Unaishi dunia nyingine wewe. Sasa hivi tumefikia mahali ambapo sh elfu ishirini (20,000/=) inatoa roho ya mtu. Jeshi la watu wanaoweza kuua wenzao kwa malipo ya 20,000/= ndiyo silaha pekee waliyobaki nayo CCM.Mh,hii ni laana!!!!!!!
Yaani ujira wa mil 2 unamshawishi mtu kutoa uhai wa mwenzake?Suala wala sio umaskini bali ushetani ulio pitiliza!!!!!
Du! huyu jamaa ni mkatili sana ,hata kama ni chuki hiyo imepitiliza
duh.kweli ni chama cha majambazi,
Pongezi kwa Jeshi la Polisi. Sasa ingieni kwa undani kujua driving force ilitokana na nini, fukua fukua ili kila mtu apate haki yake kulingana na matendo yake. Kila la heri polisi wetu.
Haihusiani na siasa, alikuwa mpangaji wake.
wale waumini wa Vitabu Vitakatifu wanasema, kuamini na kutenda ni vitu viwili lakini haviwezi kutenganishwa (inseparable).Hapana shegaboy! Usihukumu haraka hivyo kwamba ccm ni wauaji kwa maana sidhani kama kulikuwa na kikao cha ccm kilichokaa na kupanga mauaji.Kinachotokea Arumeru Mashariki ni kama kilichotokea Nduli Iringa. Ya Iringa tuyaache maana yapo mahakamani. Lipo tatizo za ukereketwa mkali. Wapo wanachama wa ccm ambao wanajiona wao ndo ccm yenyewe. Chama chake kikishindwa anaona ni yeye ameshindwa na anaumia sana kuliko mwenyekiti wake wa taifa. Ndo hao wanafanya vitendo vya ajabu si chama.
Kwa hiyo tofautisha matendo ya mtu binafsi na misimamo ya chama.
Inasikitisha sana sasa tunaanza kuamini kuwa watakaoleta machafuko Tanzania ni CCM hapa akuna ubishi kabisa kwani tumeona wenyewe na tunaendelea kuona kama mwenyekiti alishiriki hii ni kwamba CCM imeshiriki kwa namna moja katika mauaji haya jamani tunaipeleka wapi nchi yetu.