Hatimaye afande Kova ajibu shutuma juu yake

Babu yangu alimkataza baba yangu asijiunge na polisi sababu kazi hiyo ina LAANA. sasa ndo naelewa laana iko wapi
 
Mahakama ishakua kichaka cha maovu yote yatendwayo na serikali, nakumbuka nilishachangia hapa kuhusu hii movie ya ulimboka labda nikumbushie tuu ni kwamba tulishuhudia ccm kutojadili mgomo wa madoctor sababu kesi hipo mahakamani, kesi za mauaji yaliyofanywa na polisi ayakupewa mijadala bungeni sababu kesi zilikua mahakamani sasa ni hii ya ulimboka maadamu wanajua ulimboka hali yake sasa ni nzuri na anatarajiwa kurudi mda si mrefu hapa kova, mchungaji Gwajuma na TISS walichofanya ni kutengeneza movie itakayoacha maswali mengi yasiyokua na majibu na ndivyo ilivyotokea tokea ijumaa watu kuongelea hili swala na jana mchungaji kukana na mwisho wake leo kutolewa ukumu na kova mwenyewe kua swala hili lipo tiari mahakamani na akuna majadiliano tena au mtu yeyote kuliongelea hili swala.i
Kama mtu yeyote anataka kulijadili aende mahakamani kusikiliza. Sasa basi hata kama ulimboka atarudi atakua na mamlaka ya kuliongelea swala lilokua mahakamani either mtuhumiwa awe ndie au la ni mahakama ndio itakayotoa hayo maamuzi, sio mtaalamu wa sheria labda wanasheria wanaweza kutusaidia hapa.
Inabidi hii katiba mpya tuangalie hii kitu watu ukimbilia mahakamani kuficha maovu na ile kauli ya Tundu lisu inathibishwa kweli kua mahakamaccm+policeccm sivyo tena vyombo vya kuwapatia haki wananchi bali vipo pale kutekeleza matakwa ya kikundi flani.
 
Siyo kwamba hawajui kudanganya,hawaoni umuhimu wa kutumia sophisticated means kwasababu wanawadharau sana wananchi.Wanaona hakuna haja ya kutumia hizo efforts na wanauhakika litapita tu kwasbabu watanzania wengi wanasubiri hadi siku ya kiama ndo wauwaji waadhibiwe na mungu.

Umenena vyema jmushi1
 
Last edited by a moderator:
Kumbe ndo ujanja wa kukimbilia mahakamani siku hizi ili ku-silence watu wasiseme

Kova anapata wapi mandate ya kukataza watu wasiongee kuhusu masuala muhimu ya nchi, kwa nini tunakuwa mbumbumbu. Kova hana mamlaka ya ku-silence watu na watu wana haki kikatiba kudai na kupewa taarifa:

kila mtu anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala muhimu kwa jamii

Hakika hili ni tukio muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia linahusu suala muhimu kwa jamii.

Kova hebu mjibu Gwajima, ili wananchi tupate taarifa juu ya mkanganyiko ulioleta kwa kumkamata huyo mkenya!!!!!!!
 
Wait a minute,

Huyu mtuhumiwa alifikishwa mahkamani lini?

siku Kova akitoa maelezo kwa waandihi wa habari,
mtuhumiwa si alikwisha fikishwa mahakamani?

Kama ni hivyo ni vipi yeye Kova aongelee issue iliyoko mahakamni??
 
PICHA LA KI-VIETNAM vs WAMAREKANI (MMAREKANI MMOJA VS WAVIETNAM 5,000,000)


UKITAKA KUJUA ATHARI ZA SINEMA ZA KIHINDI KURATIBIWA NA UONGOZI WA KI-CHINA BASI KAMUULIZE ALHAJI AFANDE SELE PALE 'MAMBO YA NDANI' NA JINSI GANI ALIVYOLITIA KOVU LA KUDUMU JESHI LA POLISI

Kwa akili tu ya kawaida, busara zinatuamrisha ya kwamba pindi tunapoinuia kutengeneza sinema ama yaa Kihindi, Kimang'ati au hata ya Kichina, ni vema tukawapa nafasi watu wenye ufahamu mzuri na tamaduni za mahali husika wakatusaidia kuratibu mambo.

Ajabu na kweli ni kwamba katika jaribio la kumchukua uhai Dk Ulimboka, majina ambayo yatokea kutajwatajwa yametokea kuwa ni wa upande fulani tu. Madai ya Uhalifu huo ni wao, Uchunguzi ni wao, Usemaji ni wao, na hata Uratibu mzima bado ni wao tu.

Hakika hili kidogo linatatiza kwa kuwa jeshi letu la polisi sote tunajua halina dini lakini kwa mwenendo huu wa mara Abeid wa Ikulu, Ahmed Msangi wa Kanda Maalum, Selemani Kova kubwa lao, Saed Mwema ambaye ndiye Back-stopper hapo -- mmmmmmhhhh!!!

Japo ni jambo ambalo halisemwi wazi wazi na wengi LAKINI mmmhhhhh!!! Kwa nini na kwani kuna nini??? Siku zote Matokeo ya mambo kama haya, pengine ni ajali tu imetokea hadi hapo, mwisho wa siku huleta taswira kama vile ya Picha ya KIHINDI kuratibiwa vile na WACHINA.

Mtu akiangalia ki-undani,
pale kwenye ONYESHO LA PILI, jinsi gani ka-Gwajima (Mkristo) na Joshua (nalo jina la kikristo ila mbebaji wa jina hilo HATUNA UHAKIKA na dini yake mpaka atakapotuthibitishia kwa kinywa chake mwenyewe) wanavyovutwa kwa nguvu zote kuwa sehemu ya mchezo katika filamu hii - yote yanayojitokeza ni VITUKO VYA KARNE katika historia ya mambo ya kipolisi duniani kote.

Kwa watazamaji wapya wa picha hii ya '
KOVA KATIKA MABAWA YA MABADILIKO YA NGUVU YA UMMA NCHINI TANZANIA', kwa kukumbushia tu, ONYESHO LA KWANZA ilianzia pale Leaders' Club na kuishia Mabwepande Tegeta na walioonekana mwishoni mwa picha ile ni Mama Kijo Bishimba, Mzee Mwanakijiji, Mjeruhiwa Dk Ulimboka pamoja na wanakijiji katika yale mandhari asili ya MabwePande.

Sababu ya kusema hivyo ni kwamba Alhaji Afande Sele (Kanda Maalum Jijini Dar), kwa kosa moja tu la kutokufahamu desturi na taratibu za madhehebu ya ki-Kristo ki-ajali kabisa kajikuta AMEUNGUZA PICHA ZIMA kwa kudai kwamba mgeni wake Joshua Muyungi alienda na AKATUBU katika kanisa la Nabii Mkuu na Askofu Gwajima juu ya uhusika wake kwenye jaribio la kumua Dr Ulimboka. Hii ndio maana kila wanapojaribu kuunganisha picha hizo mbili hali inaendelea tu kuwa kama mafuta ya taa na maji kwenye maabara zetu za kibongo hizi.

Ukweli wa mambo ni kwamba mbali na Kanisa Katoliki ambako watu hujichagulia kwenda kwa Padre na kutubu dhambi zao, madhehebu mengine yote ya ki-Kristo hayana utaratibu huo. Lakini kwa kuwa Alhaji alikua anatafuta MNOGO WA PICHA YENYEWE ndio hapo maini yakaingia nyongo.

Kama bado tu mtu hajashtuka kitu hdi hapo, hivi watu bado tu hamjiulizi kwa nini
ONYESHO LA TATU (linalotegemewa kuwa ndefu sana mpaka hadhira kujikuta wachapa tu usingizi badala ya kuendelea kufwatilia picha) la filamu ilivyoanza kwaa usiri mkubwa katika mahakama ya Kisutu na kwamba wahusika wote huko wakawa ni WATU WA KUFIKIRIKA tu huku wengine wakidaiwa kuwasili tu kutoka katika taifa la KUSADIKIKA ('nimewasili na bado ninaendelea kuwazoea').

Mpaka hapa wala mtu hahitaji kutngaziwa kwamba kwele Alhaj Afande Kova kalitia kovu chombo hiki, tulichopata kukiamini na kukithamini sana miaka hiyo, kwa namna ambayo itachukua miaka kuturudisha imani sisi Umma wa Tanzania.

Sasa kilichobaki pengine ni wahusika wkuu wa filamu hii warudi tena mezani ili waje na ubunifu mwingine maana huu wa sasa ndio kama hivo umekwishagonga mwamba.

 
I dont believe in life after amputation but in Tanzania there is life after amputation! Fun enough a president in tz anaweza akawa hana kichwa badala yake ana kifuu cha nazi tena toka bagamoyo hafu anaiongeza nchi,KAMA SI MAAJABU NI NN?
 
Kamanda kova anazidi kuwageuza wananchi viazi vya gairo kwa kusema kuwa waandishi na watu wengine wasiliongeleee suala la Ulimboka na kuteswa kwake kwa kuwa kichaa yuko rumande na kesi ya kichaa iko mahakamani. Kwa akili yangu ndogo bado sielewi. Mie nadhani huu ndo muda muafaka wa kuendelea kusema na kujiuliza nani alifanya hicho kitendo maana aliyekamatwa ni kichaa.

Kwa nini kichaa akae rumande? Pamoja na hayo hakuomba msamaha kwa uongozi wa kanisa alilokuwa kalipakazia issue. Sasa iweje tunyamaze wakati juhudi za serikali makini yenye intelijensia makini imemfungulia kichaa kesi mahakamani kwa hiyo tuache kusema kilicho msibu Ulimboka. Huu ni UDHAIFU kwa mara nyingine. I stand to be corrected. Kama kweli waandishi na wananchi tutakubalina na reasoning ya namna hii basi nitawalaumu Mwalimu wangu Dr. Mihanjo na Rwaitama walionifundisha Critical thinking and argumentation kwa kunidanganya na kuwadanganya wote waliowafundisha.

Kilichobaki tutanyamaza na kusubiri mustakabari kwa vitendo. Nimechoka kulalamika hapa na kwingineko . Huu ni ujinga nasema ni ujinga.

Source : Channel Ten saa moja jioni leo hii.
 
Tulieni tuangalie Movie wazazi,maana mnapiga makelele kama mko mpirani tusubiri ubalozi wa Kenya waje tupa raha mtuhumiwa si mkenya ni mgogo mkazi wa mpwapwa wala Kenya hajui iko upande gani!
 
Kova anapata wapi mandate ya kukataza watu wasiongee kuhusu masuala muhimu ya nchi, kwa nini tunakuwa mbumbumbu. Kova hana mamlaka ya ku-silence watu na watu wana haki kikatiba kudai na kupewa taarifa:

kila mtu anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala muhimu kwa jamii

Hakika hili ni tukio muhimu
kwa maisha na shughuli za wananchi na pia linahusu suala muhimu kwa jamii.

Kova hebu mjibu Gwajima, ili wananchi tupate taarifa juu ya mkanganyiko ulioleta kwa kumkamata huyo mkenya!!!!!!!

Ngambo Ngali.
Hapa ndio katiba mpya inapotakiwa kubadilisha hii tabia mimi sio mtaalamu sana wa sheria ila navyoujua serikali ina mihimili mitatu bunge, mahakama na dola sasa hapa kila kimoja kinasheria zake na miongozo yake so, kwa uzoefu swala likishakua mahakamani uwezi kulijadili tena hata kama wananchi wakitaka kulijadili bado litakua limevunje sheria za nchi so mtalijadili wapi? Pia hata ulimboka akirudi atalijadili wapi? Either avunje sheria ya nchi kujadili jambo lilipo mahakamani.
 
Last edited by a moderator:
Mahakama siku hizi imekuwa kama FFU. Yaani kitu kikija moto wanakipeleka mahakamani afu hakuna kuhoji. Kama kweli mahakamani wangekuwepo majaji wenye weredi na kazi zao wangeisha piga stop hali hiyo. Naweza kukubaliana na Mh Lissu kuwa na majaji wa fasta fasta.
Hawa majaji ni wa voda fasta,Kova anajidanganya sana ati jambo liko mahakamani hivyo lisijadiliwe kwani hapo umesevu????picha ndio kwanza inaanza wee ruka vihunzi tu wakukumaliza ni Dr Uli.utavaa miwani na hayo makengeza yako.
 
KWA MTAJI WA KONA KONA KIBAO ZA KWENYE HII FILAMU YA DK ULIMBOKA JE WAWEZA KUTABIRI NINI KITAKACHOFUATIA KATIKA MSURURU MZIMA WA MATUKIO YA KUKINZANA KILA KUKICHA??

Enyi wana-JF wenzangu,

Onyesho la kwanza laa sakata la kumtoa Dk Ulimboka roho inasadikiwa kuazia pale Leaders Club na kuishia Mabwepande Tegeta.

Wahusika walioonekana tu mwishoni mwa picha katika onyesho hilo ni pamoja na Mama Bishimba, Mwanakijiji, Mdhurika Dk Ulimboka paamoja na wanakijiji maahali pale.Onyesho la pili likawa ni timu ya Ahmed Msangi, Afande Kova, Nabii Mkuu naa Mtume Askofu Gwajima pamoja na 'Joshua' Muyungi.

Onyesho la tatu ya filamu hii ni pale mahakamani Kisutu ambapo kunadaiwa wahudhuriaji karibu wote walikua ni watu wa KUFIKIRIKA tu.

Baada ya kona hizi zote na mzaha uliopita kiwango, je ni nani kati yetu hapa anayeweza kututabiria ONYESHO LA NNE litakavyokua katika filamu hii mara baada ya kutathmini onyesho zilizotangulia, je?

1. Kuna uwezekano filamu ikaishia hapa hapa?

2. Kuna uwezekano filamu ikaanza upya?

3. Yawezekana Staringi Dr Ulimboka akaibuka upya na kuipa nguvu zaidi picha hii?

4. Kuna uwezekano steringi Dr Ulimboka akanunuliwa kwa kupewa KIFUTA DAMU (Mganga Mkuu wa Serikali Wizarani) na picha zima kupata taswira mpya?

5. Yawezekana, kwa mara ya kwanza katika historia ya ulimwengu wa filamu duniani, huyu Steringi Dr Ulimboka wakamkolimba huko huko ili kinachodaiwa mezani hivi sasa ndicho kibakie ukweli na ukweli mtupu wa mambo (Afande Kova et al 2012)?

Katika onyesho la nne, watatafutwa watu wengine ambao watabebeshwa huu mzigo wa nani mhusika, maana ili picha iishe salama lazima watafute mtu watakayemtwisha mzigo walioubeba maana unawaelemea nisawa na kubeba gunia la mavi usipolemewa litakunukia, Inavyoonekana mkuu wa kaya amewapa muda wafanye haraka kumsafisha

Sasa Mahakama ni Chaka la kuchimbwa dawa na Wahalifu wote Tanzania.
Mahakama sasa inatumika kufunga midomo Watanzania wasihoji upuuzi wa serikali,
Mahakama ni pazia la chuma la viongozi wa CCM na serikali yake kujikinga kisiasa.
Wanavuruga,wanadanganya, wanaiba,wanaharibu na kuvunjavunja
kisha wanatimua mbio kujificha nyuma ya mahakama.

Kuna haja ya kujenga hoja ya kuchunguza kwa ukaribu Chaka hili la Mahakama.

Kama kazi ya Ukamishna wa POLISI ndo hii falla na mjinga yeyote anaweza kuwa njagu.

Tulieni tuangalie Movie wazazi,maana mnapiga makelele kama mko mpirani tusubiri ubalozi wa Kenya waje tupa raha mtuhumiwa si mkenya ni mgogo mkazi wa mpwapwa wala Kenya hajui iko upande gani!
 
Ngambo Ngali.
Hapa ndio katiba mpya inapotakiwa kubadilisha hii tabia mimi sio mtaalamu sana wa sheria ila navyoujua serikali ina mihimili mitatu bunge, mahakama na dola sasa hapa kila kimoja kinasheria zake na miongozo yake so, kwa uzoefu swala likishakua mahakamani uwezi kulijadili tena hata kama wananchi wakitaka kulijadili bado litakua limevunje sheria za nchi so mtalijadili wapi? Pia hata ulimboka akirudi atalijadili wapi? Either avunje sheria ya nchi kujadili jambo lilipo mahakamani.
Dr Uli akirudi atahojiwa tu na hapo ndipo atapotiririka na kumwacha kinywa wazi huyu afande mrangi.
 
Vonix

Ulimboka akirudi atalijadili wapi? Kumbuka pia mahakama ni kichaka chao na itapigwa dana dana kama kesi za kina mramba mpaka wananchi watasahau na huyo ulimboka aruhusiwe kuliongea nje ya mahakama so wananchi mtafanya nini? Si mbunge wala nani anaruhusa ya kulijadili. Khaaaa!!!!!.

Katiba mpya plse!!!!!!!
 
Last edited by a moderator:
serikali inatengeneza kaburi lake lenyewe,watatuzuia kwa fitna kulijadili suala hili kwa hila zao za kichaka cha mahakama,watafanikisha...ila trust me kumziba mtu mdomo ni kumuongezea chuki,heri mtu asemeee anyamazee...serikali haiaminiki,polisi hawaaminiki,mahakama hazina mvuto kwa wanyonge,viongozi hawana touch ya wananchi,hawapendwi.

Kinacho tokea ngado-singida ni kielelezo cha chuki ambayo ipo juu ya serikali na watu wanao i support serikali hiyo,chuki hii watawala wanaijenga kwa wananchi,chuki hii inaanza kukua,itahamia kwa akina nappe,mwigulu,wasira et el..ipo siku watapigwa kama wezi na wananchi...!

Ukiwashitaki polisi wataachiwa,ukiwapeleka mahakamani watashinda....lakini nikirusha jiwe,panga,au mkoki siwezi kuwakosa....they will feel the pinch that i always feel,the pains caused by them to me shall be paid as permanent torture to them..
Make my word

maneno yako yamenigusa sana, hawa watu ipo siku na wala si mbali, ukombozi utapatikana
 
dcp sulemani kova amesemani hataki malumbano na mchungaji gwajima kuhusiana na mtu aliyemteka dr. olimboka,
akiongea na waandishi wa habari leo hii amesema kuwa wananchi waendelee kuwa na imani na jeshi lao
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom