Harambee Ya Mjane Wa Mwangosi Imehitimishwa Jana Jumapili..

Chipolopolo,

Asante sana. Nakubaliana nawe kuhusu haja ya mimi kuweka ufafanuzi kuhusu picha za CUF Arusha kwenye Mjengwablog. Ukweli zimewekwa na mmoja wa walio kwenye timu ya Mjengwablog. Yumkini zina kasoro, lakini aliyeweka hakuwa na dhamira mbaya. Tukumbuke, hizi kazi zinafanywa na wanadamu. Makosa hutokea. Pale yanapotokea, basi, muhimu ni kukosoana ili marekebisho yafanyike.

Maana, ukiacha kublogu, nami nina kibarua changu kingine. Ndio maana ya kuwepo kwa wengine kwenye timu ya Mjengwablog ili wanisaidie. Na kutokana na kibarua changu, wakati mwingine yaweza kupita siku nzima au hata siku mbili bila mimi kuingia Mjengwablog. Na ninapoingia, nami naweza kuzishangaa picha za CUF Arusha kama wanavyoweza kushangaaa watembeleaji wengine. Na huo ndio ukweli kwa mazingira yangu ya sasa.
Usiku mwema.
Maggid
Iringa
0788 111 765

Maggid:

Huo ndio uungwana.Binafsi nimekuelewa vizuri, kabisa! Asante kwa kujali.
 
wangapi wameweza kufanya hivyo kama alivyofanya mjengwa?,ifike pahala tuache kuchanganya siasa na mambo mhimu,picha za mkutano wa Cuf wapi na wapi na michango ya mjane wa mwangosi? -by karagosi
 
big-up sana mjengwa kwa ufafanuzi wako,hakuna binadamu mtimilifu na hata hao waliokukosoa kwa hisia kali nao wanamapungufu yao kama binadamu,lakini waswahili wanasema muungwana vitendo,umekuwa muungwana kwa kuonyesha kwa vitendo
 
Ndugu zangu,

Ni harambee iliyoratibiwa na mtandao wa Mjengwablog. Imehitimishwa jana Oktoba 30 kama ilivyopangwa. Imefanikiwa. Jioni ya leo nitaweka mtandaoni ( Mjengwablog.com)jumla iliyopatikana, majina ya waliochanga na utaratibu wa kukabidhi michango hiyo.

Maggid Mjengwa,
Iringa.
Wewe ni gamba tu huna lolote, juzi umeweka picha za mwaka 2010 ukitaka watu waamini ni za mkutano wa CUF Arusha ushindwe na ulegee...
 
nitaomba ufafanuzi kwa mjengwa kupitia hapa JF,kuna hizi press club(klabu za waandishi wa habari) zinakusanya michango kwa ajili ya rambi rambi ya marehemu mwangosi,je hiyo michango nayo itakufikia? au wanazipitishia wapi hadi zimfikie mjane wa marehemu?,hofu yangu hapa ni hiyo tabia iliyoota mizizi ya kuchakachua mpaka michacgo ya waliofariki,mungu atawahukumu
 
Chipolopolo,

Asante sana. Nakubaliana nawe kuhusu haja ya mimi kuweka ufafanuzi kuhusu picha za CUF Arusha kwenye Mjengwablog. Ukweli zimewekwa na mmoja wa walio kwenye timu ya Mjengwablog. Yumkini zina kasoro, lakini aliyeweka hakuwa na dhamira mbaya. Tukumbuke, hizi kazi zinafanywa na wanadamu. Makosa hutokea. Pale yanapotokea, basi, muhimu ni kukosoana ili marekebisho yafanyike.

Maana, ukiacha kublogu, nami nina kibarua changu kingine. Ndio maana ya kuwepo kwa wengine kwenye timu ya Mjengwablog ili wanisaidie. Na kutokana na kibarua changu, wakati mwingine yaweza kupita siku nzima au hata siku mbili bila mimi kuingia Mjengwablog. Na ninapoingia, nami naweza kuzishangaa picha za CUF Arusha kama wanavyoweza kushangaaa watembeleaji wengine. Na huo ndio ukweli kwa mazingira yangu ya sasa.
Usiku mwema.
Maggid
Iringa
0788 111 765
Nilishaapa kutokutembelea blog yako sasa nafuta kauli kwni ukiacha JF huwa natembelea blog yako lakini kwa tukio Picha za CUF juzi wakati tukio nililifatilia binafsi kwa tajribani wiki nzima hakukuwa na picha za namna hiyo ilinifanya niape kutokutembelea blog yako....
 
Nilishaapa kutokutembelea blog yako sasa nafuta kauli kwni ukiacha JF huwa natembelea blog yako lakini kwa tukio Picha za CUF juzi wakati tukio nililifatilia binafsi kwa tajribani wiki nzima hakukuwa na picha za namna hiyo ilinifanya niape kutokutembelea blog yako....


Crashwise,

Nikushukuru kwa kunielewa. Na twende pamoja. Kwenye makosa njiani tusahihishane.

Maggid,
Iringa.
 
Back
Top Bottom