Halima Mdee amchana Pinda live Bungeni Ardhi ya Mpanda

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,888
6,885
Mdee Pinda(1).jpg

Waziri Mkuu Pinda Na Mbunge Halima Mdee Bungeni
Wakijadili Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Ardhi

Mdee aonya machafuko kugombea ardhi


Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee aliitahadharisha Serikali kuwa kuipuuza sekta ya ardhi kutasababisha watu wa taifa hili kuchinjana."Sekta ya ardhi ndiyo uhai wa nchi hii. Sekta hii tukiipuuza... na ninaiambia Serikali tukiipuuza watoto wetu, wajukuu wetu watakuja kuchinjana na hatutaki kutengeneza Tanzania ya kuchinjana katika kipindi," alisema Mdee.

Akizungumzia kuhusiana na Kampuni ya Agri Soil ambayo imepewa eneo la uwekezaji katika Wilaya ya Mpanda, Mdee alisema mbali na upungufu wake imekiuka sheria."Imekiuka sheria ya nchi, sheria zetu zote ziko wazi na hili namwambia Mheshimiwa Waziri Mkuu asiposhughulikia vizuri anaweza akaanguka nalo kabisa kwa sababu kuna ushahidi wa moja kwa moja kuwa ofisi yake ilihusika tutumie busara tuokoe nchi," alisema.

Mdee alisema sheria inasema kama kuna ushirikiano unamhusu raia na kwamba sheria ya uraia haijatambua halmashauri na kuhoji kuwa Serikali iwaambie wabunge ni raia gani anamiliki hekta zaidi ya 200?

Mgogoro wa shamba hilo uliibukia kwa mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Pudenciana Kikwembe ambaye aliitaka serikali kutoa asilimia 25 ya hisa katika shamba hilo kwa wazawa na kwa sababu madiwani walishirikishwa katika suala la Agro Soil basi waamue gawio la faida litakwenda katika mradi gani.

Mwananchi

Halima Mdee, Serukamba jino kwa jino

MBUNGE wa Kigoma Mjini (CCM), Peter Serukamba, amemponda Mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema) kuwa ni muongo na anapeleka siasa uchwara bungeni.

Mdee amemjibu Serukamba kwa kumweleza kuwa, anamuonea huruma kwa kuwa hajui kama mwaka 2015 Mbunge huyo atarudi bungeni.

Serukamba alisema, wabunge waache kutafuta umaarufu kwa kusema uongo bungeni na kwamba, wananchi wa Kigoma ndiyo wanaofahamu hali halisi ya mambo yao. "Huo uzalendo uchwara unaoletwa leo hatuutaki Kigoma, tunataka maendeleo' amesema Serukamba alipoomba kutoa taarifa wakati Mdee anachangia bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Mdee amesema, hatafuti umaarufu kwa kuwa yeye tayari ni maarufu, anataka kufanya kazi. Mbunge huyo amesema, hazungumzi kitu ambacho hana ushahidi nacho hawafanyi uchochezi. " Hatutafuti umaarufu wa kisiasa, upo tayari, tunataka kuijenga nchi yetu" amesema Mbunge huyo kijana, Waziri Kivuli wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Amemtahadharisha Waziri Mkuu awe makini katika kushughulikia mkataba unaodaiwa kummilikisha mwekezaji eneo kubwa la ardhi mkoani Rukwa, kwa kuwa inadaiwa kuwa ofisi yake imehusika. Kwa mujibu wa Mdee, mkataba huo umekiuka sheria za nchi na kwamba, Pinda asipokuwa makini ‘ataanguka nalo'. Amewataka wabunge waache ushabiki, hilo ni tatizo kubwa.

Baada ya Mdee kusema hivyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Mary Nagu aliomba kutoa taarifa, akasema, hakuna sheria iliyovunjwa Rukwa, na hakuna mwekezaji aliyemilikishwa ardhi mkoani humo.

Mdee amesema bungeni kuwa haitaki taarifa ya Nagu, na anashangaa kuona kuwa wanaopaswa kutekeleza sheria wanatetea uhalifu. Mbunge huyo amesema, anataka haki itendeke kwa wananchi wa Kwembe na Mabwepande mkoani Dar es Salaam na atakuwa na wananchi hao hadi mwisho. "Sisi tutakufa na wananchi wetu, liwe jua, iwe mvua"amesema Mbunge huyo na kusema, Serikali inapaswa kuweka utu kwanza, iache siasa zifanywe na vyama.

Ameiomba Serikali itumie busara kushughulikia mgogoro wa ardhi eneo la Chesimba, na amewatuhumu baadhi ya wenyeviti wa mitaa na madiwani wasio waaminifu kuwa wanauza maeneo. Amedai kuwa, maeneo ya wazi yakiwemo yakiwemo yaliyotengwa kwa shughuli maalum yanauzwa, na kwamba, wakubwa wanajenga ‘mabangaloo'. Amesema, ardhi ndiyo mhimili wa nchi na kwamba, sekta hiyo ikipuuzwa baadaye wananchi watachinjana.

"Sekta hii ikipuuzwa Watoto wetu, wajukuu wetu watakuja kuchinjana, hatutaki kutengeneza Tanzania ya Watanzania kuja kuchinjana" amesema Mdee.


Source Habari Leo.

 
Pinda kaishasema yuko tayari kutetea hii kitu hata kama itammaliza
tuna waziri mkuu kweli?
 
Alichangia vizuri kama kawaida yake,kina Pinda hawawezi kutenda tofauti na kinachofanyika,ardhi kibao ziko mikononi mwa wazawa au wawekezaji bila kufuata sheria kikamilifu
 
Wapiganapo fahali wawili ziumiazo ni nyasi...
Hofu yangu isije ikaonekana kuwa CDM ndiyo
wameleta vurugu pindi zitakapotokea
 
Nadhani Mnyika awahishe Hoja binafsi ya kutokuwa na IMAN nae. Kama wabunge wa magamba watampitisha atuletee uraiani hiyo hoja. Nguvu ya umma itumike. PM anaboa. Kila kitu anapotosha
 
Achilia mbali kuchanwa hata wakipasuliwa live hawaelewi chochote hawa wana roho ngumu kama paka mwitu. Dhuluma kibaoooo.
 
Tanzania haina rais,waziri mkuu wala serikali, kuna genge la wahalifu wanajiita serikali na mwisho wao hauko mbali. Huyu Pinda ni dhaifu sana kama bosi wake.
 
Hii serikali na watendaji wake inanikumbusha ka msemo haka'KENGE HASIKII MPAKA DAMU ZIMTOKE MASIKIONI" Huyu waziri mkuu mpaka aone nguvu ya umma ndo atajua kumbe enzi za unyapara zimepita
 
Watu wa Nape wako wapi JF jamani? Naona mijadala inapita tu bila kupingwa make wale watu nao wana umuhimu wao kwa kuchangamsha genge.

Kina MS, FF na wenzake siwaoni na ninawamiss.
 
Pinda ni msanii tu, anadai yeye ni mtoto wa mkulima lakini hao wakulima wenyewe ndo anawasaliti kila uchao
 
Watu wa Nape wako wapi JF jamani? Naona mijadala inapita tu bila kupingwa make wale watu nao wana umuhimu wao kwa kuchangamsha genge.

Kina MS, FF na wenzake siwaoni na ninawamiss.

Nape anawabania sana anadai anawalipa mamilioni kumbe anajishibisha mwenyewe sasa wamesusa mpaka fungu liongezeke, magamba bwana kwa kuzimiana taa,wamekubuhu.
 
Kwakuwa taarifa zilizopo zinaonyesha kwamba uongozi mzima wa wilaya kuanzia kwa mkurugenzi hadi madiwani walilipiwa trip ya kwenda marekani na huyo 'mwekezaji',katika mazingira kama hayo tusitarajie jambo ama kauli tofauti na hiyo ya pinda.
Mtoto wa mkulima keshasema hii ndo awamu ya mwisho kuwania ubunge,sasa kwanini ahangaikie maslahi ya watu wengine hadi akose muda wa kujiandaa kuwa muwekezaji. Tumesikia mawaziri wakuu kadhaa waliomtangulia wanavyowekeza kwa kuhodhi mahekari ya ardhi huku wananchi wa maeneo husika wakitaabika.
Kinachozidi kudhihirika kila mara ni kwamba wanamagamba wote wanafanana, kama alivyowahi kusema baba wa taifa; wanamagamba wote 'manzi ga nyanja' muda wote wao wanatekeleza sera yao ya chukua chako mapema.
Hata wale wanamagamba wachache waliokuwa wanaaminiwa na wananchi japo kidogo lakini nao wameanza kuwakatisha tamaa.
 
Na huyo Serukamba ni samsingi ya yule mdosi fisadi aliyesukumwa korongoni mwezi uliopita. Kila siku alikuwa akishinda katika outer office ya RA (caspian) utadhani alikuwa mlinzi wake.

Halafu nyie watu wa Kigoma vipi mnamchagua huyu Mrundi kuwa Mbunge wenu?
 
Watu wa Nape wako wapi JF jamani? Naona mijadala inapita tu bila kupingwa make wale watu nao wana umuhimu wao kwa kuchangamsha genge.

Kina MS, FF na wenzake siwaoni na ninawamiss.

Wameishiwa nyimbo -- walifikiri chejo???
 
ya pinda tumwachie pinda ayapindue ili apinduke nayo.Ndo maana ukimwangalia usoni amejaa matuta utafikiri ngiri ajuza sababu ya unafiki wake
 
Back
Top Bottom