Hamad Rashid ni mtaji maalum

Hapa ndipo utaona tofauti ya kwenda shule na madrasa, mara Hamad Rashid mara Wazanzibar mara Uislam, Hebu kokotaneni wenyewe kwa wenyewe huko kwa waponda urojo
 
Hapa ndipo utaona tofauti ya kwenda shule na madrasa, mara Hamad Rashid mara Wazanzibar mara Uislam, Hebu kokotaneni wenyewe kwa wenyewe huko kwa waponda urojo

Na hizo shule tuzitofautishe kati ya sunday skuli na zile za st st... skuli
 
Hamad Rashid ...arudi tu CUF hakuna mwenye shida naye..kimkakati ..what goes around comes around ..........CUF Walishangilia wakati Hamad anatumika kuiuwa CHADEMA....wanamkakati wa serikali walipoona anashindwa sasa wakaona wamtumie kuimaliza CuF kabisa...

Cuf wanafikiri ccm wanapenda serikali ya mseto ..la hasha....huu ulikuwa mkakati wa ccm kuingia kingi......wale wachezaji wa drafta mnajuwa ....ukitaka kummaliza mpinzani wako ..unamuachia chambo anakula hata double.....akishakula anajikuta mdomoni mwako nawewe unapuga double ...then kingi kabisa ..na kumaliza mchezo.....CUF WAMESHACHEZEWA DRAFT......
Nguvu zikishawaishia .....watakuwa hawana nguvu tena kwenye serikali ya umoja wa kitaifa...na mwishowe watashindwa kuitetea kwa kura na itakufa!!!!!....mkakati wa ccm kumtumia hamad ....ni matunda ya wanamkakati iliowanasa toka cuf mwaka juzi ..CUF ikasema hawana madhara...kina Fatma Maghimbi na mwenzake ..Col.mohamed..[au aliyepata kuwa mkuu wa usalama ndani ya CUF]..Maana naweza kuwa nimekosea jina......na wote ni CUF wanaoishi Kawe[mikocheni ] dar kama Hamad......pamoja na Cuf kuuwa base yao Pemba ...bado wameweza kutumia access yao kuimaliza CUF...

Mkakati wa usalama sasa ni kuiua CUF na upande wa bara mkakati unaendelea kuiuwa Chadema matawini baada ya kuiona mkakati wa kuiuwa kuanzia viongozi wa juu unakuwa mgumu ..hasa kutokana na mfumo wa kimawasiliano na kiinteligensi wa chadema kuwa imara....imeonekana rahisi..zaidi kuanza mkakati wa kuiuwa wilayani..kwa kutumia nguvu ya pesa.........
Chadema wanaonekana ...kuanza kushtuka kwa kufanya counter attack ya kutoa elimu kwa umma...na kuipa milki ya chama kwa umma hali itakayoogofya viongozi wa chini kununuliwa kwa hofu ya kutengwa na wananchi.....hii ndo sababu ccm ...imekuwa ikiambulia wana Chadema waliofukuzwa au ambao hawamo kwenye mfumo wa kiuongozi na kuwadanganya ccm kuwa wao ni viongozi na kuwala pesa.....
 
kuna sehemu nimeandika kuwa tunamuhitaji? Wazanzibari hawana shida na hamad wenu,watajijua wenyewe wapemba na viongozi wao wenye uchu!

Wapi kilaini aliongelea kuhusu Hamad? Hapo inadhihirisha jinsi gani udini unavyowatafuna

Mimi nashangaa sana wa Zanzibar wapo kimya na wamefurahia kufukuzwa kwa Hamad Rashid. Kwanini Bara mnawaingilia.

Je ni nongwa kwa pandikizi lenu kufukuzwa?
Mbona Chadema walimuengua Zitto kabwe katika kinyang'anyiro cha kugombea uenyekiti wa Chadema taifa kwa kutumia mizengwe na watu hawakusema.

Mbona wamefukuza madiwani wao Arusha, lakini hakuna aliyesema?

Kwanini iwe nongwa kwa CUF.

Tunasikia Mpaka maaskofu Akina Kilaini wanalisemea hilo.
Hii inajionyesha kulikuwa na namna kati ya hamad Rashid na maaskofu na chadema pia.

Ok all in all amefukuzwa na hatakiwi na kama nyie mnamtaka mchukueni basi kuliko kuleta zogo hapo.

Kwa CUF hilo sio tena tulufu bali ni Galasa. kama mnamuona tulufu mchukueni.

 
Hv cku hz hakuna sifa ya kuwa mwanachama wa chama cha siasa? Maana naona wa2 wanaingia na kutoka kama siafu kwenye tundu,, hata kama umefukuzwa kwa makosa yaliyodhahili lakini unapokelewa kama mfalme upande wa pili hii ni hatari sana. Enzi ya Mwl ilikuwa vp?. Turudi kama zamani vinginevyo tutakuwa na WANACHANA na cyo WANACHAMA.
 
Uasi wa Hamad Rashid ndani ya CUF umepata uungwaji mkono usio wa kawaida katika vyombo vya habari Tanzania kama kwamba tukio kama hilo halijapata kutokea kwa vyama vyengine au ni mara ya mwanzo katika CUF.

Zaidi ya uungwaji mkono huo, sasa msajili wa vyama bwana Tendwa na Jaji Werema nao wameingilia kati kuonesha kutoridhishwa kwao na uamuzi madhubuti uliochukuliwa na uongozi wa CUF. Haipendezi kwa wanasheria hao kushikilia habari za mahakama ilhali viongozi wa CUF wameshasema hawakupokea amri ya mahakama.

Ukweli ambao wanasiasa na wanaJF hawapendi kuusema ni kuwa Hamad ni mtaji maalum wa kukivuruga CUF. Na kwanini iwe CUF? Ni mkakati wa kuimeza Zanzibar.Kwa upande mwengine CUF si chama cha kiislamu lakini kwa vile kimeasisiwa Zanzibar waislamu ni wengi na hii imekuwa nongwa. Katika mtazamo uliompana huu ni mwendelezo wa kuzima ushiriki wa waislamu katika siasa na hii ni vita ya kimataifa dhidi ya uislamu.
Ami mkuu wangu unaposema CUF sio chama cha Waislaam kisha ukasema haya yaliyotokea ni mwendelezo wa kuzima Ushiriki wa WAISLAAM ktk siasa, hapa una maana gani? ikiwa kweli waislaam wanataka kuingia ktk siasa na wapo CUF ambacho sii chama cha waislaam..Je huoni kama waislaam wanataka kukitumia chama hiki kama jukwaa kufanya siasa hivyo kukifanya chama kiwe cha kiislaam?.
 
Ukiona mtu anakimbilia UDINI ujue kaishiwa HOJA za kisiasa au hakubaliki kwa hoja zake kisiasa,sasa anatafuta kukubalika kidini,sawa bwana kma huna hoja tumekukubali kwa UDINI wako.
 
Si sheikh seif na lipumba wanauchukia uislam!, kwani wewe umekuja lini hapa janvini?!
Mkuu na mimi ningependa unifafanulie ni kwa namna gani kufukuzwa kwa Hamad Rashidi kuna uhusiano na vita dhidi ya uislamu duniani?
 
Hamad Rashid alipotetea posho za wabunge alishingizia ana watoto tele anasomesha.Pesa za kugawa viti na madawati alipewa na nani wakati huko kwao Wawi waliokuwa wapigakura wake wanashindia mashelisheli machanga.Mwache aendelee kutoa madawati tu.
Hawa Tendwa na Werema inaonekana pamoja na shughuli zao nyingi katika serikali ya Kikwete lakini mienendo ya Hamad walikuwa wanaifuatilia kwa karibu sana.Barua ya mahakama walidhani imefika kwa wakati lakini haikuwa hivyo.Loo!.
Allaahu Akbar.
 
Hamad Rashid ni mtetezi wa Bara/Wazanzibara ktk hoja zake na wapo wengi sana kulikom hata idai iliyopo visiwani..Wengine ndugu zetu tumeisha karibishwa ktk undugu na tumezaa watoto na wajukuu... Haaa haaa!.. Pengine nifikirie kaa nyie wana CUF...mathlan leo hii mimi Mzanzibara, Tuache kabisa mbali swala la Utaifa maana muafaka tayari umeshajengwa baina ya Wazanzibar wa CUF na CCM kupigania maslahi ya Zanzibar kama nchi... Je vipi maslahi ya Wazanzibar bara? (Wazanzibara) nani anawatazama hawa watu ikiwa macho yote yamehamia visiwani.

HR ktk utafiti wake kagundua njama kibao na hazisemi tu mbele ya watu wala hapendi kuharibu machache mazuri yalokwisha patikana lakini Maalm Seif haitakii mema CUF kama chama cha kitaifa na chachu hili mwisho wa siku mtalinywa maanake hata kumskiliza tu HR madai yake na pengine awaonyeshe ushahidi -Hamtaki, mnaogopa kwamba atakivuruga chama.. Basi mwiteni shujaa maana kawa kama Lowassa anakinusuru chama kwa sababu akiamua kumwaga manyanga sijui kama watamwacha hai..
 
uzi wako haueleweki vizuri iunapo sema ni mtaji wa nini ? Chama chochote kikimchukua kimekwisha huyu mtu hafai
 
Chadema mpeni Hamad jimbo huko Bara kama mnamhitaji. Siku zote CUF wakivunja kitu basi hawajengi hapo.
 
yaani kila kitu kina mashiko ila dini ndio haina mashiko?, haijadiliki? Kutajwa kwake ni dhambi? Kwanini ikitajwa dini kuna watu wako mstari wa mbele kabisa kuzuia isitajwe! Hivi huyu mdini ni nani? Na hiyo dini yenyewe ni ipi? Mbona habari za ngono, mipasho, madanguro, ufuska ni ruksa kujadili lakini ikija suala la dini linakuwa nyeti! Kuna usiri gani hapa?
Mimi nafikiri kama wewe unacho cha kuchangia kuhusu kufukuzwa kwa Hamad Rashid (muislam) kulikofanywa na Wakristu; na kama unaweza kujadili mchanganyiko wa mambo ya dini na hayo mengine, basi wewe changia tu hamna shida, sisi wengine tumekosa la kusema ndo maana tulikaa kimya.
 
Huyu HR kwanini alifukuzwa?
HR ni mbunge wa wawi, watu waligoma kumpigia kura huyu kwa sababu jimboni hakupeleka maendeleo, Maalim Seif amemtetea sana HR huyu apewe kura jimboni kwake! Ndo akapata, mi naona kama hafai, amekalia kimaslahi yake Zaidi!
 
Jamani ni vizuri mkaelewa. CUF haijamfukuza Ubunge Hamad Rashid. Bali imemfukuza uanachama. Kitakacho muondolea ubunge ni shaeia za Tanzania.

Habari ndio hiyo.
 
Napita tu jamani, ntarudi baaaaaadae kabisa baada ya kupata jibu kama kweli cuf iliasisiwa zanzibar, mana nijuavyo mimi muasisi wa hiki chama ni mapalala ambaye ni wa bara.
 
ndio maana nikasema kuwa mtoa hioja alikuwa na hoja ya kimsingi lakini sasa kaingiza suala zima la udini kitu ambacho mimi nimekiona kuwa hakiendani na mkitadha wenyewe wa hamadi kufukuzwa ndani ya chama. na hata ivo swali la kijiuliza ni kwamba waliomfukuza Huyu RASHIDI ni wana CUF wenyewe na tena ni waislam sasa dhana ya udini imetoka wap[i aktika hii?

labda mh mtoa hoja ajalibu tu kuelewa tu HAMADI ni nani ndani ya nchi yetu ya tanzania ilipaswa aelewe tu kwamba Hamadi amekuwa kama moja wapo ya mhasisi wa chaa hiki cha CUF na vile amewai kuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, na hata ivo ikumbkwe kuwa suala la leo hii seif kuwa makamu wa kwanza wa raisi uapande wa zanzaibar akian hamadi walishiriki vya kutosha. Na kam ani suala la akian werema kuingilia kati hiyo sio hoja kwani akina werema nao ni watanzania na wana hakim ya kuzungumza katika hilo na hat ivo hoja ya akia werema haikuwa ya udini hata kidogo

jamani tisipende kukimblia amsuala ya udini hata pasipo na udini suala la kimsingi hapa tuangalie hoja ya kimsing ya hamadi kufukuzwa kama ni aya kimsingi na sio udini
 
James Magai na Aziza Masoud-MWANACHI
MBUNGE wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed na wenzake 10 sasa wameiomba Mahakama Kuu Dar es Salaam iiamuru Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Wananchi(CUF) wajieleze ni kwa nini wasitiwe hatiani kwa kukiuka amri ya mahakama hiyo.Ukiacha wadhamini hao, jana Hamad Rashid na wenzake, waliomba mahakama iamuru pia wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi wa chama hicho akiwemo Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, Seif Sharrif Hamad wajieleze kwanini wasitiwe hatiani kwa kukiuka amri hiyo.

Pia wanaiomba mahakama hiyo ibatilishe uamuzi wa Baraza Kuu la Uongozi la chama hicho wa kuwavua uanachama hapo Januari 4, 2012, kwa madai kwamba walikiuka katiba ya CUF.

Kabla ya uamuzi huo wa kuwavua uanachama, Januari 3, 2012, Hamad Rashid na wenzake waliwasilisha ombi Mahakama Kuu Dar es Salaama chini ya hati ya dharura wakiomba mkutano wa Baraza Kuu la chama hicho uliokuwa ukitarajiwa kufanyika Zanziba, uzuiwe kuwajadili.
Kupitia kwa mawakili wao, kampuni ya uwakili ya GF Law Chambers Advocates walidai baraza hilo lina nia ya ama kuwasimamisha au kuwavua uanachama na kwamba uamuzi huo ungeathiri haki zao za kikatiba.

Waliendelea kudai kwamba, kuna kesi ya msingi ya madai namba 1 ya mwaka 2012 waliyoifungua mahakamani hapo wakihoji muundo wa Kamati ya Nidhamu na Maadili ya chama hicho na uteuzi wa wajumbe wa kamati hiyo.
Tayari Jaji Augustine Shangwa katika uamuzi wake wa Januari 4, 2012, aliamuru CUF kusitisha uamuzi wa ama kuwasimamisa au kuwavua uanachama walalamikaji hao.

Hamad Rashid jana alirejea amri hiyo ya mahakama kuu chini ya Jaji na kueleza kwamba CUF waliikaidi na badala yake kuendelea na kutekeleza azma yake ya kuwavua uanachama.
 
James Magai na Aziza Masoud-MWANACHI
MBUNGE wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed na wenzake 10 sasa wameiomba Mahakama Kuu Dar es Salaam iiamuru Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Wananchi(CUF) wajieleze ni kwa nini wasitiwe hatiani kwa kukiuka amri ya mahakama hiyo.Ukiacha wadhamini hao, jana Hamad Rashid na wenzake, waliomba mahakama iamuru pia wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi wa chama hicho akiwemo Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, Seif Sharrif Hamad wajieleze kwanini wasitiwe hatiani kwa kukiuka amri hiyo.

Pia wanaiomba mahakama hiyo ibatilishe uamuzi wa Baraza Kuu la Uongozi la chama hicho wa kuwavua uanachama hapo Januari 4, 2012, kwa madai kwamba walikiuka katiba ya CUF.

Kabla ya uamuzi huo wa kuwavua uanachama, Januari 3, 2012, Hamad Rashid na wenzake waliwasilisha ombi Mahakama Kuu Dar es Salaama chini ya hati ya dharura wakiomba mkutano wa Baraza Kuu la chama hicho uliokuwa ukitarajiwa kufanyika Zanziba, uzuiwe kuwajadili.
Kupitia kwa mawakili wao, kampuni ya uwakili ya GF Law Chambers Advocates walidai baraza hilo lina nia ya ama kuwasimamisha au kuwavua uanachama na kwamba uamuzi huo ungeathiri haki zao za kikatiba.

Waliendelea kudai kwamba, kuna kesi ya msingi ya madai namba 1 ya mwaka 2012 waliyoifungua mahakamani hapo wakihoji muundo wa Kamati ya Nidhamu na Maadili ya chama hicho na uteuzi wa wajumbe wa kamati hiyo.
Tayari Jaji Augustine Shangwa katika uamuzi wake wa Januari 4, 2012, aliamuru CUF kusitisha uamuzi wa ama kuwasimamisa au kuwavua uanachama walalamikaji hao.

Hamad Rashid jana alirejea amri hiyo ya mahakama kuu chini ya Jaji na kueleza kwamba CUF waliikaidi na badala yake kuendelea na kutekeleza azma yake ya kuwavua uanachama.

Hamad Rashid.

nafikiri CUF wameshaweka wazi kabisaaaaa msimamo wao. Kuwa wao wamekufukuza na mahakama kama inakuhitaji basi uwe mbunge wa mahakama au mbunge wa Spika lakini sio mbunge wa wawi kupitia CUF.

Sasa unajisumbua nini.

Ok , tusubiri hilo shauri ulilopeleka mahakamani kama litakuwa na mashiko.

Pole sana kwa kulala na kukesha maelezo Dar.

 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom