Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Walionena kuwa mapenzi ni ya wawili waliona mbali. Tena mbali sana. Wengi hujaribu kuomba ushauri hapa na pale, huku na kule lakini haisaidii kwa kuwa huwezi kueleza kilichojiri kati yako na mwenzako mpaka kieleweke. Ni ninyi wawili tu mnaojua nini kilitokea. Kama mmeshindwa kukitatua msitegemee eti mtamueleza mwingine aelewe. Sana sana mtaishia kuchochea umbea na majungu. Labda muende pamoja kwa mshauri nasaha. Ila hata yeye hataelewa. Atachoweza ni kuwasaidia tu muweze kueleweshana na kutatua tatizo lenu wenyewe.