Freema Agyeman
JF-Expert Member
- Mar 3, 2011
- 3,666
- 3,524
My wife ni mjamzito wa mwezi 1 tu! lakini visa na mikasa haviishi hapa ndani kwanza;
-Nilipigwa BAN kumsogelea tukiwa tumelaa usiku japo tunashare shuka moja.
-Jana nimeamka asubuhi nikakuta perfume zangu zote hazipo kwenye dressing kuuliza jibu "sijui"
-Kila nikifika home jioni nakuta keshalala hata kula hali ati ye kashiba tangu ale mchana akiwa job.
-Ameniambia ana hamu ya kula chakula nilichopika mimi,maskini mimi kupika yenyewe anajua kabisa sijui lakini anataka nianze kuzama kitchen kukorofisha msosi.
-Hasira sasa ni balaa yaani ananipeleka kama katoto kadogo mpaka sometime najiuliza nishakuwa zoba nini?
Mmmmmmmh nahitaji pole,
Kwanza nafikiria nitatoboa kweli mda wote huu uliobaki bila ku-do kweli?, Sababu dalili zote za kutokupewa zimeshawekwa wazi sana.
Ama saa ingine nafikiri nitafute kanyumba kadogo ama niungane na chama cha watumia soap aka mkonos?
Pili nawaza what will be the next movie? sababu kila kukicha anakuja na mpya.
Tatu naomba mungu asije akanipa masharti ya kulala chini coz hali haieleweki chochote naweza ambiwa.
Ebu naomba ushauri wenu hapa wababa wenzangu.Kama nanyi mlipitia haya.
Na we mdada ebu niambie ulikuwa hivi ulipokuwa mjamzito?
kazidi, hebu mketishe chini na ukiwa na sura ya kiume ambayo hajawahi kuiona toka muanze mahusiano, kwa busara mueleze anavyokukwaza. Hata kama ni mimba hebu ajitahidi kidogo kutimiza wajibu wake labda kama ameshauriwa vinginevyo na daktari.
Endelea kutimiza wajibu wako.