Hati za Jeetu Patel zatiliwa shaka

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Hati za Jeetu Patel zatiliwa shaka
Timothy Boniface
Daily News; Tuesday,December 23, 2008 @21:15

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana ilitoa agizo la kufanyiwa uthamini upya moja ya mali zilizotumika katika moja ya hati ya dhamana ya washitakiwa Jeetu Patel na wenzake kutokana na kubainika kuwa ina makosa.

Hakimu Mkazi Richard Kabate alisema hati hiyo ambayo ni ya shamba lililoko Bagamoyo mkoani Pwani, iliyotumika hapo awali kwa ajili ya kuwadhamini washitakiwa Jeetu Patel, Devendra Vinodbhai Patel na Amit Nandy ilikuwa na makosa ambayo yanahitaji kufanyiwa uthamini upya.

Washitakiwa hao wanatuhumiwa katika wizi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania. Hakimu Kabate aliuagiza upande wa utetezi kufanya uthamini wa hati hiyo ili kurekebisha makosa yaliyopo.

Katika kesi hiyo, washitakiwa kwa pamoja wanashitakiwa kwa tuhuma za kula njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo, kuiba na kujipatia Sh bilioni 2.6 kwa kutumia kampuni yao ya Bencon ya Dar es Salaam. Inadaiwa kuwa waliiba fedha hizo baada ya kudanganya kuwa Kampuni ya Matsushita Electric Trading Company iliwapa jukumu la kulipwa fedha hizo kupitia kampuni yao ya Bencon International Ltd.

Washitakiwa hao pia kwa pamoja wanashitakiwa kula njama, kughushi, kuiba na kujipatia Sh bilioni 7.9 kwa kutumia kampuni hiyo ya Bencon International Ltd. Washitakiwa hao ni miongoni mwa washitakiwa 21 ambao wamefikishwa mahakamani tangu kuanza kwa kesi hiyo ya wizi wa mabilioni ya fedha za Benki Kuu ya Tanzania katika Akaunti ya Madeni ya Nje. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 30, mwaka huu.
 
Hati za Jeetu Patel zatiliwa shaka
Timothy Boniface
Daily News; Tuesday,December 23, 2008 @21:15

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana ilitoa agizo la kufanyiwa uthamini upya moja ya mali zilizotumika katika moja ya hati ya dhamana ya washitakiwa Jeetu Patel na wenzake kutokana na kubainika kuwa ina makosa.

Hakimu Mkazi Richard Kabate alisema hati hiyo ambayo ni ya shamba lililoko Bagamoyo mkoani Pwani, iliyotumika hapo awali kwa ajili ya kuwadhamini washitakiwa Jeetu Patel, Devendra Vinodbhai Patel na Amit Nandy ilikuwa na makosa ambayo yanahitaji kufanyiwa uthamini upya.

Washitakiwa hao wanatuhumiwa katika wizi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania. Hakimu Kabate aliuagiza upande wa utetezi kufanya uthamini wa hati hiyo ili kurekebisha makosa yaliyopo.

Katika kesi hiyo, washitakiwa kwa pamoja wanashitakiwa kwa tuhuma za kula njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo, kuiba na kujipatia Sh bilioni 2.6 kwa kutumia kampuni yao ya Bencon ya Dar es Salaam. Inadaiwa kuwa waliiba fedha hizo baada ya kudanganya kuwa Kampuni ya Matsushita Electric Trading Company iliwapa jukumu la kulipwa fedha hizo kupitia kampuni yao ya Bencon International Ltd.

Washitakiwa hao pia kwa pamoja wanashitakiwa kula njama, kughushi, kuiba na kujipatia Sh bilioni 7.9 kwa kutumia kampuni hiyo ya Bencon International Ltd. Washitakiwa hao ni miongoni mwa washitakiwa 21 ambao wamefikishwa mahakamani tangu kuanza kwa kesi hiyo ya wizi wa mabilioni ya fedha za Benki Kuu ya Tanzania katika Akaunti ya Madeni ya Nje. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 30, mwaka huu.

Uandishi wa Tanzania, unaweza kuchana gazeti. Hati ina makosa gani? Hayasemwi. Hata kuripoti tu, ni shida na hili ndio Daily News au Mkuu BAK ndo umetafsiri from original? No wonder RA na EL waliwanunua wote kama kuku wa kitoweo
 
Uandishi wa Tanzania, unaweza kuchana gazeti. Hati ina makosa gani? Hayasemwi. Hata kuripoti tu, ni shida na hili ndio Daily News au Mkuu BAK ndo umetafsiri from original? No wonder RA na EL waliwanunua wote kama kuku wa kitoweo
Ha hahaahahaaaaaaaaaaaa!

Mwalimu Zawadi, ngoja nikuudhi zaidi, angalia hii headline kwenye press leo:


Lowassa, Msekwa kortini

• Wadaiwa kukiuka amri ya Mahakama Kuu


jumatano, 24 desemba 2008
TANZANIA DAIMA

pic_happy2.jpg


na Happiness Katabazi


WASIWASI wa kuongezeka kwa idadi ya viongozi waandamizi, walio madarakani na waliong'atuka wanaoweza kufikishwa mahakamani kwa makosa mbalimbali sasa umetawala Jiji la Dar es Salaam.

Kuibuka kwa wasiwasi huo, kunatokana na hatua ya Kampuni ya Uwakili ya Marando & Mnyele ya Dar es Salaam kuwasilisha ombi katika Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi kutaka kukamatwa na kutupwa gerezani kwa vigogo kadhaa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kosa la kukiuka amri ya mahakama.

Ombi hilo
lililowasilishwa na kampuni hiyo ya uwakili kwa niaba ya mteja wake, Ibrahim G. Alibhai, linaiomba mahakama hiyo itoe amri ya kukamatwa Baraza la Wadhamini wa CCM na viongozi wengine kadhaa wa chama hicho kwa kosa hilo.

Linaeleza kuwa, Alibhai ambaye ni mlalamikaji katika kesi ya msingi ya ardhi namba 81 ya mwaka huu, anawashtaki wajumbe wa Baraza la Wadhamini wa CCM, Mwenyekiti wa CCM Tawi la Gerezani, Ismail Idrisa, katibu wa chama wa tawi hilo na mtu mwingine anayetajwa kwa jina la Abdulrahman Twalibu.

Kwamba mlalamikaji anataka alipwe sh milioni 500 na CCM ambayo ilivamia nyumba yake, namba 107, kitalu namba 11, block 53, iliyoko Mtaa wa Sikukuu, Dar es Salaam, bila kujali kama yeye ni mmiliki halali wa nyumba hiyo.

Hati ya ombi hilo, inawataja wadhamini wa CCM ambao mahakama inaombwa iamuru wakamatwe kuwa ni pamoja na waziri wakuu wastaafu wawili, Rashid Mfaume Kawawa, Jaji Joseph Warioba na Edward Lowassa, ambaye alijiuzulu wadhifa huo mapema mwaka huu.

Wengine wanaotajwa kuwa wajumbe wa baraza hilo ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Pius Msekwa, Ahmed Ameir Ally, Khadija Jabiri, Peter Kisumo, Job Lusinde, Khamisi Juma Mkandara na Juma Ame Juma.

Hati ya maombi hayo ya mlalamikaji mahakamani, inaeleza kuwa aliwasilisha maombi hayo juzi, Desemba 22 mwaka huu. Inaeleza Mei 8 mwaka huu, Jaji wa mahakama hiyo, Alice Chinguwile, alitoa amri ya zuio dhidi ya wadaiwa wote, mawakala, wafanyakazi na watumishi kuacha kuendelea na ujenzi hadi shauri la msingi lililopo mahakamani hapo litakapomalizika.

Hati ilieleza Desemba 12 mwaka huu, mlalamikaji alitembelea eneo husika na kukuta wadaiwa wakiendelea na ujenzi, kinyume cha amri hiyo ya mahakama na kwamba wadaiwa wana mpango wa kukamilisha ujenzi wa jengo hilo, ili waweze kulipangisha.

Mlalamikaji alidai alipata taarifa za kuendelea kwa ujenzi huo kutoka kwa wakili wake, Mabere Marando, aliyeeleza kuwa kitendo hicho cha kukaidi zuio la amri ya mahakama ni kukiuka amri halali ya mahakama iliyotolewa Mei 8, mwaka huu.

Mlalamikaji aliiomba mahakama kuwakamata na kuwatupa gerezani wadaiwa wote bila kutoa adhabu mbadala ya faini kwa kukiuka amri hiyo.

Alibhai alifungua kesi ya msingi chini ya kampuni ya mawakili hao katika mahakama hiyo, Aprili 14 mwaka huu dhidi ya wadhamini wa CCM na viongozi wa chama hicho, akitaka alipwe sh milioni 500 kwa kuwa waliingia katika eneo hilo bila idhini yake.

Kampuni ya mawakili hao ilieleza kuwa anayedharau amri halali ya mahakama kwa mujibu ya sheria ya mwenendo wa kesi za madai, sura ya 33 ya mwaka 1966, anapaswa kutumikia kifungo cha miezi sita gerezani au kukamatwa kwa mali zake.
Ha hahaahahahahaaaaaa!

Dada Happy muongo ile mbaya unaambiwa. Hata yeye mwenyewe anatucheka!
 
Ha hahaahahaaaaaaaaaaaa!

Mwalimu Zawadi, ngoja nikuudhi zaidi, angalia hii headline kwenye press leo:


Ha hahaahahahahaaaaaa!

Huyo dada Happy muongo ile mbaya unaambiwa. Halafu na yeye mwenyewe anacheka!

Ulitaka anune kama yule mnuka samaki wako? ebo....maisha mafupi wewe...ununenune ili iweje sasa....
 
Uandishi wa Tanzania, unaweza kuchana gazeti. Hati ina makosa gani? Hayasemwi. Hata kuripoti tu, ni shida na hili ndio Daily News au Mkuu BAK ndo umetafsiri from original? No wonder RA na EL waliwanunua wote kama kuku wa kitoweo

Sijatafsiri chochote hapo. Kwa maoni yangu huyu mwandishi labda hakuhangaika kutafuta sababu za hizi hati kutiliwa mashaka labda kwa kutaka kutoa article yake haraka au wahusika wenye undani wa habari hii hawakutaka kutoa info zaidi kulikoni hata hati hizo zikawa na walakini. Tusubiri kama habari hii ina ukweli basi tutajua ni sababu zipi hati hizo zimetiliwa mashaka. Subira yavuta heri.
 
uyu Happiness Katabazi si ndo FM Academia wamemwimba kwenye nyimbo ya inayoitwa "Heshima ya mwanamke" so mnatarajia nini kutoka kwake?????wizi mtupuuu...
 
Date::12/23/2008
Jeetu Patel, wenzake wataka tathmini mpya ya mali zao
Nora Damian
Mwananchi

MFANYABIASHARA Jayantkumar Chandubhai Patel (Jeetu Patel) na wenzake ambao wanakabiliwa na kesi ya tuhuma za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Malimbikizo ya Madeni ya Nje (EPA), wametakiwa kuwasilisha upya mahakamani ripoti ya tathmini za mali walizoweka kama dhamana baada ya kuonekana mapungufu.

Uamuzi huo ulitolewa jana na Hakimu Mkazi, Richard Kabate wa Kisutu baada ya upande wa utetezi kuwasilisha maombi mahakamani hapo wakiomba ripoti ya tathmini ya mali waliyoweka kama dhamana ifanyiwe tathmini upya baada ya kubadilishwa jina la kampuni.

Wakili wa washtakiwa hao, Martin Matunda alidai mahakamani hapo kuwa Julai 2 mwaka 1995 washtakiwa walibadilisha jina la Kampuni ya Azania Investment Ltd na kuwa Noble Azania Investment Ltd, lakini hawakuomba kubadilisha hati ya kampuni.

"Baada ya washtakiwa kufikishwa mahakamani Novemba 5 mwaka huu na moja ya masharti ya dhamana kuwataka walete fedha au hati, tulilazimika kwenda Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kubadilisha hati ya kampuni na ripoti ya tathmini," alisema Matunda.

Alieleza kuwa ripoti hiyo ilitolewa Novemba 7 mwaka huu ikiwa na jina la Azania na Novemba 14 mwaka huu ilitolewa hati ya kampuni ikionyesha kuwa kampuni hiyo imebadilishwa jina na kuwa Noble Azania Investment Ltd.

Alieleza kuwa waligundua kuna mapungufu kwani hati ya kampuni ndiyo ilitakiwa itolewe kwanza kabla ya ripoti ya uthamini.

Hakimu Kabate aliahirisha shauri hilo hadi Desemba 30 mwaka huu upande wa utetezi utakapowasilisha ripoti hiyo.

Jeetu Patel na wenzake Kentan Chohan na Amit Nandi wanashtakiwa kwamba,mwaka 2005 walikula njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka bandia na kuiibiaBoT Sh3,323,974,942.30 kupitia kampuni yao ya Navy Cut Tobacco (T) Ltd kwamadai kuwa imerithishwa deni la kiasi hicho cha pesa kutoka kampuni yaMatsushita Electric Trading Company ya Japan.

Katika kesi hiyo Jeetu na wenzake walipata dhamana baada ya kuwasilisha hati za mali zisizohamishika zenye thamani ya zaidi ya Sh 3.5 bilioni.
 
pumbafuuuuuuuuuuuuuuuuu zao wooooooooote mahakamani na majaji zao
unatoa dhamana ndio unadai ......oohhhhhhhhhhhhh shit hawana maana kabisa
 
Back
Top Bottom