Harakati bila mikatati na mbinu dhaifu za Dr Slaa

Mkuu naona umetoka na single mpya unatafuta hela ya futari kwa nguvu zote

Naona saizi Dr kaja na mbinu mpya kuwa usalama wa taifa wanataka kumuua ili wananchi wamuhurumie amemua kufata mkondo wa Dr Augustino Mrema mwaka 1995 alivyokuwa anaomba ahrumiwe na wananchi kwa mambo ya uongo, yakiwamo ya kutaka kuuwa na vyombo vya dola.
 
Sasa sijui wewe unafuata mkumbo au ndio Chadema-Kata..Chadema hii ni janga la taifa juzi tena tumeona wamedakia suala la mgomo wa madaktari na kutaka kuligeuza liwe mtaji wao wa kisiasa wa kujinadi na kusikika kwa wananchi wakati inajulikana na wote kwamba mgomo ni suala la kikazi linalohusu maslahi na kwa hiyo ufumbuzi wake ni kati ya mwajiriwa na mwajiri wake, kama ni mjadala utakuwa baina ya pande mbili zinazohusika mwajiri na mwajiriwa hakuna upande wa tatu wa aidha bunge ama chama cha siasa, lakini Chadema hasa akina Mnyika na Mbowe na Slaa walitaka mgomo ujadiliwe bungeni.
Wakati Mwigulu alitaka kifo cha kujitakia cha mrusha mawe mkutanoni kijadiliwe bungeni! spika akaona aibu.
 
Najua umetumwa na bwana zako,sina sababu ya kupoteza muda wangu.

Nenda kamwambie Dr Slaa kuwa mbinu yake yakuonewa huruma na wananchi imegonga mwamba...hiyo mbinu alikuja nayo Dr Augustine Mrema mwaka 1995 kuwa usalama wa taifa wanataka kumtoa roho.
 
Masopakyindi, au ndio mtumikie kafiri upate mradi wako? See mwakyembe, mwandosya, dr uli, mwanjisi nk! Sio wanafiki!
We malafyale vipi?
Usi sterio-type makabila hapa nchini, sitaki kuadili mada ili nijzungumzie mimi.
Lakini ni vizuri ukaniambia unafiki wangu ni upi.
Maana Dr Slaa anataka nji hii isitawalike, na wewe unaunga mkono hilo?
Vile vile hao uliowataja wote wanatumikia serikali ya CCM , tena bila matatizo yoyote.
 
Hizi si tuhuma za kwanza za Dr Slaa kwa usalama wa taifa mwaka 2010 alisema usalama wa taifa kushirikiana na tume ya uchaguzi imeingiza makontena ya kura za bandia kutoka Afrika Kusini polisi walipoyakamata hayo makontena wakayafungua mbele ya viongozi wa Chadema na kubainika hayakuwa na kura bandia bali ni Vipodozi! Viongozi wa Chadema wakaonekana waongo na wazushi.

Hivi kumbe!
Na wakachukuliwa hatua gani za kisheria kwa uongo na uzushi huo wenye kuweza kuhatarisha amani ya kisiwa, TZ?
 
Wakati Mwigulu alitaka kifo cha kujitakia cha mrusha mawe mkutanoni kijadiliwe bungeni! spika akaona aibu.

Yaani mnampiga mtu mawe ya kichwa mpaka anakufa halafu unasema kajitakia?
 
Yaani mnampiga mtu mawe ya kichwa mpaka anakufa halafu unasema kajitakia?
Nini kilimtuma kwenda kwenye mkutano usiomhusu na kuanza kurusha mawe? Kipi kilistahili kujadiliwa bungeni katika ya mgomo wa madaktari na huyu mrusha mawe? Au Mwigulu na ugonjwa wake wa akili ni wa mhimu sana bungeni kwa vile anatoka chama cha mabwepande? Huna hoja wewe na uache machozi ya mamba, pokea fedha haramu ya Nape kwa kazi haramu ya kutetea machinjachinja na mafisadi wa mabwepande kioja we!
 
Mkuu wangu hawa Chadema kama unakumbuka walianza kufanya maandamano ya ajabu yenye lengo la kuvamia kituo cha polisi mjini Arusha kilichokuwa na silaha za moto, haijulikani kama azma yao ingefanikiwa sijui ingekuaje.

ngoja 15 labda kisinuke walah naanza na ww kutofoa hilo tumbo lako nyie ndo mnatucheleweshea maendeleo kwa kung'ang'ania madhaifu
 
Chadema haiwezi kuwaambia wananchi kwamba CCM imeshindwa hili na sisi tutafanya hili na lile, ndio maana wamebakia kuwa watu wa kudandia matukio na kuyatolea kauli za ajabu ili waendelee kusikika kwa wananchi kwamba bado wapo kwenye harakati za kisiasa.

Naona umeanza kupayuka kwa maana ufalme unaanza kuwaponyoka. Unauhakika CDM imeshindwa kuwaambia wananchi nini watafanya wakishika dola? Kama wameshindwa waliwezaje kupata idadi kubwa ya wabunge? Hata kura za urais your dingi na UWT walichakachua. Kama JK alishinda urais kwa uhalali mbona hathubutu kutembea mikoani kukagua na kuhamasisha maendeleo? Badala yake amekuwa rais wa mambo ya nchi za nje; sijui Membe anafanya nini?

Pamoja na kuchakachua, ni rais ambaye amechaguliwa na wananchi milioni tano tu. Nchi hii ina watu zaidi ya milioni 45. Embu jiulize ni kweli hao wapiga kura milioni kumi na mbili hawakupiga kura? Ulitaka Dr. Slaa na CDM wakubali huo upuuzi. Rekodi zimekaa sawa CDM walipinga matokeo ya kura za urais. Pia ni sahihi kusema baadaye CDM walimtambua JK kama rais wa TZ ili kuepusha machafuko.

Kama CDM na Dr slaa wana mbinu dhaifu, wewe na CCM yako nini kinawasumbua? Nafikiri ni faida kwenu mkatumia huo udhaifu kujiimarisha. Ubavu wa kwenda kwa wananchi hamna kwa sababu ya udhaifu wenu. Ninyi pigeni kelele CDM inasonga mbele. Dhaifu ni ninyi CCM mlioshindwa kufanya hata chaguzi za mashina na matawi kwa kukosa wagombea.
 
Wanabodi,

Baada ya kuja na mbinu za kisiasa tofauti tofauti hatimaye Dr Slaa, kaja na mbinu mpya ambayo ni harakati bila mikatati na mbinu dhaifu.

Dr Slaa sasa kaanza mkakati wa kutaka aonewe huruma na wananchi kutokana na kile anachokiita kufuatwafuatwa na vyombo vya dola kwa ni ya kutaka kumuua, inashangaza Dr Slaa kubadili mwelekeo wa siasa zake za kutaka nchi isitawalike na kuomba huruma kwa wananchi.

Neno kutaka kuniua ni zito sana ni jinai ndio maana mtu akitishiwa kuuwawa anakimbilia polisi kutoa taarifa na kupatiwa RB. Hakuna aliyeko juu ya sheria ambaye anaweza kumtishia kuua kiongozi kama Dr Slaa halafu akaachwa tu eti yeye ni usalama wa taifa.

Dr Slaa anasema hana imani na taasisi za dola, huyo huyo anayelilia kutaka kwenda Ikulu sasa akifika huko atafanya kazi na taasisi gani, Itakumbukwa mwaka 2010 Dr Slaa aliwangoza viongozi wa chama chake kupinga matokeo ya urais lakini wakikubali matokeo ya ubunge na udiwani. Alikuja na msamiati wa kuchakachuliwa kura zake bila ushaidi.

Dr Slaa kama hana imani na uongozi wa rais Kikwete ilikuaje yeye pamoja na viongozi wenzake kuwa watu wa kwanza kwenda Ikulu kuonana na rais Kikwete katika mchakato wa katiba...hivi Dr Slaa kweli hujui kwamba hii amani na utulivu tunayojivunia Watanzania tangu tupate uhuru wetu inatokana na uimara wa taasisi zetu za dola.

Tafuta inverse ya maandishi yako na hizo dola ni za watanzania na sio za ccm, wewe unadhani hii ni amani ama uwoga? wewe huna cha kuongea hapa nenda ukalale tu uendeleze umasikini wako.
 
Chadema haiwezi kuwaambia wananchi kwamba CCM imeshindwa hili na sisi tutafanya hili na lile, ndio maana wamebakia kuwa watu wa kudandia matukio na kuyatolea kauli za ajabu ili waendelee kusikika kwa wananchi kwamba bado wapo kwenye harakati za kisiasa.

Ni chama kipi kinadandia matukio zaid CCM? Unakiabisha chama chako mwnyw we mzee'
 
Wanabodi,

Neno kutaka kuniua ni zito sana ni jinai ndio maana mtu akitishiwa kuuwawa anakimbilia polisi kutoa taarifa na kupatiwa RB. Hakuna aliyeko juu ya sheria ambaye anaweza kumtishia kuua kiongozi kama Dr Slaa halafu akaachwa tu eti yeye ni usalama wa taifa.

Mkuu hayo ni maneno tu Kwani waliotaka kumuua Ulimboka wao walikua chini ya sheria...? kwahiyo unataka kusema kua haiwezekani kwa watu kutaka kumkili Dr Slaa..?
 
Naona umeanza kupayuka kwa maana ufalme unaanza kuwaponyoka. Unauhakika CDM imeshindwa kuwaambia wananchi nini watafanya wakishika dola? Kama wameshindwa waliwezaje kupata idadi kubwa ya wabunge? Hata kura za urais your dingi na UWT walichakachua. Kama JK alishinda urais kwa uhalali mbona hathubutu kutembea mikoani kukagua na kuhamasisha maendeleo? Badala yake amekuwa rais wa mambo ya nchi za nje; sijui Membe anafanya nini?

Pamoja na kuchakachua, ni rais ambaye amechaguliwa na wananchi milioni tano tu. Nchi hii ina watu zaidi ya milioni 45. Embu jiulize ni kweli hao wapiga kura milioni kumi na mbili hawakupiga kura? Ulitaka Dr. Slaa na CDM wakubali huo upuuzi. Rekodi zimekaa sawa CDM walipinga matokeo ya kura za urais. Pia ni sahihi kusema baadaye CDM walimtambua JK kama rais wa TZ ili kuepusha machafuko.

Kama CDM na Dr slaa wana mbinu dhaifu, wewe na CCM yako nini kinawasumbua? Nafikiri ni faida kwenu mkatumia huo udhaifu kujiimarisha. Ubavu wa kwenda kwa wananchi hamna kwa sababu ya udhaifu wenu. Ninyi pigeni kelele CDM inasonga mbele. Dhaifu ni ninyi CCM mlioshindwa kufanya hata chaguzi za mashina na matawi kwa kukosa wagombea.

Kwenye blue ni mkoa gani Rais ajafika? kwenye red kama Chadema waliyajua hayo yote kwa nini wayakubali matokeo ya Ubunge na Udiwani halafu matokeo ya urais wayakatae?
 
Nenda kamwambie Dr Slaa kuwa mbinu yake yakuonewa huruma na wananchi imegonga mwamba...hiyo mbinu alikuja nayo Dr Augustine Mrema mwaka 1995 kuwa usalama wa taifa wanataka kumtoa roho.

kwahiyo wabunge na viongozi wote wa CCM wanaodai wanataka kuuwawa wanataka huruma ya wananchi??nataka nifahamu mantiki yao kwakuwa Dr. Slaa katoa taarifa unataka mpaka mumtoe roho ndo tuanze kujadili? Tumia hata akili za jirani yako ukishindwa kufikiri kama zako zimestack'
 
Back
Top Bottom