platozoom
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 9,364
- 11,150
Hivi juzi Nilikuwa napita mahali mara nikawaona wazee wawili wamesimama kimtindo kwenye kona ya nyumba (babu around 70s na bibi 60s) nikashikwa na udadisi nikabana karibu yao na kusikiliza maongezi yao:
Babu; jana nilikuita lakini hukuja
Bibi: mmh miguu ilikuwa inauma sana halafu wewe uwe usiwe unamtuma yule mjukuu wangu anaweza kujifunza tabia mbaya.
Babu; sawa lakini ujue nakupenda sana,nashindwa kuvumilia.Sasa lile ombi langu vipi?
Bibi; nilikwambia uwe mvumilivu nitakupa jibu
Babu; Muda mrefu unanizungusha,leo nipe tu jibu la kueleweka umri unakwenda na nguvu zinapungua
Bibi:Wewe hukumbuki nilipokuwa binti nilivyokuwa nakutukana ukiniiita?shukuru Mungu sasa hivi nakubali kuongea na wewe.Vumilia tu nitakupa jibu la kueleweka mvumilivu hula mbivu
Babu; (Huku akilengwalengwa na machozi) sawa...kama nimesubiria zaidi ya miaka arobaini..nitajitahidi tu kuvumilia.
Baada ya hapo ikabidi niondoke huku nikisononeka moyoni kwa namna babu alivyoppigwa tarehe,lakini pia nikajaribu kufanya comparison na namna kizazi chetu cha sasa kinavyotongoza......................!
Babu; jana nilikuita lakini hukuja
Bibi: mmh miguu ilikuwa inauma sana halafu wewe uwe usiwe unamtuma yule mjukuu wangu anaweza kujifunza tabia mbaya.
Babu; sawa lakini ujue nakupenda sana,nashindwa kuvumilia.Sasa lile ombi langu vipi?
Bibi; nilikwambia uwe mvumilivu nitakupa jibu
Babu; Muda mrefu unanizungusha,leo nipe tu jibu la kueleweka umri unakwenda na nguvu zinapungua
Bibi:Wewe hukumbuki nilipokuwa binti nilivyokuwa nakutukana ukiniiita?shukuru Mungu sasa hivi nakubali kuongea na wewe.Vumilia tu nitakupa jibu la kueleweka mvumilivu hula mbivu
Babu; (Huku akilengwalengwa na machozi) sawa...kama nimesubiria zaidi ya miaka arobaini..nitajitahidi tu kuvumilia.
Baada ya hapo ikabidi niondoke huku nikisononeka moyoni kwa namna babu alivyoppigwa tarehe,lakini pia nikajaribu kufanya comparison na namna kizazi chetu cha sasa kinavyotongoza......................!