Kauli ya JK haijitoshelezi kwa namna yoyote.
1. Kuwataja wapinzani kuwa wameshikilia bango vita ni Uongo. Hakuna kumbu kumbu za wapinzani kuliongelea suala hilo katika mizani aliyoongelea JK. Kama ipo mkuu Gaijin tujulishe.
2. Watu waliotoa kauli kama viongozi wa serikali ni Sitta, Membe na EL. Hawa ndio war mongering kwa kauli za JK.
Endapo si hao, basi tupe mtu mmoja nje ya serikali na mwenye hadhi ya kisiasa aliyetoa kauli za kwenda vitani.
Tusicheze na maneno, JK hakuongea kama Mwanadiplomasia. Alichosema ni utaratibu wake wa kawaida wa kutaka kumfurahisha kila mtu ili asionekane mbaya. Hii si mara ya kwanza au ya pili au ya tatu ni 'norm' kwa JK
Nina uhakika Membe, Sitta na Lowassa hawakufurahishwa. JK alitakiwa aongelee msismamo wa nchi si kuwatuhumu wenzake. Yeye kama Amir jeshi hakuwa na sababu ya kujitambulisha kuwa ndiye amir jeshi. Hii maana yake ni kutaka kuonyesha kuwa yoyote aliyesema ni bla bla tu kwasababu yeye ndiye mwenyewe. Yoyote ni nani?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.