Hamad Rashid amesahau 1995 - 2000?

Nadhani mjadala unakwenda pasipo, haitoshi kumtukana Hamad Rashidi, la kujadili ni kwamba CUF watashirikiana CCM na pengine hata NCCR ingawaje TLP mwenyekiti ameshatoa msimamo wa kukiunga mkono CHADEMA na kubadili kanuni za bunge zitakazo weza kuwa- disadvantage kwa CHADEMA kama kambi rasmi ya upinzani. Cha kujadili ni kwa vipi hili linaweza kuzuilika? Viongozi wa Chadema lazima wafikiri kabla vema strategies zao kabla ya mafisadi wa CCM pamoja na CUF. CCM watalipendana hili sana. Je si vema Chadema wakafanya mazungumzo na TLP na NCCR angalau kuzuia CUF wakishirikiana na CCM kuchakachua kifungu chenye kuipa uhalali Chadema kama kambi rasmi ya upinzani? JF lazima tutambue sasa multiparty politics si jazba bali strategies na sharpness. Isije ikawa kama uchaguzi wa spika na naibu wake...Let us try to strategize here!
 
CUF ndo wanazidi kuendesha fitina zidi ya CHADEMA kwa kuwarubuni wabunge wa NCCR, TLP, UDP kuunda kambi ndogo isiyo rasmi sasa iwe ni payback time, mtenda hutendwa, chadema waunde baraza la mawaziri kivuli linalojumuisha vyama vyote vya upinzani bungeni with exception ya CUF, CUF wapigwe buti kali, kwani wao wanataka kujitia wana haki sana kuliko chama chochote
 
CUF na HR ni machangudoa wa kisiasa kabisa, mshika mbili moja humponyoka, lazima wachague moja chama tawala au upinzani! Nadhani wanakosa ile nafasi muhimu ya kuzungumza kutoka kambi ya upinzani, sasa walitaka kujificha kwa mwamvuli wa NCCR, TLP na UDP ili watimize azma yao, wamewapoteza wenzao sasa wana mangamanga hovyo kama wendawazimu

Hawa wanafaa kupigwa chini tu bila huruma, lakini chadema wawakubalie, cheyo, kafulila, mkosamali, mrema na yule mama wa NCCR, CUF wapigwe chini
Naungana na wewe ili kumfanya HR na CUF wachanganyikiwe zaidi CDM ichague wabunge wawili au watatu kutoka aidha NCCR au UDP ama TLP iwape wizara na kuwapiga chini Hamad na CUF yake ili next time ajifunze kushirikiana toka kwenye chaguzi ndogo ndogo.
 
Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni ndiye waziri mkuu kivuli, hivyo anapata
  1. Ofisi pale bungeni Dodoma yenye wafanyakazi 4 na ofisi ndogo Dar es Salaam yenye wafanyakazi 2
  2. Nyumba ya serikali pale Dodoma yenye watumishi wawili na ulinzi 24/7
  3. Gari la serikali lenye hadhi, na dereva/bodyguard, mafuta kumwezesha kuzunguka nchi nzima.
  4. Posho kama ya Waziri Mkuu.
  5. Ndiye mtu wa kwanza kuulizwa swali kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo.
  6. Kipaumbele kwenye safari za nje
  7. etc etc
Sasa yote haya uyakose!, hata ningekuwa mimi, ningeomba kanuni zibadilishwe na kupata japo nusu ya marupurupu haya!

Wanasiasa wa Tanzania njaa na michoso. Ni kukoroga wananchi bila sababu za msingi wakiutukuza umaarufu na kupata misifa
 
Bunge la 2000 hadi 2005 CUF waliwashirikisha Chadema kwenye kambi ya Upinzani! Sasa hapa nani mrafi wa madaraka kama sio Mbowe na Chadema? Maskini akipata makalio hulia Mbwata!


acha ujuha wewe...uliza sababu iliyowalazimisha wawashirikishe! usifikiri walipenda
 
WILDCARD: Hii point yako ndiyo ya msingi kuitafakari.. hayo mahela kila mtu angeyatamani, labda Nyerere (si hawa nyerere wa sku iz lkn).

Kama inaitwa kambi ya upinzani, na wakati huohuo hawa jamaa si wapinzani huko visiwani (katibu wake kitaifa ni rais mwenza ktk serkali ya CCM), wanawezaje kuitwa wapinzani wa washirika wao huku bara? JAMANI, HAMUONI KAMA HAYA YANACHOCHEWA NA CCM WENYEWE ili kuzima moto wa upinzani mkali tunaoutarajia bungeni? So kunyimwa kuanzisha kambi nyingine (nafikiri), ni kuitilia chachu CUF ilazmishe kuingia kambi ya CDM, which literally means kuiingiza CCM ktk kambi ya upinzani? Nafikiria tuuuuu......
 
Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni ndiye waziri mkuu kivuli, hivyo anapata

  1. Ofisi pale bungeni Dodoma yenye wafanyakazi 4 na ofisi ndogo Dar es Salaam yenye wafanyakazi 2
  2. Nyumba ya serikali pale Dodoma yenye watumishi wawili na ulinzi 24/7
  3. Gari la serikali lenye hadhi, na dereva/bodyguard, mafuta kumwezesha kuzunguka nchi nzima.
  4. Posho kama ya Waziri Mkuu.
  5. Ndiye mtu wa kwanza kuulizwa swali kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo.
  6. Kipaumbele kwenye safari za nje
  7. etc etc
Sasa yote haya uyakose!, hata ningekuwa mimi, ningeomba kanuni zibadilishwe na kupata japo nusu ya marupurupu haya!
Ama kuumbe mie nilikuwa siyajui mwaego ndio maana Hamad analia namuna hiyo si amuombe Maalimu amwingize kwenye serikali ya umoja kule kwetu Unguja
 
Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni ndiye waziri mkuu kivuli, hivyo anapata
  1. Ofisi pale bungeni Dodoma yenye wafanyakazi 4 na ofisi ndogo Dar es Salaam yenye wafanyakazi 2
  2. Nyumba ya serikali pale Dodoma yenye watumishi wawili na ulinzi 24/7
  3. Gari la serikali lenye hadhi, na dereva/bodyguard, mafuta kumwezesha kuzunguka nchi nzima.
  4. Posho kama ya Waziri Mkuu.
  5. Ndiye mtu wa kwanza kuulizwa swali kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo.
  6. Kipaumbele kwenye safari za nje
  7. etc etc
Sasa yote haya uyakose!, hata ningekuwa mimi, ningeomba kanuni zibadilishwe na kupata japo nusu ya marupurupu haya!
jaman hamad komaa ili iyo kambi maruhani iwemo utaishije bila hayo marupurupu? HR + kafulila nendeni bungeni mkatete CCM mujikomoe 2015.
 
Hamadi is such a gold digger! Hana jipya, ni mroho wa madaraka tu! Anang'ang'ania kujoin na cdm baada ya kuambiwa kambi mbili za upinzani haziwezekani? Kwani kuna nini kubwa analo ng'ang'ania? Ana lake jambo namuomba Mbowe amtose maana huo uking'ang'anizi wake una jambo ndani yake.

M. M.
 
Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni ndiye waziri mkuu kivuli, hivyo anapata

  1. Ofisi pale bungeni Dodoma yenye wafanyakazi 4 na ofisi ndogo Dar es Salaam yenye wafanyakazi 2
  2. Nyumba ya serikali pale Dodoma yenye watumishi wawili na ulinzi 24/7
  3. Gari la serikali lenye hadhi, na dereva/bodyguard, mafuta kumwezesha kuzunguka nchi nzima.
  4. Posho kama ya Waziri Mkuu.
  5. Ndiye mtu wa kwanza kuulizwa swali kwenye kipindi cha maswali ya papo kwa papo.
  6. Kipaumbele kwenye safari za nje
  7. etc etc
Sasa yote haya uyakose!, hata ningekuwa mimi, ningeomba kanuni zibadilishwe na kupata japo nusu ya marupurupu haya!

Pasco, ungejitofautisha na wengine for the way I know you, ww ni great thinker wa kweli, nilidhani unakwenda kwenye point, kuwa advantage zote hizo ndiyo zinazowafanya chadema si kuwatenga wenzao tu bali hata kutengana wao kwa wao, maana si Hamad Rashid tu peke yake anayetaka faida hizo hata aliyezipata alishaweka mkakati wa kuzipata mapema na hakutaka mwengine yeyote asogee. Mbowe alishataka kumtoa kafara Zitto Kabwe mara ngapi kwasababu ya cheo hicho hicho?
Tulichotaka hapa ni spirt of togetherness ya upinzani...hakuna asiyejuwa kuwa hata wapinzani wote washikane bado CCM inanguvu bungeni sikwambii wajigawanye wao kwa wao.
Chadema wasiungane na CUF basi hata NCCR-Mageuzi?
Kwa taarifa yenu Hamad Rashid hana tamaa hiyo ya cheo, shida yake umoja na ushirikiano wa kambi ya upinzani bungeni kwa manufaa ya wananchi wenyewe.
Mimi nawakumbusha wakereketwa wa chedema humu wasione kufanya hivyo ndiyo wanawasaidia wananchi, upinzani ulivyo sasa hawana hoja yoyote itakayopata nguvu bungeni bila wao kuwa imara na kuwashawishi wenzao wa CCM wenye msimamo wa wastani kuwasaidia. Atakayekosa huko mbeleni si Hamad Rashid ni wananchi wenyewe.
 
Ni kweli kafu ni wapinzani na wanaweza kuwa kambi moja na cdm hamjaona hata wakati wanachagua spika na naibu wake walimpigia nani kura? Hata kama kura ni siri lakini matokeo sio siri. Mix with yours:clap2:
 
Hivi uhai wa CUF kisiasa ni nini hasa? Maana hicho, NCCR-Mageuzi na TLP ni vyama ambavyo siasa zao kwa kweli zimenishinda kuelewa. Kiitikadi na kimatendo sijui wanaamini nini, wanataka nini, wana malengo gani, wanafanya nini nk

Naomba msaada kuwaelewa vizuri hawa jamaa.
 
Pasco, ungejitofautisha na wengine for the way I know you, ww ni great thinker wa kweli, nilidhani unakwenda kwenye point, kuwa advantage zote hizo ndiyo zinazowafanya chadema si kuwatenga wenzao tu bali hata kutengana wao kwa wao, maana si Hamad Rashid tu peke yake anayetaka faida hizo hata aliyezipata alishaweka mkakati wa kuzipata mapema na hakutaka mwengine yeyote asogee. Mbowe alishataka kumtoa kafara Zitto Kabwe mara ngapi kwasababu ya cheo hicho hicho?
Tulichotaka hapa ni spirt of togetherness ya upinzani...hakuna asiyejuwa kuwa hata wapinzani wote washikane bado CCM inanguvu bungeni sikwambii wajigawanye wao kwa wao.
Chadema wasiungane na CUF basi hata NCCR-Mageuzi?
Kwa taarifa yenu Hamad Rashid hana tamaa hiyo ya cheo, shida yake umoja na ushirikiano wa kambi ya upinzani bungeni kwa manufaa ya wananchi wenyewe.
Mimi nawakumbusha wakereketwa wa chedema humu wasione kufanya hivyo ndiyo wanawasaidia wananchi, upinzani ulivyo sasa hawana hoja yoyote itakayopata nguvu bungeni bila wao kuwa imara na kuwashawishi wenzao wa CCM wenye msimamo wa wastani kuwasaidia. Atakayekosa huko mbeleni si Hamad Rashid ni wananchi wenyewe.

Hivi JF kuna ugonjwa gani siku hizi, haya mambo ya HR na Mbowe hayana hata miezi mitatu tayari historia inapindishwa makusudi kabisa!!!!!!
 
Yaani huyu jamaa inaelekea CDM wakipata Urais, hakawii kusema- "kwa kuwa ni chama cha upinzani kama wao, basi awepo Rais Kivuli toka chama pinzani..!!" Roho ya "kwa nini" haiwaishi hawa jamaa...!!!

Wewe unafahamu kabisa kuwa kanuni zinasema nini kuhusu kambi ya upinzani; Chadema hawakuwahi kuomba kambi kivuli wakati wewe unakula kuku kama kiongozi wa upinzani leo wamepata wao unang'ang'ania sahani..!! Hana tofauti na jamaa wa Ivory Coast..!! Huyu Hamad pamoja na viongozi wenzie na walee ndugu zangu wa NCCR, siwatofautishi na viongozi wanaopenda madaraka; wako tayari hata kuchakachua kura ili wayapate. Wako tayari kusababisha vurugu nchini ili waupate uongozi. Watu wa namna hii hawafai hata kidogo kuwa viongozi sio wa serikali kuu tu, bali hata ya kitongoji..!!
 
CUF imo ndani ya serikali ya CCM kule Zanzibar na Maalim Seif ni Makamu wa Kwanza wa Rais. Hadhi ya CUF kuendelea kuitwa wapinzani upande mmoja wa Muungano ni kichekesho kama sio dhihaka kwa siasa za ushindani!

Hamad Rashid na CUF yake hawawezi kuilazimisha wala kuipangia Chadema ni chama/vyama gani ivialike kwenye kambi yake rasmi ya upinzani (Serikali kivuli). Hii ni ikiwa itapenda kwani imetimiza takwa la 12.5% la kuunda kambi rasmi ya upinzani peke yake.

Haiingii akilini kuwa CUF ni sehemu ya Serikali kule Zenji, na Tanganyika inadai ni chama cha upinzani.

Chadema iunde Serikali kivuli peke yake, ndiyo itakuwa Serikali makini. Isijiunge na vyama hivyo vingine ambavyo hata kwenye Bunge vilichagua Spika, Naibu Spika na wagombea wa CCM kuwakilisha hata huko kwenye Bunge la SADC, vikawaacha Chadema.

CUF si iliiacha NCCR-Mageuzi Bunge la 1995-2000?

What goes around, comes around...
 
Mnao sapoti Cuf wajumuishwe kambi ya upinzani,are u greater thinkers?Acheni ushabiki wa kitoto!Kuna watu wameogelea sijui togherness mara chenk n balance na mambo mengine mengi tu!Nianze na Chadema kwanini wasiungane hasa na Cuf,baada ya uchaguzi Chadema hawakukubaliana na jinsi uchaguzi ulivyoendeshwa kuanzia ngazi ya udiwani,ubunge na uraisi lakn Cuf walidhia matokeo hayo hapa bara na visiwani,pili Cuf wameunda serikali ya umoja w kitaifa na hapa nawajibu akina togetherness na chenk n balance kuwa kutokana na kuzaliwa SUK kimezaliwa kingine katika utendaji nacho ni Conflict of Interest ambacho kinaua togetherness na chenk n balance!Kwa pointi ya kwanza kimsimamo wapo tofauti!NCCR-MAGEUZI mwenyekiti wao anawatuhumu Chadema wamemchezea rafu ktk jimbo la kawe na amefungua kesi dhidi ya Mh.Mdee ,leo wawe kambi moja!Unafiki ulipitiliza!T.L.P waliweka rekodi ya dunia,wanamgombea wa uraisi lakini mwenyekiti wao anampigia kampeni mgombea uraisi wa Ccm!Leo waungane!Shame on you!UDP ya Mh.Cheyo mara ngapi wamemfukuza kambi ya upinzani kwa kujipendekeza Ccm?Leo mnapiga kelele ajumuishwe!Waache Chadema waunde kambi yao yenye Lengo na Dira moja,ili wakishindwa kazi hiyo hukumu yao 2015.Maana watu humu wameanza kujifanya watabiri.CDM msimamo huo huo,kuna msemo wa lugha ya kikoloni If u want.........join them!So CDM take care!
 
Back
Top Bottom