HAMAD RASHID katika Njama za Kumng'oa Maalim Seif?

tulijua haya madubwasha yake yatamfikisha mahali pabaya.mnafiki wa kambi ya upinzani aliiwangia,sasa yamemshinda.
 
CUF yafanya mabadiliko ya uongozi Thursday, 26 May 2011 22:25 0diggsdigg

Elizabeth Ernest
CHAMA cha Wananchi (CUF), kimemteua Julius Mtatiro, kuwa Naibu Katibu Mkuu Tanzania Bara na Ismail Jusa Ladhu kushika wadhifa huo huko Zanzibar.

Akitangaza uteuzi huo jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahimu Lipumba, alisema tayari Baraza Kuu la CUF, limewapitisha.Alisema baraza hilo pia limepokea na kuridhia mabadiliko yaliyofanywa na wabunge wa CUF, kwa kumchagua Mohamed Habib Mnyaa, kuwa kiongozi wa kambi ya CUF bungeni na Magdalena Sakaya, kuwa Katibu wa kambi hiyo.

Mbunge mwingine ni Hemed Salim ambaye alichaguliwa kuwa Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya CUF.Katika hatua nyingine, CUF imemtaka Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kujiuzulu kwa madai kuwa ameshindwa kutumia vyanzo vya umeme vilivyopo, kukabiliana na tatizo la nishati hiyo.

Chama hicho kimesema Tanzania ina uwezo wa kufua umeme wa megawati 5,000 ikilinganishwa na megawati 791 za sasa zinazoingizwa katika gridi ya taifa.Kwa mujibu wa Profesa Lipumba vyanzo vya maji vinachangia kwa megawati 562 ya umeme huo.

Alisema makaa ya mawe yaliyogunduliwa yanaweza kuzalisha umeme wa megawati 1000 kwa zaidi ya miaka 50 ijayo wakati gesi iliyogunduliwa Mnazi Bay, mkoani Mtwara, Mkuranga na Songosongo, Kilwa inaweza kuzalisha umeme zaidi wa megawati 1000 kwa zaidi ya miaka 50 ijayo.

"Lakini pia madini ya uraniamu yaliyogunduliwa Namtumbo na Manyoni, yana uwezo wa kuzalisha malaki ya megawati za umeme kwa muda mrefu. Gharama za kuzalisha umeme wa jua na upepo zimepungua na zinaendelea kushuka,"alisema Profesa Lipumba. "Miaka 50 baada ya uhuru hatuna sababu ya kutokuwa na umeme wa uhakika, lakini Serikali ya CCM na Waziri Ngeleja,

Source: Mwananchi 27/5/2011
hapo kwenye red naomba msaada hivi kila chama kina kambi yake? Ufahamu wangu bungeni kuna kambi mbili ya Serikali na ya Upinzani ( Ya Pinda na nyingine ya Mbowe) sasa hii ya Mnyaa ni kitu gani
 
Rais+Dk+Ali+Mohammed+Shein+akisalimiana+na++Mbunge+Hamad++Rashid.JPG


MZEE WA KAMBI NDOGO YA UPINZANI.... CUF KAZI KWENU
 
na Asha Bani

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimefanya mabadiliko ya uongozi kwa kuwaondoa baadhi ya wakongwe kwenye nafasi zao na kuwaweka wanasiasa wapya wakiwemo vijana.

Mabadiliko hayo yamefikiwa baada ya Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la chama hicho kukaa vikao vyake kwa siku mbili katika hoteli ya Triz iliyoko Mbezi jijini Dar es Saalam.

Katika mabadiliko hayo wabunge wa chama hicho wamemuengua aliyekuwa mkuu wa kambi ndogo isiyo rasmi bungeni, Hamad Rashid Mohamed (Mbunge wa Wawi), na kumchagua Mohamed Habib Mnyaa (Mbunge wa Mkanyageni) kushikilia wadhifa huo.

Katika mabadiliko hayo, Magdalena Sakaya, mbunge wa viti maalum Tabora amechaguliwa kuwa katibu wa kambi hiyo bungeni huku Hemed Salim mbunge wa Chambani akichaguliwa kuwa mnadhimu mkuu wa kambi hiyo.

Mabadiliko hayo pia yamemuondoa kwenye nafasi yake aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu upande wa Zanzibar, Juma Duni Haji, na nafasi yake imechukuliwa Ismail Jusa Ladhu ambaye ni mwakilishi wa Mji Mkongwe. Kwa mabadiliko hayo, Duni Haji sasa anabakia na wadhifa wa Waziri wa Afya katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ).

Julius Mtatiro ameidhinishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho upande wa bara.

Akisoma maazimio hayo Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba, alisema yamefanyika ili kuleta ufanisi zaidi kwa chama hicho katika kuwatumikia Watanzania kwa kugawana majukumu kutokana na viongozi wa awali kupangiwa majukumu mengine.

Hata hivyo, awali ilidaiwa kuwa Hamad Rashid aliyekuwa mkuu wa kambi ndogo isiyo rasmi angeondolewa katika kambi hiyo kwa sababu ya kutokuwa na ushirikiano na wabunge wenzake bungeni.

Mbali na mabadiliko hayo, baraza kuu hilo la CUF lilimtaka Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha, kujiuzulu kwa kuwa ni mzigo kwa serikali.

Akizungumzia ukiukwaji wa haki za binadamu nchini alisema baraza kuu limelaani vitendo vya ukiukwaji na uvunjwaji wa haki hizo kutokana na mauaji ya raia yanayoendelea kuripotiwa mara kwa mara yanayofanywa na polisi.

Alisema mauaji yaliyotokea katika mgodi wa North Mara unaomilikiwa na kampuni ya Barrick sasa yamekuwa ni jambo la kawaida ambalo watendaji wanaweza kufanya bila ya kuchukuliwa hatua yoyote.
Kutokana na hilo baraza kuu limeazimia uchunguzi wa kina ufanyike huku wakimtaka Waziri wa Mambo ya Ndani awajibike kwa kujiuzulu kutokana na mauaji hayo.
Akizungumzia hali ya maisha ya Wazanzibari wanaoongozwa na serikali ya umoja wa kitaifa inayoundwa na vyama vya CUF na CCM, Profesa Lipumba alikiri kuwa bado si nzuri.

Alisema hali hiyo inatokana na utekelezaji wa kazi ya serikali za umoja huo kuanza wakati bajeti ya Zanzibar ikiwa tayari imekwishapitishwa.

Alisema changamoto nyingine wanazokabiliwa nazo ndani ya serikali ni mtikisiko wa uchumi wa dunia na kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbali.

Hata hivyo, aliwataka wale wote waliopata nafasi ya kuwatumikia wananchi kupitia serikali ya umoja wa kitaifa kufanya kazi kwa ufanisi huku wakipambana na changamoto zote zilizopo mbele yao kwa lengo la kuwaletea maisha yenye neema Wanzanzibari na Watanzania wote kwa ujumla.

Baraza Kuu limesikitishwa na matukio ya milipuko ya mabomu inayotokea kwa wakazi wa Gongo la Mboto na kusababisha athari kubwa kwa wananchi ikiwa ni pamoja na uharibifu wa mali zao na kuathirika kiuchumi.
 
Nice CUF wameonyesha kuwa sio wadini kwa Mabadiliko hayo... Tungojee tuone Ushiriki wao utakuwaje

Inachekesha CCM wanaukimbilia Udini; CUF inataka kujisafisha...
 
Baada ya CCM-A kujivua gamba nao CCM-B wamejivua... move inaendelea NCCR, TLP, lini?
 
Hata mimi najua kuna wafuasi watiifu kwa CUF na wanakitambua chama chao kama cha upinzani na si vinginevyo.

ila bado...

lazima iundwe CUF mpya. wawaache mamluki waende. wamepata walichokuwa wanataka...madaraka.
 
CUF na CCM si kitu kimoja...kinachofanywa na ccm lazima kifanywe pia na cuf
 
Gamba ni lipumba na seif, ambao wamekifanya chama kuwa cha watu 2!, cuf ni chama kisicho na dira wala mwelekeo!,
 
Nice CUF wameonyesha kuwa sio wadini kwa Mabadiliko hayo... Tungojee tuone Ushiriki wao utakuwaje

Inachekesha CCM wanaukimbilia Udini; CUF inataka kujisafisha...

Mmmh, majina meengi ni yaliyotajwa ni ya kimujahidina. Julius Mtatiro ana sigda kubwa huyo inafanana na tochi itakayo msaidia kuonea ahera!
 
Sasa inadhihirisha Hamad ndio aliyekuwa hapendi muungano wa Upinzani Bungeni... Ndio Maana wameumuondoa

Sasa atakula wapi? alikuwa anapenda kutembelea nje ya nchi na siasa zake kali, mara nyingi Kikwete akisafiri ilimbidi amchukue waende pamoja kumtuliza... WOW CUF!!!
 
Haya ni mawazo yako, ya kiutafiti, au ya Hamad mwenyewe? Nafurahi sana kwa aina ya siasa za leo za tz,kwetu sie wapenda mageuzi zinamafaa.
 
Hivi Mlima Kilimanjaro sorry Profesa Lipumba bado ni mwenyekiti wa CUF? Kama ndio, kazi yake hasa ni nini ndani ya chama?
 
Tayari mgogoro mkubwa wa kimaslahi binafsi umeikumba Cuf baada ya hamad Rashid kumpinga waziwazi maalim seif na sasa anamkakati wa kumngoa ktk nafasi ya katibu mkuu wa cuf na pia kutaka kuiteka kambi ya maalim seif huko Pemba. Mkakati huo umekuja baada ya hamad rashid na kundi lake kutumia muda mwingi kutembelea kisiwa cha Pemba ili kumkosanisha maalim seif na wakazi wa Pemba ambao idadi yake kubwa ni Cuf.
Hamad rashid amechukua hatua hiyo baada ya kugonga mwamba kupata nafasi ktk bunge kama mmoja ya viongozi wa kambi ya Upinzani bungeni baada ya CDM kumwekea vikwazo. pia hatua ya rashid inakuja baada ya kuongolewa nafasi ya mkuu wa kambi isiyorasmi bungeni ambapo habib mnyaa ameichukua.
habari amabazo zimeenea eti Mpango huo wa hamad rashid kutaka kutafautiana na Maalim unatoka na mpango hamad rasdhid kutaka kuahmia chadema. rashid licha ya kuonekana waziwazi kutomshinda maalim seif . mapngo huo unafanywa ili hamad aone ameonewa na apate sababu ya kuhamia cdm. kwani cdm ilihusishwa na hamad rashid kutaka kuwa mgombea mwenza wa dk slaa 2010

where's ma gun @?

shyt!!!
 
Back
Top Bottom