Zogwale
JF-Expert Member
- Jul 10, 2008
- 15,287
- 10,842
Mkuu umenena wazi na kweli kabisa. Wapinzani hapa ndipo wanapoudhi wapiga kura. Kwanza kila mpinzani ni lazima atizame maeneo ambayo comperative advantage kwa chama chake ipo. Kwa mantiki hii kama chama pinzani kina political comperative advantage jimbo fulani basi wakiachie ili kipambane na mmbadala wake ambao kwa sasa ni CCM. Kwa kawe ninaona Halima anafaa kuliko Mbatia hivyo Mbatia angemwacha Halima apambane na huyo msanii wa CCM na lazima angedondoka tu. Hata hivyo, bado mapema na Mbatia anaweza shauriwa ajitoe kwa sasa na kutangaza wafuasi wake wampe Halima. Kiukweli kama watabaki vijana hawa jua kabisa jimbo litachukuliwa na CCM. Upinzani ukitaka kufanikiwa ni lazima wakubali kufanya maamuzi magumu. Hii pia hata kwa wagombea urais sikuona mantiki ya kutoamua kumwachia yule ambaye tayari watu wana Imani naye na badala yake mnaweka wagombea ambao hata hawajawahi kusikika katika redio mbao na wengine ni wale wale ambao walishajaribu awamu zilizopita na kushindwa vibaya.
Lile jimbo la CCM, na wamemwaga posters kila kona, kila mti mpaka kwenye mitaro ya maji machafu. Halima hawezi kushinda.
Mkuu mabango si hoja!! Hata kule Marekani kwa Obama unataka kuniambia kuwa Republican hawakuwa na mabango au strategy?? Walishindwa pia!! Halafu nikuulize kama kweli huyo mgombea wenu anajiamini mbona anatumia nguvu kubwa sana kuomba hizo kura??Kama alifanya mambo mazuri si asubiri kura? Chema chajiuza kibaya chajitembeza!! Yaani anatumia nguvu kubwa na hela za walipa kodi kuwatuma mke na mtoto watangulie kupeleka bakuli la kuomba kura?? Subiri matokeo mkuu, tarehe 31 Oktoba si mbali.