Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
Jeetu Patel akiri kumiliki kampuni iliyochota fedha za EPANa Nora Damian
WAFANYABIASHA Jayant Kumar maarufu kama Jeetu Patel na Devendra Patel ,wamekiri mahakamani kuwa Kampuni ya Bencon Internatinal Limited, inayodaiwa kujipatia fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ni ya kwao.
Wafanyabiashara hao walikiri hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakati walipokuwa wakisomewa maelezo ya awali ya kesi yao.
Maelezo hayo yalisomwa na wakili wa serikali, Timon Vitalis, mbele ya jopo la mahakimu watatu wanaosikiliza kesi hiyo, Ruwaich Meela, Grace Mwakipesile na John Kahyoza.
Washtakiwa hao walikiri kuwa wao ni kati ya wakurugenzi wa kampuni hiyo iliyoanzishwa hapa nchini Aprili 4 mwaka 2005.
Pia Jeetu Patel na mshtakiwa mwingine Amit Nandy, walikubali kuwa kampuni hiyo ilianzishwa nchini Aprili 4 mwaka 2005 na kwamba wao ndio waliokwenda kufungua akaunti benki.
Maelezo mengine yalisomwa, lakini yakakataliwa na ni ya kughushi hati za uhamishaji deni kati ya kampuni yao na kampuni za Matshusta na Marubeni za Japan.
Wakili wa serikali Vitalis alidai kuwa kati ya Agosti 12 na Septemba mosi mwaka 2005, mshtakiwa Nandy aligushi hati ya uhamishaji deni la Sh 2,599,944,458.12 kuonyesha kuwa kampuni yao imepewa deni na kampuni ya Matshusta ya Japan.
Alidai kuwa kati ya Oktoba 18 na Novemba 2 mwaka 2005 Nandy alighushi hati nyingine akionyesha kwamba kampuni yao, imepewa deni la Sh 7,962,978,372.48 na kampuni ya Marubeni ya Japan.
Pia alidai kuwa mshtakiwa huyo ni Mkurugenzi wa fedha wa kampuni ya Bencon International Limited.
Upande wa mashtaka ulidai kuwa kutakuwa na mashahidi 18 watakaotoa ushahidi katika kesi hiyo. Baada ya kusikiliza hoja zote Mwenyekiti wa jopo la mahakimu wanaosikiliza kesi hiyo, Hakimu Meela aliahirisha kesi hiyo hadi itakapoanza kusikilizwa Agosti 3 hadi 14 mwaka huu.
WAFANYABIASHA Jayant Kumar maarufu kama Jeetu Patel na Devendra Patel ,wamekiri mahakamani kuwa Kampuni ya Bencon Internatinal Limited, inayodaiwa kujipatia fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ni ya kwao.
Wafanyabiashara hao walikiri hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakati walipokuwa wakisomewa maelezo ya awali ya kesi yao.
Maelezo hayo yalisomwa na wakili wa serikali, Timon Vitalis, mbele ya jopo la mahakimu watatu wanaosikiliza kesi hiyo, Ruwaich Meela, Grace Mwakipesile na John Kahyoza.
Washtakiwa hao walikiri kuwa wao ni kati ya wakurugenzi wa kampuni hiyo iliyoanzishwa hapa nchini Aprili 4 mwaka 2005.
Pia Jeetu Patel na mshtakiwa mwingine Amit Nandy, walikubali kuwa kampuni hiyo ilianzishwa nchini Aprili 4 mwaka 2005 na kwamba wao ndio waliokwenda kufungua akaunti benki.
Maelezo mengine yalisomwa, lakini yakakataliwa na ni ya kughushi hati za uhamishaji deni kati ya kampuni yao na kampuni za Matshusta na Marubeni za Japan.
Wakili wa serikali Vitalis alidai kuwa kati ya Agosti 12 na Septemba mosi mwaka 2005, mshtakiwa Nandy aligushi hati ya uhamishaji deni la Sh 2,599,944,458.12 kuonyesha kuwa kampuni yao imepewa deni na kampuni ya Matshusta ya Japan.
Alidai kuwa kati ya Oktoba 18 na Novemba 2 mwaka 2005 Nandy alighushi hati nyingine akionyesha kwamba kampuni yao, imepewa deni la Sh 7,962,978,372.48 na kampuni ya Marubeni ya Japan.
Pia alidai kuwa mshtakiwa huyo ni Mkurugenzi wa fedha wa kampuni ya Bencon International Limited.
Upande wa mashtaka ulidai kuwa kutakuwa na mashahidi 18 watakaotoa ushahidi katika kesi hiyo. Baada ya kusikiliza hoja zote Mwenyekiti wa jopo la mahakimu wanaosikiliza kesi hiyo, Hakimu Meela aliahirisha kesi hiyo hadi itakapoanza kusikilizwa Agosti 3 hadi 14 mwaka huu.