Hatimae; Jeetu Patel akiri kumiliki kampuni iliyochota fedha za EPA

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,148
Jeetu Patel akiri kumiliki kampuni iliyochota fedha za EPANa Nora Damian

WAFANYABIASHA Jayant Kumar maarufu kama Jeetu Patel na Devendra Patel ,wamekiri mahakamani kuwa Kampuni ya Bencon Internatinal Limited, inayodaiwa kujipatia fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ni ya kwao.

Wafanyabiashara hao walikiri hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakati walipokuwa wakisomewa maelezo ya awali ya kesi yao.

Maelezo hayo yalisomwa na wakili wa serikali, Timon Vitalis, mbele ya jopo la mahakimu watatu wanaosikiliza kesi hiyo, Ruwaich Meela, Grace Mwakipesile na John Kahyoza.

Washtakiwa hao walikiri kuwa wao ni kati ya wakurugenzi wa kampuni hiyo iliyoanzishwa hapa nchini Aprili 4 mwaka 2005.

Pia Jeetu Patel na mshtakiwa mwingine Amit Nandy, walikubali kuwa kampuni hiyo ilianzishwa nchini Aprili 4 mwaka 2005 na kwamba wao ndio waliokwenda kufungua akaunti benki.

Maelezo mengine yalisomwa, lakini yakakataliwa na ni ya kughushi hati za uhamishaji deni kati ya kampuni yao na kampuni za Matshusta na Marubeni za Japan.

Wakili wa serikali Vitalis alidai kuwa kati ya Agosti 12 na Septemba mosi mwaka 2005, mshtakiwa Nandy aligushi hati ya uhamishaji deni la Sh 2,599,944,458.12 kuonyesha kuwa kampuni yao imepewa deni na kampuni ya Matshusta ya Japan.

Alidai kuwa kati ya Oktoba 18 na Novemba 2 mwaka 2005 Nandy alighushi hati nyingine akionyesha kwamba kampuni yao, imepewa deni la Sh 7,962,978,372.48 na kampuni ya Marubeni ya Japan.

Pia alidai kuwa mshtakiwa huyo ni Mkurugenzi wa fedha wa kampuni ya Bencon International Limited.

Upande wa mashtaka ulidai kuwa kutakuwa na mashahidi 18 watakaotoa ushahidi katika kesi hiyo. Baada ya kusikiliza hoja zote Mwenyekiti wa jopo la mahakimu wanaosikiliza kesi hiyo, Hakimu Meela aliahirisha kesi hiyo hadi itakapoanza kusikilizwa Agosti 3 hadi 14 mwaka huu.
 
Didy hakuna jipya hapa lakini hakuna wa kumgusa maana anajua uchafu uliofanyika katika kampeni za kuwania Urais 2005 uliofanywa na wana mtandao. Wanajua fika wakimgusa tu jamaa anaweza kutoa data zote maana wahindi hawa wameshajizatiti na ni wazuri mno kwa kuweka kumbukumbu, sasa hivi wakiguswa tu basi kutakuwa na patashika nguo kuchanika.
 
Yaani hiiiiii nchi we acha tuuuuuuuuuuuuuuuu mungu pekee

nasikia jakaya anaifwatilia hiiiii kesi kwa udi na uvumba na ole wake hakimu atakae wawashia mooto cha moto atakiona...mnamkumbuka mwankenja.....alianza na moto we.anajua alichoambiwa

kweli wa madhabahuni ale madhabahuni
 
Yaani hiiiiii nchi we acha tuuuuuuuuuuuuuuuu mungu pekee

nasikia jakaya anaifwatilia hiiiii kesi kwa udi na uvumba na ole wake hakimu atakae wawashia mooto cha moto atakiona...mnamkumbuka mwankenja.....alianza na moto we.anajua alichoambiwa

kweli wa madhabahuni ale madhabahuni

ebanaeee

aliambiwaje?
 
Yaaani hii ni OVIASI, hakuna jipya na wala si breaking nyuzi. Kesi hii inaweza kufika 2014 na kuonekana hawana hatia.
 
enhee! hapo patamu babaa! cjui kama hili litawezekana iwapo mmiliki kitanzi anaweza kujinyonga, bt kama ni ndotoni na ardhi nyingine tofauti na hii basi itawezekana! tulilazwa na nusu kaputi watanzania, tunaamshwa na wezi walewale walotupiga nusu kaputi je inawezekana kuwahisi wao ndo chanzo cha ucngizi we2, ni ngumu hiyo wakubwa 2jipange kivingine, kwani iliyo tamu ndimini itaendelea kulambwa! watadhalilika siku moja tuwepo au wawepo we2 sie!
 
ilichobaki ni watanznaia kujipanga upya na kuangalia wapi walipokula kihalali wapi wasipostahili kupagusa then tudumbukie wote humo........
hakimu mwankenja alikuwa shujaa sana alipogusa mboni ya jicho kidogo .......
tteeennette mete
 
asante kwa habari hii nadhani wakati umewadia sasa kwa 'wahusika' kuwaendea wote wenye hela za BoT na walio na hela za NBC mimi nimesema ni watanzania wachache mno wenye hela ya halali ya kupita. embu tu jiulize wanazitoa wapi iwapo miradi yenyewe aizunguki hata dar-es-salaam nzima let alone the whole country yet unakuta mtu ana maisha utadhani yuko mbinguni ukilinganisha na mlalahoi.

i dont want to sound like a socialist, because im all for capitalist lakini hii function on the basis of a capital society tunaua nchi kuwapa hela watu ambao hawa invest back. mi ni kijana wa kitanzania (mwafrika) nina rafiki yangu yuko huko bongo mwenye asili ya kimanga ni best wangu siwapi jina. jamaa alikuja mwaka juzi kununua magari yake ya biashara (ma-lorry) ana umri kama wangu early 30's tayari ameshapewa mkopo wa millioni mia nane. hapo hapo baba yake ni tajiri tayari kitu cha kwanza baada ya kupewa mkopo baba alipewa VX mpya na mama akalalamikaa akapewa na yeye ya kwake mpya. Yaani awana nia ya kulipa na ni wengi mno ambao wanafanya michezo hii.

kama uko nje ya tanzania au hata waliopo tanznania ni wadosi wangapi au wamanga wangapi unawaona mlimani. ukija ulaya wadosi wakitanzania wanaosoma huku hawarudi wakisha pata elimu yao. wamanga wanaoenda shule kwa kweli ni wachache wao kuoana tu ndio walichoweka mbele. alafu ukirudi unakuta wao ndio wenye hela eti wanakipaji cha biashara what a stupid explantion. ni hela hizo za benki ndio zinawapa head start kibaya in most cases azilipwi zote. i have been saying this for sometime but people dont want to see what is obvious.

tunarudi tena unakuta watu design ya 'EL' wanasapoti vitu hivi on a greater scale kiasi ambacho hiyo hela ingewasaidia watu wengi mno. hivi mnajua kuna watu tanzania hata kuwasha hii computer awajui. kuna watu wanaishi pembeni ya madibwi ya maji machafu, kuna ma albino wanauliwa polisi wanashidwa kuwa protect, kuna watu wana amka awajui leo mlo unatoka wapi, kuna watoto yatima wanajilisha wenyewe na mengineo mengi utakayo yafikiria ya kimaskini wakati hapo juu hela inayotajwa kuisoma nimeona tabu.

tatizo sio hawa wezi wa kihindi wala wa kimanga kwa sababu kuna waafrica pia wengi tu, tatizo ni watu mnao watetea EL sio mwana siasa jamaa ni mwizi na inabidi atolewe kabisa kwani hana mapenzi na Tanzania inaeleweka Monduli watafunga macho kwa sababu ni wa kwao lakini Tanzania si Monduli kwanza iko nje kabisa ya Arusha. its time to look on the perspective of the whole rather concentrate on individual tunao wasomi wengi mno at the moment nje na ndani ya nchi things have to change tatizo sio Jeetu Patel and co tatizo ni tabia za viongozi wetu hawana mapenzi LONG LIVE TANZANIA
 
Last edited by a moderator:
asante kwa habari hii nadhani wakati umewadia sasa kwa 'wahusika' kuwaendea wote wenye hela za BoT na walio na hela za NBC mimi nimesema ni watanzania wachache mno wenye hela ya halali ya kupita. embu tu jiulize wanazitoa wapi iwapo miradi yenyewe aizunguki hata dar-es-salaam nzima let alone the whole country yet unakuta mtu ana maisha utadhani yuko mbinguni ukilinganisha na mlalahoi.

i dont want to sound like a socialist, because im all for capitalist lakini hii function on the basis of a capital society tunaua nchi kuwapa hela watu ambao hawa invest back. mi ni kijana wa kitanzania (mwafrika) nina rafiki yangu yuko huko bongo mwenye asili ya kimanga ni best wangu siwapi jina. jamaa alikuja mwaka juzi kununua magari yake ya biashara (ma-lorry) ana umri kama wangu early 30's tayari ameshapewa mkopo wa millioni mia nane. hapo hapo baba yake ni tajiri tayari kitu cha kwanza baada ya kupewa mkopo baba alipewa VX mpya na mama akalalamikaa akapewa na yeye ya kwake mpya. Yaani awana nia ya kulipa na ni wengi mno ambao wanafanya michezo hii.

kama uko nje ya tanzania au hata waliopo tanznania ni wadosi wangapi au wamanga wangapi unawaona mlimani. ukija ulaya wadosi wakitanzania wanaosoma huku hawarudi wakisha pata elimu yao. wamanga wanaoenda shule kwa kweli ni wachache wao kuona tu ndio walichoweka mbele. alafu ukirudi unakuta wao ndio wenye hela eti wanakipaji cha biashara what a stupid explantion. ni hela hizo za benki ndio zinawapa head start kibaya in most cases azilipwi zote. i have been saying this for sometime but people dont want to see what is obvious.

tunarudi tena unakuta watu design ya 'EL' wanasapoti vitu hivi on a greater scale kiasi ambacho hiyo hela ingewasaidia watu wengi mno. hivi mnajua kuna watu tanzania hata kuwasha hii computer awajui. kuna watu wanaishi pembeni ya madibwi ya maji machafu, kuna ma albino wanauliwa polisi wanashidwa kuwa protect, kuna watu wana amka awajui leo mlo unatoka wapi, kuna watoto yatima wanajilisha wenyewe na mengineo mengi utakayo yafikiria ya kimaskini wakati hapo juu hela inayotajwa kuisoma nimeona tabu.

tatizo sio hawa wezi kihindi wala kimanga kwa sababu kuna waafrica pia wengi tu, tatizo ni watu mnao watetea EL sio mwana siasa jamaa ni mwizi na inabidi atolewe kabisa kwani hana mapenzi na Tanzania inaeleweka Munduli watafungaa macho kwa sababu ni wa kwao lakini Tanzania si Munduli kwanza iko nje kabisa ya Arusha. its time to look on the perspective of the whole rather concentrate on individual tunao wasomi wengi mno at the moment nje na ndani ya nchi things have to change tatizo sio Jeetu Patel and co tatizo ni tabia za viongozi wetu hawana mapenzi LONG LIVE TANZANIA

Tanzania kuna watu wa aina mbili tu. Wanaotengeneza mavumbi na wanaokula mavumbi.
 
asante kwa habari hii nadhani wakati umewadia sasa kwa 'wahusika' kuwaendea wote wenye hela za BoT na walio na hela za NBC mimi nimesema ni watanzania wachache mno wenye hela ya halali ya kupita. embu tu jiulize wanazitoa wapi iwapo miradi yenyewe aizunguki hata dar-es-salaam nzima let alone the whole country yet unakuta mtu ana maisha utadhani yuko mbinguni ukilinganisha na mlalahoi.

i dont want to sound like a socialist, because im all for capitalist lakini hii function on the basis of a capital society tunaua nchi kuwapa hela watu ambao hawa invest back. mi ni kijana wa kitanzania (mwafrika) nina rafiki yangu yuko huko bongo mwenye asili ya kimanga ni best wangu siwapi jina. jamaa alikuja mwaka juzi kununua magari yake ya biashara (ma-lorry) ana umri kama wangu early 30's tayari ameshapewa mkopo wa millioni mia nane. hapo hapo baba yake ni tajiri tayari kitu cha kwanza baada ya kupewa mkopo baba alipewa VX mpya na mama akalalamikaa akapewa na yeye ya kwake mpya. Yaani awana nia ya kulipa na ni wengi mno ambao wanafanya michezo hii.

kama uko nje ya tanzania au hata waliopo tanznania ni wadosi wangapi au wamanga wangapi unawaona mlimani. ukija ulaya wadosi wakitanzania wanaosoma huku hawarudi wakisha pata elimu yao. wamanga wanaoenda shule kwa kweli ni wachache wao kuoana tu ndio walichoweka mbele. alafu ukirudi unakuta wao ndio wenye hela eti wanakipaji cha biashara what a stupid explantion. ni hela hizo za benki ndio zinawapa head start kibaya in most cases azilipwi zote. i have been saying this for sometime but people dont want to see what is obvious.

tunarudi tena unakuta watu design ya 'EL' wanasapoti vitu hivi on a greater scale kiasi ambacho hiyo hela ingewasaidia watu wengi mno. hivi mnajua kuna watu tanzania hata kuwasha hii computer awajui. kuna watu wanaishi pembeni ya madibwi ya maji machafu, kuna ma albino wanauliwa polisi wanashidwa kuwa protect, kuna watu wana amka awajui leo mlo unatoka wapi, kuna watoto yatima wanajilisha wenyewe na mengineo mengi utakayo yafikiria ya kimaskini wakati hapo juu hela inayotajwa kuisoma nimeona tabu.

tatizo sio hawa wezi wa kihindi wala wa kimanga kwa sababu kuna waafrica pia wengi tu, tatizo ni watu mnao watetea EL sio mwana siasa jamaa ni mwizi na inabidi atolewe kabisa kwani hana mapenzi na Tanzania inaeleweka Monduli watafunga macho kwa sababu ni wa kwao lakini Tanzania si Monduli kwanza iko nje kabisa ya Arusha. its time to look on the perspective of the whole rather concentrate on individual tunao wasomi wengi mno at the moment nje na ndani ya nchi things have to change tatizo sio Jeetu Patel and co tatizo ni tabia za viongozi wetu hawana mapenzi LONG LIVE TANZANIA

Kwa kweli kama hali halisi ndio hii tunakazi kubwa ya kufanya Tanzania ili matunda ya uhuru yawe kwa faida ya wengi na sio mafisadi wachache kama ilivyo sasa.
 
Yaani hiiiiii nchi we acha tuuuuuuuuuuuuuuuu mungu pekee

nasikia jakaya anaifwatilia hiiiii kesi kwa udi na uvumba na ole wake hakimu atakae wawashia mooto cha moto atakiona...mnamkumbuka mwankenja.....alianza na moto we.anajua alichoambiwa

kweli wa madhabahuni ale madhabahuni

Yaani Tanzania kama vile tumeleweshwa na hatujijui tunakoelekea,watu wanakuja kutoka huko nje hawana kitu.Wanatuibia tena kimachomacho huku wakisaidiwa na vibaraka wachache na sisi tunakodoa macho tuu,hivi kweli sisi watanzania wazima?

Hata kama JK anafuatuilia hapa hatoki mtu,wametudanganya,wametuibia,sasa tumeamka wa watanzania wa leo sio wa jana, ni ama zao mafisadi ama zetu, hatoki mtu hapa.
 
Back
Top Bottom