Handbag ya Madam

Aisee umenifurahisha unavyohesabu..Eti Umemkuta mara 15 au mara 13...Kwanini unahesabu kiasi hicho. Unapaswa kumwambia kuwa hupendelei anavyofanya
 
Pole sana, mumeo atakau hajatulia ila wivu unamtafuna, siku zote mwizi hapendi huibiwa, Kuna jirani yangu mmoja, mumewe alikua anampekua hadi kwenye chupi, anamnusa kila kona ya mwili. kumbe yule mwanaume alikua ni mhuni sana huko nje, na katika mawazo yake alidhania kua kile anachokifanya kwa wanawake wengine huko nje ndio hicho hicho anachofanyiwa mkewe na vidume vya nje , aliendeleza ugomvi na wivu usio na maana kwa mkewe, ndugu wamesuluhisha wakachoka, sasa hivi wameshatengana.
 
Habari zenu wapendwa, Jamani naomba mnisaidie nina tatizo dogo tu ambalo kadri siku zinavoenda naona linanikwaza, mume wangu kila nikirudi home kutoka job au popote tu lazima atavizia handbag yangu ataipekua, nimeshamkutia karibia mara 15 sikumuuliza wala sikuchukia, juzi nimemkutia tena na hafanyi hivo mbele yangu anapekua kwa usiri hivo ata kumkutia inakuwa ni bahati tu, hiyo ya juzi nilikuwa nimetoka chuo nikaenda kuweka handbag room, nimerudi sitting room nimekaa kama dakika 5 tu akaja nayeye alikuwa chumbani, akachungulia pale sitting room kaniona niko busy na mtoto akarudi tena chumbani, namie hapohapo nikaingia chumbani nikamkuta tena busy anachambua handbag yangu, jamani ata kama kuna kitu anatafuta kwa mara hizo zote angekuwa ameshakipata, mimi binafsi nachukia na nilishawai kumwambia karibuni tu kama mara ya 13 hivi kuwa kwanini unapenda kufungua handbag yangu, unatafuta nin nikamuuliza vipi mimi nikiwa nakagua mifuko yako ya suruali kila ukirudi utajisikiaje maana wanaume hawabebi handbag, nikamwambia naomba uwe na imani na mimi hili jambo kwakweli linanikwaza, tangia nimemwambia hiyo juzi kaninunia mpaka leo hii eid imepita kimyakimya tu, jamani nisaidieni nifanye nini ili huyu mtu awe na imani namm au anatafuta sababu?
tafuta namna ya kumfanya akuamini. kuna kitu lazima.
 
Mwanaume anayechunguza handbag ya mwanamke ana tatizo kubwa...mwishoe atakagua make-up zako nk..! si kawaida,mweeeh!
 
Habari zenu wapendwa, Jamani naomba mnisaidie nina tatizo dogo tu ambalo kadri siku zinavoenda naona linanikwaza, mume wangu kila nikirudi home kutoka job au popote tu lazima atavizia handbag yangu ataipekua, nimeshamkutia karibia mara 15 sikumuuliza wala sikuchukia, juzi nimemkutia tena na hafanyi hivo mbele yangu anapekua kwa usiri hivo ata kumkutia inakuwa ni bahati tu, hiyo ya juzi nilikuwa nimetoka chuo nikaenda kuweka handbag room, nimerudi sitting room nimekaa kama dakika 5 tu akaja nayeye alikuwa chumbani, akachungulia pale sitting room kaniona niko busy na mtoto akarudi tena chumbani, namie hapohapo nikaingia chumbani nikamkuta tena busy anachambua handbag yangu, jamani ata kama kuna kitu anatafuta kwa mara hizo zote angekuwa ameshakipata, mimi binafsi nachukia na nilishawai kumwambia karibuni tu kama mara ya 13 hivi kuwa kwanini unapenda kufungua handbag yangu, unatafuta nin nikamuuliza vipi mimi nikiwa nakagua mifuko yako ya suruali kila ukirudi utajisikiaje maana wanaume hawabebi handbag, nikamwambia naomba uwe na imani na mimi hili jambo kwakweli linanikwaza, tangia nimemwambia hiyo juzi kaninunia mpaka leo hii eid imepita kimyakimya tu, jamani nisaidieni nifanye nini ili huyu mtu awe na imani namm au anatafuta sababu?
ukute kashauriwa na waganga wa kienyeji.............maana siku hizi kuna upuuzi mwingi wa kuleta utajiri. wee unaona bora kipi, akubali kukutoa wewe sadaka, aambiwe asilale kitandani au awe anakagua pochi yako kila siku?
 
bora uwaeleze wanaume wenzangu wenye tabia kama hizi
inakera sana kupekua pochi za mke wako ni aibu pia
lazima ajue wanawake mnahifadhi vitu vingi kwa pochi na ni kama siri yako mwenyewe
huyu alikuwa anapekua hata nguo za mama yake pia.
rafiki yangu alinisimulia alimshauri ndugu yake kutokupekua pochi ya mke wake kwani shemji yake alimshtaki mbele ya wazazi akadai anamuingilia familia yake baada ya kumshauri sio ustaarabu.
kama walivosema kila unapotoka job uwe unampa kabisa apekue
popote unapomkuta mpe kabisa atajisuta ataacha
Shosti huyo hajiamini kama yuko peke yake.lakini kwakweli nitabia mbaya sana mwanamme kufungua Handbag ya mkewe
malezi gani hayo alolelewa? tena usimcheke bora ajue kama hupendi na usichoke kusema,ama sivyo ukimuachia atataka akupekua mpaka kwenye chupi ajue kama umelala namwengine au laa.
 
Wengine Hawana hata hao Wa kuwakagua.. Wanagugumia kila siku kusaka hata wa kuwasumbua wanaambulia 'used' .. Amakweli Kazi ukiwa nayo Mbaya ..
 
Why do we all marry?
Because romance is not
the only element of life.
We should also know horror,
terror, suspense, irony,
stupidity & tragedy of LIFE
 
wewe mwache tu aendelee na hiyo tabia,maana ni mwanaume asiyejiamini,na mara nyingi wanaume wenye tabia hii ni wale wenye mahusiano mengine ya nje,anahisi na wewe unatoka nje,wewe wala usimuulize,endelea kumwacha apekue simu na pochi zako, usimuulize tena maana unavyomuuliza ndo kwake yeye anadhani kweli una mambo yako!kupekuliwa ni wengi tu tunafanyiwa hivyo na wala hatukereki maana sina cha kuficha!najiamini!vumilia tu mdogo wangu,wenzio tunapekuliwa hadi visivyosemeka na akimaliza unampa bonge la busu na tabasamu pana!anavimbaje bichwa!
 
ni sawa tu na kupekua sms na phonebook ya simu zako,sasa fanya hivi we ukirudi tu toka job mpelekee pochi mwambie sachi dia
 
naima take it easy, mwenzio nikifika tu kama nimemkuta nambwagia cm naenda jikoni! kama hayupo akinikuta baada ya salam nambwagia cm nakaa mbali naye kabisa. manake sitaki apate tabu nishajua ndio ugonjwa wake kunipekua, lkn nina amani sana wala sioni tatizo. ndio walivyo my dia.
 
Pole N. Ni bora akague na kuondoka kuliko akuibie. Kuna mtu mmoja yeye alimsachi mkewe akitafuta vito vyake vya thamani na akaviiba akenda kuuza na kugawia wanawake mahawara ili awaonyeshe kuwa ana hela. Mkewe alivyostuka ikabidi ahamishe vitu afungie sandukuni tena kwa kofuli na akahamishia chumba cha wageni lile sanduku. Kumbe mwanaume yule akatafuta tena vile vitu vya thamani hakuvipata na siku moja alipoona sanduku lina kofulu basi akasubiri usiku wamelala akaamka na akaenda kuvunja lile kofuli la sanduku na kuiba vile vito vya mke wake pamoja na vitu vya thamani. Kesi hii ilitua kwangu na kwa tathmini ya haraka haraka ilionekana alichukua vitu vya zaidi ya milion 60 vya huyu mkewe. Nilisuluhisha but kwa kweli hadi ninapoandika hapa ile ndoa ni gumzo. Hakuna amani kabisa na mke alikuwa ni mama wa familia kwa kujitoa sana kumsaidia mume kwa kuwa mume ni the so called wafanyabiashara wasio na ofisi mujini!!!

Ni jambo la fedheha kumkagua mwenzako hasa kama mwenzi huyo hana tabia za kutia wasiwasi. Na mbaya zaidi kumwibia!!! Yaani hadi leo nikikumbuka kisa hiki huwa natema mate kisikumbe kizazi changu. Mume kumuibia mke ni laana ambayo haina kipimo, mbaya sana.

Hiyo red dah imenigusa mie hutendwa hivyo kila mara mpaka siku hizi vitu vyangu naweka ofisini naacha huko kabisa na hata pesa natembea na ya kutumia siku hiyo hiyo tu
 
Nimekuwa nikifuatilia uzi huu kwa umakini sana, nimefurahishwa na jinsi ya wanandoa walivyofunguka kiufasaha juu ya machungu ya ndoa. Lakini ukiletwa uzi unaosema ndoa ni karaha wataitetea ndoa utafikiri wanazifurahia ndoa zao. Hakuna watu wanafki kama waliyooa/olewa, machoni mwa watu wanajifanya wanapendana, lakini mmh.... Ndoa!!
 
Asante kaka, naona wengi kweli wamenishauri nimpatie kabisa mkoba nitakuwa nafanya hivo

Mmmh! binafsi sikubaliani na ushauri huu, it's like you want to solve a problem by creating another problem, si vizuri kabisa
 
Asipochungulia handbag ya mkewe akachungulie ya mamake ama dada zake? Muache aji-enjoy bwana, mapenzi ni ukichaa. Kama huna cha kuficha, usitie shaka. As long as akimaliza ukaguzi anarudisha kila kitu alivyokuta na anafunga zipu ama bakoli, akhuuu! Muache mtoto wa mwanamke mwenzio akuonee wivu kifaa chake bwana! Wenzio hata wakitoka kazini salamu hawapewi!
 
Hivi unamaanisha? Nikajua unatania aisee! Kwangu hata maid asie muaminifu simuwezi, bora kahaba! Nina colleague anafungiaga hela ofisini ama anatupa tumuwekee. Ila yeye mumewe haibi, anazipangia matumizi! Unakaaje na mwanaume mwizi!!!! Uwiiii! Si unaishi kama stendi!
Hiyo red dah imenigusa mie hutendwa hivyo kila mara mpaka siku hizi vitu vyangu naweka ofisini naacha huko kabisa na hata pesa natembea na ya kutumia siku hiyo hiyo tu
 
Hivi unamaanisha? Nikajua unatania aisee! Kwangu hata maid asie muaminifu simuwezi, bora kahaba! Nina colleague anafungiaga hela ofisini ama anatupa tumuwekee. Ila yeye mumewe haibi, anazipangia matumizi! Unakaaje na mwanaume mwizi!!!! Uwiiii! Si unaishi kama stendi!

My friend I realy mean it my dear take it from me..........ni kero ajabu yaani hata mimi nafungia pesa ofisini maana home hakukaliki pesa
 
Back
Top Bottom