BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,006
Hati za Jeetu Patel zatiliwa shaka
Timothy Boniface
Daily News; Tuesday,December 23, 2008 @21:15
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana ilitoa agizo la kufanyiwa uthamini upya moja ya mali zilizotumika katika moja ya hati ya dhamana ya washitakiwa Jeetu Patel na wenzake kutokana na kubainika kuwa ina makosa.
Hakimu Mkazi Richard Kabate alisema hati hiyo ambayo ni ya shamba lililoko Bagamoyo mkoani Pwani, iliyotumika hapo awali kwa ajili ya kuwadhamini washitakiwa Jeetu Patel, Devendra Vinodbhai Patel na Amit Nandy ilikuwa na makosa ambayo yanahitaji kufanyiwa uthamini upya.
Washitakiwa hao wanatuhumiwa katika wizi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania. Hakimu Kabate aliuagiza upande wa utetezi kufanya uthamini wa hati hiyo ili kurekebisha makosa yaliyopo.
Katika kesi hiyo, washitakiwa kwa pamoja wanashitakiwa kwa tuhuma za kula njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo, kuiba na kujipatia Sh bilioni 2.6 kwa kutumia kampuni yao ya Bencon ya Dar es Salaam. Inadaiwa kuwa waliiba fedha hizo baada ya kudanganya kuwa Kampuni ya Matsushita Electric Trading Company iliwapa jukumu la kulipwa fedha hizo kupitia kampuni yao ya Bencon International Ltd.
Washitakiwa hao pia kwa pamoja wanashitakiwa kula njama, kughushi, kuiba na kujipatia Sh bilioni 7.9 kwa kutumia kampuni hiyo ya Bencon International Ltd. Washitakiwa hao ni miongoni mwa washitakiwa 21 ambao wamefikishwa mahakamani tangu kuanza kwa kesi hiyo ya wizi wa mabilioni ya fedha za Benki Kuu ya Tanzania katika Akaunti ya Madeni ya Nje. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 30, mwaka huu.
Timothy Boniface
Daily News; Tuesday,December 23, 2008 @21:15
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana ilitoa agizo la kufanyiwa uthamini upya moja ya mali zilizotumika katika moja ya hati ya dhamana ya washitakiwa Jeetu Patel na wenzake kutokana na kubainika kuwa ina makosa.
Hakimu Mkazi Richard Kabate alisema hati hiyo ambayo ni ya shamba lililoko Bagamoyo mkoani Pwani, iliyotumika hapo awali kwa ajili ya kuwadhamini washitakiwa Jeetu Patel, Devendra Vinodbhai Patel na Amit Nandy ilikuwa na makosa ambayo yanahitaji kufanyiwa uthamini upya.
Washitakiwa hao wanatuhumiwa katika wizi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania. Hakimu Kabate aliuagiza upande wa utetezi kufanya uthamini wa hati hiyo ili kurekebisha makosa yaliyopo.
Katika kesi hiyo, washitakiwa kwa pamoja wanashitakiwa kwa tuhuma za kula njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo, kuiba na kujipatia Sh bilioni 2.6 kwa kutumia kampuni yao ya Bencon ya Dar es Salaam. Inadaiwa kuwa waliiba fedha hizo baada ya kudanganya kuwa Kampuni ya Matsushita Electric Trading Company iliwapa jukumu la kulipwa fedha hizo kupitia kampuni yao ya Bencon International Ltd.
Washitakiwa hao pia kwa pamoja wanashitakiwa kula njama, kughushi, kuiba na kujipatia Sh bilioni 7.9 kwa kutumia kampuni hiyo ya Bencon International Ltd. Washitakiwa hao ni miongoni mwa washitakiwa 21 ambao wamefikishwa mahakamani tangu kuanza kwa kesi hiyo ya wizi wa mabilioni ya fedha za Benki Kuu ya Tanzania katika Akaunti ya Madeni ya Nje. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 30, mwaka huu.