Chigwiyemisi
JF-Expert Member
- Jun 22, 2011
- 531
- 225
Wadau jana nilimsikiliza HR akiongea na waandishi wa habari mara baada ya shauri lake kusikilizwa na mahakama! Katika maelezo yake alidai kuwa ana imani kubwa na mahakama na ana imani kuwa itatenda haki. Kimsingi ukimuangalia HR ni kwamba anaung'ang'ania uanachama wa CUF kwa udi na uvumba na ndio kisa cha kwenda mahakamani!
Lakini kinachonishangaza ni kwamba katika maelezo yake aliendelea kusema kwamba CUF IMEPASUKA na wananchi wasubiri tumaini jipya. Akatoa mfano akimnukuu Mwalimu Nyerere kuwa alipata kusema kuwa kioo kikiingia vumbi kifute na kikipasuka kiondoe kwa hiyo alimaanisha kwamba CUF imepasuka na inapaswa kuondolewa. Hapa mimi nilifikiri anazungumzia wazo lake la kuanzisha Chama.
Maswali yangu ni haya;
Lakini kinachonishangaza ni kwamba katika maelezo yake aliendelea kusema kwamba CUF IMEPASUKA na wananchi wasubiri tumaini jipya. Akatoa mfano akimnukuu Mwalimu Nyerere kuwa alipata kusema kuwa kioo kikiingia vumbi kifute na kikipasuka kiondoe kwa hiyo alimaanisha kwamba CUF imepasuka na inapaswa kuondolewa. Hapa mimi nilifikiri anazungumzia wazo lake la kuanzisha Chama.
Maswali yangu ni haya;
- Kwa nini kama CUF imepasuka anaing'ang'ania hadi mahakamani?
- Ikumbukwe kuwa Mtatiro anasema hata kama mahakama itamrudisha maamuzi yao POLITICALLY yako palepale, je HR anaweza kufanya kazi bila ushirikiano na wenzakle endapo atarudishwa?
- Kwa nini kama yeye ni jasiri na ana support ya watu kama anavyodai asiachane na hiyo kesi akaendelea na taratibu nyingine za kufungua chama chake na kuleta tumaini jipya analosema wananchi wanahitaji?