AridityIndex
Senior Member
- Mar 22, 2011
- 149
- 38
na Khamis Mvulla, Mtwara
HALMASHAURI ya Tandahimba mkoani Mtwara imepata hati safi ya mahesabu baada ya ukaguzi wa Tamisemi.
Hayo yalisemwa na Abdallah Njovu, katibu wa baraza la madiwani na pia mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo katika kikao maalumu cha baraza la madiwani mwishoni mwa wiki.
Njovu alisema hati safi waliyoipata ni ya mwaka 2009-2010 baada ya ukaguzi wa hesabu ya Tamisemi na kuridhika na matumizi ya fedha za miradi zilizopelekwa katika halmashauri hiyo na kutumika vyema bila ubadhirifu na kuridhika na miradi husika iliyotekelezwa kwa viwango vinavyokubalika.
Aidha Njovu aliwashukuru madiwani pamoja na wakuu wa idara na vitengo kwa kusimamia vyema miradi yote na kupelekea kupata hati safi.
Katibu huyo wa baraza la madiwani alisema kuwa katika fedha za makusanyo ya ushuru wa halmashauri imekusudia kumaliza shida ya madawati ya shule za msigi 116 mwaka huu ambapo zimetengwa jumla ya shilingi 242,775,000 kwa kutengeneza madawati 4,866. shule zitakazonufaika na madawati hayo ni za tarafa ya Mahuta, shule 42; tarafa ya Litehu, shule 30; na tarafa ya Namikupa, shule 44.
Ni mara ya pili halmashauri ya Tandahimba inapata hati safi kufuatana na utekelezaji bora wa miradi na utumiaji mzuri wa fedha za miradi husika ya maendeleo wilayani humo.
Njovu alisema kuwa katika bajeti ya mwakani halmashauri yake ina mpango kabambe wa kuanzisha kituo cha redio FM abacho kitakuwa kichocheo kwa maendeleo ya watu wa Tandahimba.
Source: Tanzania daima. 5/05/2011
HALMASHAURI ya Tandahimba mkoani Mtwara imepata hati safi ya mahesabu baada ya ukaguzi wa Tamisemi.
Hayo yalisemwa na Abdallah Njovu, katibu wa baraza la madiwani na pia mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo katika kikao maalumu cha baraza la madiwani mwishoni mwa wiki.
Njovu alisema hati safi waliyoipata ni ya mwaka 2009-2010 baada ya ukaguzi wa hesabu ya Tamisemi na kuridhika na matumizi ya fedha za miradi zilizopelekwa katika halmashauri hiyo na kutumika vyema bila ubadhirifu na kuridhika na miradi husika iliyotekelezwa kwa viwango vinavyokubalika.
Aidha Njovu aliwashukuru madiwani pamoja na wakuu wa idara na vitengo kwa kusimamia vyema miradi yote na kupelekea kupata hati safi.
Katibu huyo wa baraza la madiwani alisema kuwa katika fedha za makusanyo ya ushuru wa halmashauri imekusudia kumaliza shida ya madawati ya shule za msigi 116 mwaka huu ambapo zimetengwa jumla ya shilingi 242,775,000 kwa kutengeneza madawati 4,866. shule zitakazonufaika na madawati hayo ni za tarafa ya Mahuta, shule 42; tarafa ya Litehu, shule 30; na tarafa ya Namikupa, shule 44.
Ni mara ya pili halmashauri ya Tandahimba inapata hati safi kufuatana na utekelezaji bora wa miradi na utumiaji mzuri wa fedha za miradi husika ya maendeleo wilayani humo.
Njovu alisema kuwa katika bajeti ya mwakani halmashauri yake ina mpango kabambe wa kuanzisha kituo cha redio FM abacho kitakuwa kichocheo kwa maendeleo ya watu wa Tandahimba.
Source: Tanzania daima. 5/05/2011