..hii imetoka kwenye gazeti la raia mwema.
..Hatibu Senkoro amezungumza mambo mengi kuanzia masuala ya sekta ya madini, historia yake, mpaka mahusiano yake na Basil Pesambili Mramba.
..Hatibu Senkoro amezungumza mambo mengi kuanzia masuala ya sekta ya madini, historia yake, mpaka mahusiano yake na Basil Pesambili Mramba.
kusoma interview nzima bonyeza hapa.Raia Mwema: Kuna hisia zimeibuliwa kuwa ilipotokea umemdhamini Mramba (aliyekuwa Waziri Basil Mramba) waliamini mnamiliki hisa katika Mgodi wa Dhahabu Geita, unasemaji?
Senkoro: Aaah! Hilo swali lako sina hakika nalo. Lakini ni kweli mimi nimemdhamini Mheshimiwa Mramba. Kama nilivyoeleza, mimi na Mheshimiwa Mramba tunajuana tangu NDC miaka mingi tukiwa bado vijana.
Tumesoma Tabora School. Tumefanya kazi wote Williamson Diamonds. Tumehamishwa wote kutoka Williamson Diamonds kwenda NDC. Tumefanya kazi wote NDC.
Wake zetu wamesoma shule moja pamoja. Wanafahamiana. Watoto wetu wanafahamiana. Mimi Mramba ni ndugu yangu. Simwoni kama waziri. Mramba namwona kama ndugu kutokana na uhusiano huo, mimi ni Mpare yeye ni Mchaga, lakini Mramba ni ndugu yangu damu-damu.