Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Hivi watu hawajachoka bado na mikutano ya waandishi wa habari ambayo kila siku huzaa mikutano mingine ya waandishi wa habari ambayo nayo ilitanguliwa na mikutano ya waandishi wa habari? Inaudhi!
Yaani, utaona jambo limetokea na katika kutokea kwa jambo hilo basi kiongozi anaamua kuita waandishi wa habari na kuwajulisha juu ya jambo hilo (au kutowajulisha kiundani). Akimaliza anaruhusu maswali mawili matatu, anatabasamu, anagonga na meza halafu waandishi hao wanaondoka na kwenda kuandika.
"Waziri ajibu mapigo", "Mheshimwa X,Y aunguruma" n.k n.k
Siku chache baadaye kiongozi mwingine naye anaitisha mkutano na waandishi wa habari na kuanza kujibu mapigo ya yule mwingine. Wakati anafanya hivyo, yule wa kwanza anaandaa mkutano mwingine wa waandishi wa habari.
Lengo la hawa wote ni kujaribu kuonesha kuwa wako juu ya mambo yanayowahusu na kuwa hakuna aliyetayari kupikuliwa na mwingine. Katika kufanya hivyo, utaona viongozi wa kisiasa na watendaji wa serikali na hata taasisi mbalimbali wanatembea na namba za simu za waandishi wao rafiki; waandishi ambao hawachelewi kufika kwenye eneo la "tukio" na ku "cover" story.
Cha kuudhi zaidi ni kuwa katika kufanya hivyo waandishi hao wanahitaji kupatia posho ya kutembea, posho ya kalamu, posho ya kupigwa na jua na wakati mwingine wanatakia kuhakikishiwa kuwa lile gari lililokuwa gereji linatoka kabla ya jumatatu kwa msaada wa mheshimiwa huku mheshimiwa wetu akiahidiwa "stori" nzuri ambayo itaonekana haimpendelei au kumharibia.
Tukiwa bado tunashangaa kinachoendelea tunasikia kuwa kuna mkutano mwingine wa waandishi wa habari ambapo serikali imeamua kutoa onyo na kukemea "vikali" tabia "fulani".
Sasa nimegundua kuwa mikutano ya waandishi wa habari ni siri mojawapo ya kuficha kinachoendelea. Watawala wetu wameshagundua kuwa kwa kadiri ya kwamba wanazungumza na waandishi wa habari na kutoa maelezo marufu (haijali kama wanachokielezea kina umakini) basi wananchi watakuwa wanajua!!
Ndiposa, nimefikia hitimisho kuwa watawala wetu wakiwa wanalala kitanda kimoja na kujifunika mashuka ya ulaghai wamekula njama ya kutupatia taarifa za kutuliza hasira, kiu, kero na kisirani ambao wao wenyewe wametujengea.
Wanajua Watanzania wanaridhika kwa taarifa mbalimbali. Ndipo utaona kwenye magazeti na kwenye matangazo mbalimbali taarifa za serikali na wizara mbalimbali zimejazana huku kila kukicha mkutano mpya wa waandishi wa habari umeandaliwa.
Sasa najiuliza lile swali ambalo nililiuliza kabla ya kutoa ripoti ile ya Meremeta; tunajua ili kiwe nini? Maana kama ni kutaka kujua tu kwa kweli tunajua sana yaani tunajua hata yale ambayo kujua kwake kunatufanya tuwe wahitimu wa kozi ya ujuaji wa ufisadi ambayo darasa lake ni ukumbi wa MAELEZO na wakufunzi wake ni waheshimiwa walioishiwa hoja.
Tumekuwa ni mabingwa wasio na upinzani katika ujuzi wamadudu ya watendaji wetu na kama wataalamu wa siasa za kejeli tumeng'ang'ania vyeti vyetu. Tunajua Rais alikuwa wapi, akibembea nini na harusi ya mtu gani mashuhuri ilivutia vigogo; tunajua nani ana mimba na nani analala nani! Tumefika mahali tunajua hata vile ambavyo kimsingi ni vitu vya chumbani kwa mtu na mwenzake!
Tumekuwa ni vigogo wa ujuzi usio na umuhimu - experts in irrelevant knowledge! Lakini ujuzi huu wote umetufanya tufanye nini nao? Je kujua kwetu yanayotokea Benki Kuu, Ikulu, Wizarani, na ujuzi wa malumbano ya vibosile wa siasa zetu umetusaidia nini zaidi ya kulisha udadisi wetu tu na kutufanya tuwe mabingwa wa kuwaeleza wengine ule ujuzi wetu?
Kwamba tunaweza kusimulia kwa kina ufisadi wa EPA, ufisadi wa Mwananchi Gold, Richmond na mgongano wa maslahi wa kambi za RIchmond kumetufanya tuwe tofauti namna gani zaidi ya tofauti ya kujua zaidi?
Leo hii watu wanaona madudu yanafanywa kwa jina la serikali yao na badala yake wanaamua kuitisha mikutano ya waandishi wa habari; leo hii waliokuwa vigogo wa nchi hii badala ya kusimama na kutaka hatua zichukuliwe na wao wenyewe kuonesha mfano wa mambo hayo wanabakia kuitisha waandishi wa habari na kutoa kauli nzito huku aliyeshutumiwa naye anakutana na wenzaka akiandaa majibu (bila ya shaka itakuwa mbele ya waandishi wa habari!).
Well.. ngoja na mimi niitishe mkutano wa waandishi wa habari nilalamikie jinsi waandishi wa habari wanavyopoteza muda wa kukusanyahabari zisizonaumuhimu na kutujuza vitu ambavyo tayari tunavijua lakini wakivuria kama kaseti iliyokwama au santuri iliyogoma kwenye neno moja!
Tafadhali waandishi wa habari mpo?
Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com
Yaani, utaona jambo limetokea na katika kutokea kwa jambo hilo basi kiongozi anaamua kuita waandishi wa habari na kuwajulisha juu ya jambo hilo (au kutowajulisha kiundani). Akimaliza anaruhusu maswali mawili matatu, anatabasamu, anagonga na meza halafu waandishi hao wanaondoka na kwenda kuandika.
"Waziri ajibu mapigo", "Mheshimwa X,Y aunguruma" n.k n.k
Siku chache baadaye kiongozi mwingine naye anaitisha mkutano na waandishi wa habari na kuanza kujibu mapigo ya yule mwingine. Wakati anafanya hivyo, yule wa kwanza anaandaa mkutano mwingine wa waandishi wa habari.
Lengo la hawa wote ni kujaribu kuonesha kuwa wako juu ya mambo yanayowahusu na kuwa hakuna aliyetayari kupikuliwa na mwingine. Katika kufanya hivyo, utaona viongozi wa kisiasa na watendaji wa serikali na hata taasisi mbalimbali wanatembea na namba za simu za waandishi wao rafiki; waandishi ambao hawachelewi kufika kwenye eneo la "tukio" na ku "cover" story.
Cha kuudhi zaidi ni kuwa katika kufanya hivyo waandishi hao wanahitaji kupatia posho ya kutembea, posho ya kalamu, posho ya kupigwa na jua na wakati mwingine wanatakia kuhakikishiwa kuwa lile gari lililokuwa gereji linatoka kabla ya jumatatu kwa msaada wa mheshimiwa huku mheshimiwa wetu akiahidiwa "stori" nzuri ambayo itaonekana haimpendelei au kumharibia.
Tukiwa bado tunashangaa kinachoendelea tunasikia kuwa kuna mkutano mwingine wa waandishi wa habari ambapo serikali imeamua kutoa onyo na kukemea "vikali" tabia "fulani".
Sasa nimegundua kuwa mikutano ya waandishi wa habari ni siri mojawapo ya kuficha kinachoendelea. Watawala wetu wameshagundua kuwa kwa kadiri ya kwamba wanazungumza na waandishi wa habari na kutoa maelezo marufu (haijali kama wanachokielezea kina umakini) basi wananchi watakuwa wanajua!!
Ndiposa, nimefikia hitimisho kuwa watawala wetu wakiwa wanalala kitanda kimoja na kujifunika mashuka ya ulaghai wamekula njama ya kutupatia taarifa za kutuliza hasira, kiu, kero na kisirani ambao wao wenyewe wametujengea.
Wanajua Watanzania wanaridhika kwa taarifa mbalimbali. Ndipo utaona kwenye magazeti na kwenye matangazo mbalimbali taarifa za serikali na wizara mbalimbali zimejazana huku kila kukicha mkutano mpya wa waandishi wa habari umeandaliwa.
Sasa najiuliza lile swali ambalo nililiuliza kabla ya kutoa ripoti ile ya Meremeta; tunajua ili kiwe nini? Maana kama ni kutaka kujua tu kwa kweli tunajua sana yaani tunajua hata yale ambayo kujua kwake kunatufanya tuwe wahitimu wa kozi ya ujuaji wa ufisadi ambayo darasa lake ni ukumbi wa MAELEZO na wakufunzi wake ni waheshimiwa walioishiwa hoja.
Tumekuwa ni mabingwa wasio na upinzani katika ujuzi wamadudu ya watendaji wetu na kama wataalamu wa siasa za kejeli tumeng'ang'ania vyeti vyetu. Tunajua Rais alikuwa wapi, akibembea nini na harusi ya mtu gani mashuhuri ilivutia vigogo; tunajua nani ana mimba na nani analala nani! Tumefika mahali tunajua hata vile ambavyo kimsingi ni vitu vya chumbani kwa mtu na mwenzake!
Tumekuwa ni vigogo wa ujuzi usio na umuhimu - experts in irrelevant knowledge! Lakini ujuzi huu wote umetufanya tufanye nini nao? Je kujua kwetu yanayotokea Benki Kuu, Ikulu, Wizarani, na ujuzi wa malumbano ya vibosile wa siasa zetu umetusaidia nini zaidi ya kulisha udadisi wetu tu na kutufanya tuwe mabingwa wa kuwaeleza wengine ule ujuzi wetu?
Kwamba tunaweza kusimulia kwa kina ufisadi wa EPA, ufisadi wa Mwananchi Gold, Richmond na mgongano wa maslahi wa kambi za RIchmond kumetufanya tuwe tofauti namna gani zaidi ya tofauti ya kujua zaidi?
Leo hii watu wanaona madudu yanafanywa kwa jina la serikali yao na badala yake wanaamua kuitisha mikutano ya waandishi wa habari; leo hii waliokuwa vigogo wa nchi hii badala ya kusimama na kutaka hatua zichukuliwe na wao wenyewe kuonesha mfano wa mambo hayo wanabakia kuitisha waandishi wa habari na kutoa kauli nzito huku aliyeshutumiwa naye anakutana na wenzaka akiandaa majibu (bila ya shaka itakuwa mbele ya waandishi wa habari!).
Well.. ngoja na mimi niitishe mkutano wa waandishi wa habari nilalamikie jinsi waandishi wa habari wanavyopoteza muda wa kukusanyahabari zisizonaumuhimu na kutujuza vitu ambavyo tayari tunavijua lakini wakivuria kama kaseti iliyokwama au santuri iliyogoma kwenye neno moja!
Tafadhali waandishi wa habari mpo?
Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com