Mzalendowetu
Member
- May 22, 2012
- 87
- 34
Hasheem Thabit, mtanzania mwanamichezo mwenye mafanikiozaidi Tanzania, amegonga Bajaj. Ni kwamba alikuwa akijaribu kuipita gari iliyombele yake, bila kujua kumbe mbele ya hiyo gari kulikuwa na bajaj ndipoakalazimika kurudi upande wa kushoto ambao bajaj ilipo na kuigonga. Alijaribukukimbia lakini alipofika Kijitonyama kwenye mataa ya Sayansi alikwama kutokanana foleni. Dereva wa bajaji aliposhuka na kuanza kumhoji Hashim nikwa nini amemgonga na ni vipi Hasheem atalipa fidia kwa uharibifu wa bajajaliosababisha, cha kushangaza, star huyo alishuka na kuanza kumpa kibanodereva wa bajaj kwa kumpiga mitama ya kiutu uzima. Nakumbuka mwaka 2010 Hashim alishawahikuzikunja kavukavu na TID wakiwa Bilicanas.Ndugu zangu, huu si ustaarabu hata kidogo. Pia, ni aibu nafedheha kubwa kwa mtu maarufu kama Hasheem kwa vitendo anavyovifanya. Naaminikabisa star huyu alikuwa na uwezo wa kumalizana na huyu mwendesha bajaj bilahata kujichukulia sheria mkononi hasa ukizingatia yeye ndiye alikuwa mwenyemakosa. Kwa picha nahabari zaidi, tembelea Source: www.sethought.blogspot.com