Hamza Mwapachu, Abdulwahid Sykes na Chief Michael Lukumbuzya

Unachoambiwa una udini ni kuona kwamba Waislam wanaonewa japo walipigania uhuru wa Tanganyika pengine kuliko dini zingine. Hutaki kuona sababu za ndani zinazorudisha nyuma harakati za Waislam kupiga hatua ambazo zinatokana na wao wenyewe!
Mkuu waislam wameonewa tokea mkoloni mreno mjerumani na muengereza.
Ndio maana ktk harakati za kupigania uhuru wa tanganyika waislam walijitokeza kwa wingi sana na hawakusita kufanya siasa miskitini na kushirikisha mamufti na mashekhe ktk mbio hizo.
Utengano wetu ni wa kihistoria na kimfumo.
Labda tulifanikiwa kumuondowa mkoloni lakini mfumo bado unatutesa.
Lakini chakufurahisha ni hii changamoto muayo tupa ya kutukebehi hii itatufanya tujiweke sawa na kuondowa mfumo kama tulivyo muondowa muasisi wa mfumo mkoloni.
 
Mzee wangu Mohammed

Naweza kuamini kabisa haya uyasemayo pasipo shaka kabisa.

Sasa hivi nimeanza kufuatilia mihadhara yako mbalimbali kuanzia ile ya TV Stations, Radio Stations na hata Misikitini. Mimi always naangalia arguments za mtu irrespective anazungumzia wapi.

Mzee wangu Mohamed nilikuwa naangalia Clip yako moja ukagusia Habari ya bibi Titi Mohammed alivyofanyiwa, kwa lugha ya sisi vijana tunaita "Figisu-Figisu". Kwa kweli ilinisikitisha sana.

Mwanamama muhimu kama Bibi Titi, Leo hii humsikii kabisa katika historia ya nchi yetu. Yaana kwa ujumla, watu wachache waliibaka historia yetu.

Na kinachoniuma zaidi ni kufundishwa uchafu, uhongo, ujinga na upuuzi katika masomo yangu ya historia tokea niko Primary mpaka Secondary School.
Kuna barabara yake.
 
Je? Familia hii ya mzee wetu na mwanaharakti Abdulwahid sykes ndo hii hii na huyu msanii wa sasa aitwae dully sykes?
Kwezisho,
Baada ya ufafanuzi huu wako sasa nimekuelewa.
Labda nami nijibu swali lako kwa kukuuliza swali.

Naamini umesoma historia ya TANU na uhuru wa
Tanganyika kuna mahali popote ametajwa Abdul?

Unasema Abdul hakutaka kujumuika na Nyerere.

Kwa nini isiwe labda Nyerere hakupenda kujumuika
na Abdul?

Lakini katika kundi hilo hakuwa Abdul peke yake.

Alikuwapo Sheikh Hassan bin Amir vile vile ambae
pia alitoa mchango mkubwa wa kukiongoza chama
vizuri na kumpa ''support'' kubwa Nyerere kati ya
1954 - 1961.

Iweje Nyerere alikuwa kimya kuhusu watu hawa
kama vile hakupata kujuananao?

Sasa hapa msiniachie mimi nifikiri peke yangu sote
tupige kichwa kufikiri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu samahani sana, swali lilikuwa hivi:

Nawe wasema hivi:

Uncle Jei Jei, mie naheshimu sana tafiti za kihistoria nawe pia umeniongezea kitu kwa kusema kiu kubwa ya wazee wetu ilikuwa ni kumuondoa mkoloni. Ila kidogo naomba kutofautiana nawe kwamba, watu waliojumuika na Julius Nyerere baada ya kuikomboa Tanganyika walikuwa na "uchu wa madaraka".
Hili neno uchu wa madaraka linanipa ukakasi na kunikwaza na hata mtafiti wetu Mzee Mohamed Said hapendi kulitumia katika hoja zake. Mzee wetu, Mohamed Said ni gwiji na hazina yetu hilo sote tunaliafiki.
Mimi nilitaka kufahamu kwa nini Abdulwahid Sykes na kizazi chake hawakutaka kujumuika na Julius Nyerere kama ilivyo kwa Mwapachu na familia yake? Je kuna kitu cha ziada au kina Sykes walikuwa na kiu ya kumuondoa mkoloni kisha hawakutaka kulijenga taifa walililolipigania? Yawezekana zipo sababu nyingine za ziada, hebu tujaribu kumdadisi na kumfikirisha Mzee Mohamed Said aendelee na utafiti wake ili aje atujuze.
Hawa walikuwa ni matajiri wa miaka hiyo pamoja na kuujenga mfumo walisaidia Sana Mambo yasikwame kifedha .magari .na sehemu za kulala kwa wageni .pia baada ya kufanikisha walibaki kwenye biashara zao .
 
Inapendeza. Hizi ndiyo historia za kufundisha watoto wetu badala ya kujifunza sana historia za ulaya.

Kuna kisa kimoja, kuna wazungu walikuja hapa kwetu. Na katika majadiliano na vijana wa nyumbani wakashangazwa kuona vijana wenzao wanafahamu sana historia ya bara la Ulaya kuliko historia za bara la Afrika na matukio yake mengi muhimu.
Kwasababu wenzetu wanaweka kumbukumbu. Hata Ulaya historia kubwa tulipiga hamu baada ya Roman Empire kwani ndiyo ilisambaza ustaarabu wa kusoma na kuandika.
 
Kwasababu wenzetu wanaweka kumbukumbu. Hata Ulaya historia kubwa tulipiga hamu baada ya Roman Empire kwani ndiyo ilisambaza ustaarabu wa kusoma na kuandika.
Kweli kabisa, Roman Empire ilisambaza "ustaarabu" (Arabs influence).

Naunga mkono hoja.
 
Ni kweli literacy iliannza kwa Wagiriki, Waarabu walianza number lakini Romans walisambaza elimu kote walikotawala.
Umebadili kauli yako ya mwanzo kuwa Roman Empire walisambaza "ustaarabu"?

Soma kidogo historia ya kwenu hapa useme lugha ipi ya kusoma na kuandika ilifika hapa kwa mababu zako kwanza? Tukipata na kukubaliana hilo halafu tuhamie huko kwa Warumi.

Kuna post leo nimeisoma kuna wageni wa kizungu walikuja wakawashangaa Watanzania, wamewakuta wanaijuwa historia ya Ulaya kuliko ya kwao. Wewe unayakinisha.
 
Historia ya Mohamed Said kuhusu Abdul Sykes na Nyerere ina matobo mengi sana.
Mzee Mohamed Said, ingawa umejibu lakini yaonekana zipo sababu nyingine zaidi. Jibu lako bado halijatosheleza kiu ya watu wanafuatilia harakati za uhuru na kwa nini baadhi ya watu hawamo katika "historia rasmi". Napata shida sana kulimeza jibu lako.
Mzee wangu, haiwezekani muungwana kama Abdulwahid Sykes 'akasusa' na 'kukataa'(?) kujumuika na wenzake ili kuendeleza kile walichokiamini na kukipigania huku akichotumia muda, nguvu na raslimali kubwa.
Je kwa nini Julius Nyerere hakupenda kuwatumia kina Sykes katika kukiendeleza kile walichokiamini na kukipigania (Uhuru wa Tanganyika) ila ikawa vyepesi sana kuwatumia kina Mwapachu?
 
Historia ya Mohamed Said kuhusu Abdul Sykes na Nyerere ina matobo mengi sana.
Yoda,
Usitumie neno, "kususa."
Ikiwa unaona matundu katika historia ya Abdul Sykes kama nilivyoieleza siwezi kukuzuia.

Kwa nini hujiulizi iweje kafutwa katika historia ya TANU?
Ukiwa na jibu tafadhali.
 
Back
Top Bottom