozikabili changamoto hizo. Wakati mwingine siyo kila hoja inajibika kwa hoja peke yake.

TANMO,Watz wa leo si wa jana, wana ufahamu na uwezo wa kujuja mchele na chuya.
Pamoja na kejeli, propaganda umeona umaarufu wa CDM umeporomoka?
 
Chama cha kichaga. Naona wameamua wamempe mchaga mwenzao ukatibu.
Acha mawazo ya KIPUUZI wewe,Regia ni mchaga?Zitto ni mchaga?Wenje,Dr Slaa je?Mbona mnakua na mawazo ya kigasho gasho nyinyi?Hata mkijaribu kutuvuruga HATUVURUGIKI ,sanarana mnawaongezea viongozi wetu UMAARUFU tu,na kamwe Watanzania walishachoka kusikiliza siasa zenu zenye VINYESI.
 
Wakuu habari!

Baraza la Vijana CHADEMA(BAVICHA) hatimaye limepata Sekretariet iliyokamilika na hivyo kuwa na Uongozi uliokamilika.Kikao Cha Kamati Tendaji Cha BAVICHA kilifanyika Siku ya Jumamosi tarehe 12 Nov Mjini Dodoma.Wajumbe wa Kikao hicho ambao ni Wenyeviti wa BAVICHA wa Mikoa,Viongozi Vijana wa Chama Taifa,Wawakilishi Watano wa Wabunge Vijana na Wawakilishi Watano wa Madiwani Vijana.

Katika Uchaguzi huo uliokuwa na mchuano mkali,wafuatao walichaguliwa;
1. Katibu Mkuu wa Baraza hilo Bwana Deogratius Munishi
2. Naibu Katibu Mkuu Bara wa Baraza hilo Bi Esther Daffa
3. Naibu Katibu Mkuu Zanzibar bwana Suleiman Maabad
4. Mratibu wa Uhamasishaji au Katibu Mwenenzi wa Baraza hilo Bwana Rafiki Rufunga
5. Mwekahazina wa Baraza Bwana Mrisho Ramadhani

Mbali na Uchaguzi huo Kikao hicho pia kilijadili Hali ya Siasa nchini na mambo mengineyo.

Aluta Continua.
Thanx KAMANDA REGIA kwa taarifa,tupo pamoja.
 
Bila unafki wowote, mi nimefanya kazi Munishi mwaka jana wakati wa uchaguzi mkuu pia nimefanya kazi na Rafiki Lufunga(mratibu uhamasishaji) hapa UDOM yeye akiwa M/kit wa cdm na mimi kama katibu wa moja ya collage:
Nianze na munishi, nimejuana nae kwa kipindi kifupi tu wakati wa uchaguzi wa mwaka jana ila kwa namna tulivyo weza kufanya kazi kwa pa1 na kwa ufanisi mzuri inanifanya nisiwe na shaka kabisa kabisa kwa nafasi aliyopata sasa, nakumbuka wiki mbili kabla ya kupiga kura tulifanya kazi kubwa ya kushambulia majimbo mawili kwa mpigo katika mazingira magumu mno kwan hata pesa ya kula tulikuwa hatuna, ila pa1 na hayo Munishi alikuwa mbele.
Rafiki Lufunga nimefanya nae kazi kwa muda wa zidi ya mwaka1, ni kijana anaye kipenda chama chake kutoka ndani ya mifupa yake, huwezi amini yuko tayari kuuza mali yake ili aweze fanikisha mipango ya chama, pili ni mnyenyekevu na mwingi wa busara, anapenda mashauriano zaidi ya maamuzi binafsi, mwepesi kuwajibika, nakumbuka alikuwa wakwanza kujiuzulu ukatibu wa cdm baada ya kugundulika kuwa mwenyekiti wake alihongwa kwenye uchaguzi mkuu wa mwakajana na alikataa kugombea nafasi yoyote hadi pale viongozi tulipo msihi kwa muda mrefu.
All in all, tuna majembe ya uhakika!
 
I have been following various political threads in this forum, most of which always turns to disgusting tribal bashing. And as far as am concerned most of these internet gangsters/gladiators cannot burst a grape in a fruit fight, they rather hide behind their inconspicuous screen and say stuff that any real Tanzanian knows to be garbage.

As far as am concerned most of these sentiments does represent the actual view except that of cowards that knows they can't change or influence things about their environment. I look forward to a time when young people in this country can actually use their limited time on something productive and even when they want to engage in a debate, they do it with an open mind with actual good intention of being productive.

That said, I can only say that the stands been presented on JF about political issues most times do not represent the stand or the opinion of the man on the street or anywhere trying to feed himself and his family. just as this issue on ground do not have anything to do with an average Tanzanian hustling to make ends meet or for his benefit.

Kama tunaweza kupata ukombozi au njia ya kupigania maslahi ya watanzania kutumia vyama vya siasa au maslahi ya vijana kupitia mabaraza na jumuiya za vijana ndani ya vyama vya siasa basi tuwaunge mkono na tuwasaidie katika planning na mawazo ili mradi wawe wanakubali ushauri

Tuache kujadili ukabila na udini ambao hautatufikisha popote let us discuss issues.

As for Bavicha : BAVICHA needs to be more realistic with our expectations, we have gone past the era for begging for little things, now it is a demand. Learn to talk that way, we are not the only ones demanding. Power has never been a business of begging, you demand it and work for it..Tupigania maslahi ya vijana kwa njia hiyo,tupiganie demokrasia ya kweli ndani ya chama na nje ya chama bila unafiki.Anything less we are in a mess ! ! !
 
Back
Top Bottom