Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Hii kamata kamata inayoendeshwa na Takukuru hivi sasa za wagombea wa CCM watoa rushwa zina udhati wowote katika kukabiliana na ufisadi uliokithiri ndani ya chama hicho au ni changa tu la macho tunalotupiwa sisi wananchi na taasisi hiyo?
Binafsi, naona ni changa tu la machoni la kumsaidia JK aonekane anaushughulikia uozo huo kabla ya uchaguzi. Sasa hivi tutasikia sifa kwa JK kwamba kawashughulikia watoa rushwa katika chama chake, ingawa naamini kabisa mwisho wa siku, hakuna chochote kitakachotokea kwa maana ya wahusika kupelekwa mahakamani na kuiingia jela.
Aidha pamoja na uchafu wote huu unaofichuliwa, baadaye CCM itajigamba na kusema Ingekuwa siyo Takukuru, mafisadi wangejipenyeza katika uteuzi majigambo ambayo ni upuuzi kama nitakavyoeleza hapa chini:
Mfano mzuri ni wa yule Mama DC wa Kasulu. Pamoja na kukamatwa kwake, bado aliruhusiwa kuendelea kugombea na hatimaye kuwashinda wenziwe, kwa maelezo yaliyotolewa na viongozi wa CCM kuwa hizo zilikuwa ni tuhuma tu, zisizothibitishwa.
Kama mpango ni huu, basi Takukuru wanafanya kazi ya bure tu yaani wanamkamata mgombea kwa tuhuma za kutoarushwa halafu anaachiliwa kuendelea kugombea! Kwa mfano mgombea huyu akipitishwa na vikao vya juu vya CCM na kuwa Mbunge Takukuru hawawezi tena kuleta fyoko ndiyo iatkuwa imepita hiyo! Its all nonsense!
Pili, Hosea naye ana ajenda yake dhidi ya baadhi ya Wabunge waliokuwa mstari wa mbele kutaka angolewe kutokana na husika yake ya kashfa ya Richmond. Inawezekana sasa anaona amepata another axe to grind baada ya ile ya kuwahoji kuhusu double allowance kushindikana.
Tatu, jee harakati hizi za Takukuru dhidi ya watoa rushwa katika teuzi ndani ya CCM, wanaweza kuzirudia katika kampeni za uchaguzi wenyewe? Mimi nadhani hawana ubavu wa kuziendeleza harakati hizi hadi huko kwani wakifanya hivyo kuna Wagombea Ubunge wa CCM wengi tu wanaweza wakapoteza sifa za kuwania nafasi hiyo!