OSOKONI
JF-Expert Member
- Oct 20, 2011
- 10,965
- 5,336
Hatima ya Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini (CCM), Virajilal Jitu Son itajulikana leo wakati Mahakama Kuu Kanda ya Arusha itakapotoa hukumu ya kesi ya kupinga ubunge wake iliyofunguliwa na aliyegombea ubunge wa jimbo hilo, Laurence Surumbu Tara (NCCR Mageuzi).
Kesi hiyo namba 12/2010 ipo mbele ya Jaji Fatuma Massengi na ilifunguliwa Novemba 2010 na kuanza kusikilizwa Februari 16, mwaka huu huku wadaiwa wakiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo na Jituson.
Novemba 2010, Tara ambaye ni Diwani wa Kata ya Bashnet alifungua kesi hiyo ambayo ilianza kusikilizwa Februari 16, mwaka huu akiiomba Mahakama hiyo imtangaze kuwa mbunge halali wa jimbo hilo kwani ndiye mshindi halali wa jimbo hilo na kudai kuwa alishinda kwa tofauti ya kura 58 baada ya kupata kura 32,248 na Jituson kura 32,190.
Tara katika madai yake, aliiomba Mahakama hiyo itangaze kuwa matokeo yaliyompa ushindi mbunge wa sasa ni batili kwani yalikiuka taratibu za kisheria za uchaguzi na kanuni zake mwaka 2010.
Chanzo: Gazeti la MWANANCHI
Kesi hiyo namba 12/2010 ipo mbele ya Jaji Fatuma Massengi na ilifunguliwa Novemba 2010 na kuanza kusikilizwa Februari 16, mwaka huu huku wadaiwa wakiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo na Jituson.
Novemba 2010, Tara ambaye ni Diwani wa Kata ya Bashnet alifungua kesi hiyo ambayo ilianza kusikilizwa Februari 16, mwaka huu akiiomba Mahakama hiyo imtangaze kuwa mbunge halali wa jimbo hilo kwani ndiye mshindi halali wa jimbo hilo na kudai kuwa alishinda kwa tofauti ya kura 58 baada ya kupata kura 32,248 na Jituson kura 32,190.
Tara katika madai yake, aliiomba Mahakama hiyo itangaze kuwa matokeo yaliyompa ushindi mbunge wa sasa ni batili kwani yalikiuka taratibu za kisheria za uchaguzi na kanuni zake mwaka 2010.
Chanzo: Gazeti la MWANANCHI