Hamad Rashid aing'arisha Tanzania kimataifa.....

Mwana Mpotevu

Platinum Member
Sep 7, 2011
3,295
2,500



Mbunge wa Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Mkutano wa Chama cha Mabunge Duniani Mhe. Hamad Rashid Mohamed ameteuliwa na kamati tendaji ya chama cha Mabunge duniani (IPU) kuwa mjumbe wa kamati ndogo ya ukaguzi wa ndani kwa mahesabu ya mwaka 2013 ya chama hicho.

Uteuzi huo ulifuatia pendekezo la umoja wa Mabunge ya Afrika lililowasilishwa na katibu mkuu wake Koffi N'Zi tarehe 22 Oktoba, 2012 kufuatia kikao cha wajumbe wa umoja wa Mabunge ya Afrika kumchagua Mhe. Hamad kuwakilisha Afrika kuwania pendekezo hilo mbele ya kamati tendaji ya chama hicho.

Mhe. Hamad Rashid Mohamed, hii ni mara ya pili kuiwakilisha Tanzania na Afrika katika kamati mbalimbali za IPU ambapo mwaka jana katika Mkutano uliofanyika Mjini, Benn, Uswis, alichaguliwa kuwa mjumbe wa Kamati ya Fedha na Uchumi ya IPU cheo ambacho anakitumikia hadi hivi sasa.

Katika kamati hiyo ya ukaguzi wa ndani, Mhe. Hamad Rashid atafanya kazi pamoja na mjumbe mwingine aliyeteuliwa Mhe. Duarte Pacheko kutoka Ureno, ambapo wanatarajia kutoa taarifa ya kazi yao mwaka 2014 katika mkutano mkuu wa IPU

JIWE WALILOKATAA WAASHI LINAPOKUWA JIWE KUU LA PEMBENI
 
Ingawa aliwanyoosha akina Dr Slaa enzi alipokuwa kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni. labda huko anakutana na wajanja zaidi yake

Hapa ndipo unapoonekana mtu wa ajabu.Mambo ya kuwaanyoosha Dr Slaa yanahusika vipi hapa.Kitu kidogo tu kinaharibu hoja yako yote.
 
Hapa ndipo unapoonekana mtu wa ajabu.Mambo ya kuwaanyoosha Dr Slaa yanahusika vipi hapa.Kitu kidogo tu kinaharibu hoja yako yote.

usijali sana ukitaka kuniona mtu wa ajabu poa tu. lakini ukweli ndio huo

alipokuwa kiongozi wa upinzani bungeni wale mawaziri vivuli wote walikuwa wakipata tabu sana wanapoandaa bajeti zao na hata wakati mwingine walipaswa kutoa pesa zao mfukoni bila kupata msaada wowote wa Ofisi ya kiongozi wa upinzani wakati bajeti ni ya kambi ya upinzani.

Hili Dr Slaa hatasahau walivyokuwa wakifanyiwa na huwa anasema kwa uwazi hata kama wewe hupendi kulisikia.
 
Congrats Hon. Hamad Rashid

Nilikuwa namkubali sana wakati akiwa KUB lakini baada ya kuikosa nafasi ile akaporomoka kwenye ubinafsi na choyo dhidi ya CDM. Kwa ujumla huwa ni mchakapazi mzuri na mjenga hoja mzuri.
 
Kupitia CUFU mkuu!!! Bunge letu ninamtuambua kama mbunge halali wa CUF kama ilivyo kwa Kafulila na NCCR Mageuzi!!! Utaziweza SI HASA za nchi hii!!!?

Tunasubiri maamuzi ya jaji kama atamfunga jela makamu wa rais Maalim seif na Mtatiro wake maana dalili zaonyesha kuwa na hatia na kilichobaki ni kuangalia impact yake itakuwa nini wakifungwa maana kosa la kudharau mahakama halina faini, ni jela tu. Hamad kweli kiboko
 
Hongera Bw Hamad Rashid, mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CUF, na pia mlezi wa chama cha ADC.
 
Siyo mwadilifu kivile, anavimeo kibao anashindwa kulipa, anatoa cheques hewa, ukimpigia simu hapokei anaishia kuzima simu na kuhama line za simu. Hata ofisi kahamisha upanga hataki kutoa ushirikiano.
 
Ok anaiwakilisha Tanzania. Muungano ukivunjika ataiwakilisha nchi gani?
 
Back
Top Bottom