Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,461
- 39,928
Mganga Mkuu wa Tanzania (Chief Medical Officer) Dr. Deo Mtasiwa amedaiwa na wadau mbalimbali wa masuala ya afya nchini kwa kushindwa kutoa maagizo ya kuondolewa kwa vifaa vya kupimia virusi vya Ukimwi (HIV) kufuatia taarifa ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kuwa vifaa hivyo vina kasoro kubwa na hivyo vinapaswa kuondolewa kwenye matumizi ya binadamu mara moja.
Kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika Dr. Mtasiwa alipokea barua toka Shirika hilo ikimtaarifu juu ya mapungufu hayo makubwa ya vifaa vya SD Bioline HIV-1/2 3.0 vinavyotengenezwa huko Korea ya Kusini na kampuni ya Standard Diagnostic ya Jiji la Kyonggi-do.
Hata hivyo tangu kupokea taarifa hiyo toka WHO pamoja na taarifa toka kampuni ya Standard Diagnostic yenye kuthibitisha maamuzi ya WHO Dr. Mtasiwa hajachukua hatua yoyote ya kutahadharisha wanunuzi na watumiaji wa vifaa hivyo ambavyo vingi vinamuda wa matumizi unaoishia mwaka 2012 na 2013.
Maisha ya vifaa hivyo ni miezi 24 (sawa na miaka miwili) kabla havijaondolewa kwa kupita muda wake wa matumizi.
Kutokana na kinachodaiwa kuwa ni uamuzi huo wa Dr. Mtasiwa ambaye anatajwa na vyanzo mbalimbali kuwa na "ushawishi mkubwa pale Wizarani" hata kuzidi baadhi ya watendaji wa juu maisha ya wananchi wa Tanzania yako hatarini kwani matumizi ya vifaa hivyo ambavyo WHO imesema inauwezekano wa kuwa na uharibu wa asilimia 50 majibu yanayotolewa kupitia vifaa hivyo yaweza kuwa na makosa makubwa.
Habari zaidi: Fikrapevu.com
Kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika Dr. Mtasiwa alipokea barua toka Shirika hilo ikimtaarifu juu ya mapungufu hayo makubwa ya vifaa vya SD Bioline HIV-1/2 3.0 vinavyotengenezwa huko Korea ya Kusini na kampuni ya Standard Diagnostic ya Jiji la Kyonggi-do.
Hata hivyo tangu kupokea taarifa hiyo toka WHO pamoja na taarifa toka kampuni ya Standard Diagnostic yenye kuthibitisha maamuzi ya WHO Dr. Mtasiwa hajachukua hatua yoyote ya kutahadharisha wanunuzi na watumiaji wa vifaa hivyo ambavyo vingi vinamuda wa matumizi unaoishia mwaka 2012 na 2013.
Maisha ya vifaa hivyo ni miezi 24 (sawa na miaka miwili) kabla havijaondolewa kwa kupita muda wake wa matumizi.
Kutokana na kinachodaiwa kuwa ni uamuzi huo wa Dr. Mtasiwa ambaye anatajwa na vyanzo mbalimbali kuwa na "ushawishi mkubwa pale Wizarani" hata kuzidi baadhi ya watendaji wa juu maisha ya wananchi wa Tanzania yako hatarini kwani matumizi ya vifaa hivyo ambavyo WHO imesema inauwezekano wa kuwa na uharibu wa asilimia 50 majibu yanayotolewa kupitia vifaa hivyo yaweza kuwa na makosa makubwa.
Habari zaidi: Fikrapevu.com