Hivi karibuni ndugu zetu waislamu waliadhimisha sikukuu ya idd mubarak ijulikanayo kama sikukuu ya kuchinja. Kila msikiti ulichinja na kugawa nyama kwa wahumini wao. Kero imekuja baada ya baadhi ya misikiti kuwa na kiasi kikubwa cha nyama na nyingine kuachwa imetelekezwa misikitini hadi kuozeana kama ilivyokutwa katika msikiti wa jirani na maktaba mkoani Mtwara. Watumiaji wa maktaba wanashindwa kujisomea na wahudumu kuikimbia maktaba. Harufu ni kali mno hadi majirani wamehama makazi yao. Swali ni kwa nini hawakuchinja nyama ya kuwatosha au kuigawa kwa watu wengine? Nawasilisha...