Halima Mdee achambua mswada wa sheria ya vyama vya siasa bungeni

Asha Abdala

JF-Expert Member
Mar 21, 2007
1,130
44
Halima Mdee, Msemaji wa kambi ya upinzani bungeni wizara ya sheria na katiba leo ameuchambua mswada wa mabadiliko ya sheria ya vyama vya siasa uliowasilishwa bungeni. Mbunge huyo ameeleza wazi kwamba serikali ya CCM haina nia ya kuongeza demokrasia nchini badala yake imeonyesha woga wa kiasiasa. Maoni yake hayo yametokana na Serikali kuwasilisha bungeni mswada ambao umetoa nafasi kwa vyama vya siasa kuungana lakini wakati huo huo ukitamka kwamba kama vyama hivyo vikiungana rais, wabunge, madiwani na viongozi wote wa kuchaguliwa watapoteza nafasi zao na uchaguzi kurudiwa. Ametaka sheria iruhusu pia aina zingine za ushirikiano kama alliance na coalition, badala ya kulazimisha kuungana pekee.


Halima Mdee amekwenda mbali zaidi na kuchambua kuwa kikwazo kikubwa ni baadhi ya vifungu vya kikatiba ambavyo vinatamka kwamba mbunge akihama chama anapoteza nafasi yake. Lakini ameeleza kuwa katiba hiyo hiyo inajichanganya kwa kuwa upande wa Rais hakuna sharti la Rais kupoteza nafasi kama atahama chama. Mdee ameitaka serikali ya CCM ikubali mabadiliko ya katiba kwa ajili ya kupanua demokrasia nchini.


Mbunge huyo ametaka vilevile, msajili wa vyama kutangaza kwenye vyombo vya habari ripoti za fedha za vyama zinazoonyesha mapato na matumizi.


Akichangia mswada huo, mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe ameipongeza serikali kutaja katika mswada huo kwamba mahesabu ya vyama sasa yatakaguliwa na Mkaguzi Mkuu wa Serikali(CAG) hasa fedha zinazotokana na ruzuku. Amesema hatua hiyo itasidia pia kudhibiti vyanzo vichafu vya fedha za kuendesha vyama ambapo kwa kiasi kikubwa chama tawala kimekuwa kikiendeshwa kwa fedha nyingi za namna hiyo ikiwemo katika uchaguzi.

Zitto ametaka pia sheria hiyo ya vyama vya siasa itoe fursa ya kupatikana kwa National Consesus ama muafaka wa kitaifa. Amesema hatua hiyo itawezesha kuwa na tunu za kitaifa pamoja na utofauti wa vyama vya siasa. Ametoa mifano ya nchi duniani ambazo zina mfumo wa kuwa na national consesus



Asha
 
Hawa jamaa wanajitahidi ila serikali ya CCM haiwezi kukubali kuweka uwanja sawa kwani huo ndio utakuwa mwisho wao. Kama hakuna Katiba iliyokubaliwa na wadau wote, hata sheria zikiwa nzuri kiasi gani matatizo yatakuwepo tu. Laiti CCM wangejua kuwa endapo akitokea kichaa akachukua nchi tukiwa bado na sheria za hovyo na katiba ya chama kimoja basi wataoteseka zaidi ni wao. Kwani jamaa akiamua kusweka mtu yeyote detention, sheria itamlinda na akiamua katibu wa chama chake awe mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ni poa tu. Laiti watawala wetu wangejua kuwa mwisho wa siku watakaoteseka ni wananchi wa kawaida, basi wasingeendekeza ubinafsi uliozidi kipimo.!
 
Madai ya upinzani siku zote ni yale yale hayabadiliki hata mpinzani afe leo akifufuka mwaka 3000 malalamiko yale yale jamani tunataka mabadiliko ambayo yanaanzia kwenu huko huko katika upinzani tunataka mambo mapya
 
Hiyo ya kufanya auditing hata mimi naiunga mkono sana. Na hili sio kwa chama tawala pekee yake, bali hata kwa upande wa vyama vya upinzani. Kumekuwa na malalamiko juu ufujaji wa fedha za ruzuku unaofanywa na viongozi wa baadhi ya vyama vya siasa. Hii inawezekana ikawa ni kweli au labda ni propaganda tu za wapinzani wao. Lakini ukaguzi wa fedha hizi utaondoa kabisa malalamiko na kusingiziana. Vivyo hivyo, kwa upande wa chama tawala watadhibitiwa kupokea hela chafu kutoka kwa akina Somaiya na wengineo.
 
upinzani wa kisiasa si kupinga kila kitu bali ni ushindani wa hoja na sera wananchi wakizikubali basi chama chenye sera zilizokubaliwa kitashika hatamu.

kwa mfano Wanadai ccm inabana uwanja wa demokrasia kwa kuogopa kung'olewa hili si sawa wakati ukifika hakuna ubishi kama yaliyotokea Ghana yanaweza kutokea hapa pia,lakini tunahitaji uvumilivu,upinzani wa kweli na demokrasia ya kweli ndani ya vyama vya siasa.

kwani utakuta baadhi ya vyama vya siasa hapa nchi tangu kuanzishwa kwao mwenyekiti ni mtu huyohuyo hata kwenye nafasi ya uraisi ni huyohuyo, sasa hapa unaweza kiuliza hivi ndani ya chama hicho hakuna wanafaa zaidi yake.

wazungu wansema charity start at home,wapinzani waanze kuimarisha na kujenga demokrasia kwanza ndani ya vyama vyao si vinginevyo.

Na muswada huu uliopitishwa leo na bungev letu tukufu naamini kuna baadhi ya vyama vitapata wakati mgumu sana hasa baada ya sheria hii kumpa meneo msajiri na CAG.

Maana vingi naamini vilikuwepo au kuanzishwa kwa maslahi binafsi kama Mbunge mmoja wa chama tawala alipokuwa anachangia hoja hii leo bungeni.

Hakuna haja ya ktumia nguvu sera bora na hoja zenye maslahi ya taifa letu ,watanzania si wajinga wataona na kuamua.
 
Madai ya upinzani siku zote ni yale yale hayabadiliki hata mpinzani afe leo akifufuka mwaka 3000 malalamiko yale yale jamani tunataka mabadiliko ambayo yanaanzia kwenu huko huko katika upinzani tunataka mambo mapya

Wapinzani ni kina nani?

Upinzani ni hali siyo jinsia au namna yeyote ambayo mtu anazaliwa nayo.
Katiba ni ya nchi si ya chama tawala wala watu waitwao wapinzani.
Mabadiriko ya katiba ya nchi yanaanzia ndani ya katiba ya nchi siyo ndani ya chama. Huwezi kubadiri kifungu chochote ndani ya katiba ya chama ili kufanikisha mabadiriko ndani ya katiba ya nchi, katiba ya chama ni kikundi cha watu wakati katiba ya nchi ni kila mwananchi bila kujali itikadi yake. Au labda sikuelewa maana ya ujumbe wako.

Kudai kwamba wapinzani siku zote madai yao ni hayo hayo ni kuanzisha hoja isiyoweza kusimama yenyewe.
Haipiti miaka 10 CCM watakuwa upande wa pili. Nasema hivi kwa sababu nguzo zote za CCM zimebomoka imebakia nguzo moja tu, Fedha, nayo kwa asili yake wimo wake hautabiriki. Umoja uzalendo na utaifa ndani ya CCM ni mambo ya kihistoria. Fedha ndilo jambo pekee linalo waunganisha wana CCM watoto vijana wazee na vikongwe kama akina Kawawa, Malecela,Msekwa na Kingunge.

Ni vema kila mtu kusoma alama za nyakati na kuzitafakari.
Kuvunjika kwa iliyokuwa dola kubwa na yenye mabavu, dola ya Urusi kulileta madhara makubwa karibu katika kila nchi duniani. Hakuna nchi ambayo haikukumbwa na kishindo cha vunjiko hilo.
Aidha nchi nyingi zilizo tegemea uwepo wake moja kwa moja hasa zile za Ulaya ya Mashariki zilimegeka vipande vipande na kufufua uhasama wa zamani. Uhasama huo unaendelea mpaka leo hii.

Mabadiriko ya kisiasa kiuchumi na kiutendaji yanayoendelea nchini Marekani hivi sasa na anguko la kubwa la mfumo wa fedha na uchumi duniani lililotokana na Uchoyo na pupa ya utajiri kutoka kwa watu wachache wanaodhani fedha ndo kila kitu,yataweka watawala wengi wakongwe katika nchi nyingi duniani katika benchi la mauti muda si mrefu. Tanzania ni moja ya nchi za dunia ya tatu zenye utawala mkongwe uliovurugika na kuingia giza, sioni sababu hata moja ya kuzuia utawala wa CCM kuonja mauti.

Kwa sababu CCM iko madarakani na viongozi wake hawaoni ni sababu zipi zitawaondoa madarakani, hawaoni haja ya kurekebisha mambo mengi yenye utata wa kiutendaji ndani ya katiba.
Siku watakayo tambua kwamba chama chochote cha kisiasa kinaweza kuwa katika kambi ya upinzani, ndiyo siku watakayojua kwamba katiba hii wanayoipuuzia ni jambia likalo kuwili. Upande mmoja wa jambia hili sasa hivi unawakata wengine (Wapinzania) kitu ambacho si cha kuhofia kwa muda huu, upande wa pili ambao sasa hivi unaoendelea kunolewa kwa nguvu zote ni wa kuwakata wao lakini nao pia si kitu ambacho kinawatia hofu.
Mseto huu wa mamtatizo ya nje na ya ndani ni lazima ulete changa moto itakayopelekea kila mtu kutaka kujua kwa dhati, kulikoni. Hiyo kulikoni kutoka kwa kila mwananchi ndo hofu yao kuu CCM.

Wapinzani ni kina nani?
 
Last edited:
mwanzo kulikuwa hakuna haja ya vinasa sauti kwa sababu huyo huyoi zitto ndiye aliyekuwa nalikisha kila kitu

halafu mnatafuta mchawi...

psx839hd8r1y2cxmr2x.jpg
 
Last edited:
Wakuu,

Mimi naungana na huyu mwanamama, katika kauli yake kuwa CCM na serikali ni waoga sana kuondolewa katika madaraka. Uoga huu unadhihirika, sio tu katika muswada huu bali katika katiba zote mbili za CCM na ile ya nchi. Uoga pia unaashiriwa katika muundo na utendaji wa serikali.

Tanganyika ilipata uhuru wake kutoka kwa Waingereza chini ya Katiba ya Lancaster ya mwaka 1961. Katiba iliyotuwezesha kuwa na serikali iliyochaguliwa, yenye bunge lenye nguvu, kwa bunge ndio sauti ya wananchi, tulikuwa na vyama vingi vikiwa na uwanja shwari na huru wa ushindani wa kisiasa na mahakama huru yenye msimamo usioingilika na ushabiki wa kisiasa.

Lakini, mwaka mmoja tu baada ya uhuru huo, nchi ikapewa katiba mpya. Katiba ya Jamhuri ya mwaka 1962. Matatizo yote ya kisiasa tuliyonayo, yalianzia hapo.

Katiba hii ya ilituletea mfumo wa Urais mwenye mamlaka yote na nguvu zote za uendeshaji wa serikali na nchi. Kiasi ya kwamba Rais alipewa uwezo, chini ya katiba hii, ya
kuiendesha nchi na serikali atakavyo yeye binafsi bila ya kuzingatia maelekezo na ushauri wa mtu yeyote mwingine.

Katika kutengeneza eneo la kujidai la Rais huyu mwenye nguvu zote, ikapitishwa sheria ya kumpa uwezo wa kumsweka mtu lupango bila kupitia mahakamani ya 1962.

Mapema tu ulipoanza mwakw wa 1963 pakatangazwa kuwa Kamati ya Halmashauri Kuu ya Tanganyika African National Union (TANU) imeamua kuifanya Tanganyika kuwa nchi ya utawala wa chama kimoja, nacho ni TANU. Hali hii ilikuja bila ya kutafutwa maoni ya wananchi au ya vyama vingine vya kisiasa vilivyokuwapo.

Vyama vyote vingine vya kisiasa vilipigwa marufuku na TANU hatimaye CCM ikavikwa kilemba cha hatamu za nchi. Maamuzi yote ya nchi na serikali yamekuwa ni jukumu la CCM tangu hapo mpaka hii leo. Madaraka yote na nguvu zote za nchi ni za Rais kupitia National Executive Council na Central Committee ya CCM. Sauti ya wananchi kupitia Bunge ikazimwa.

Katiba zote zilizofuatia na marekebisho yake yote yako chini ya msingi wa katiba hii ya jamhuri ya 1962.

Kuviwekea vigingi na vizingiti vyama vya upinzani visipate upenyu wa kuungana ni moja ya maashirio ya uwoga wa CCM kuondoka madarakani. Kuzuia wagombea binafsi ni uwoga wa CCM kuondoka madarakani. Wanajua wagombea binafsi wengi wao watatokea humo humo CCM. Hali ambayo inaweza kuidhoofisha CCM.

Kuwanyima nafasi wabunge kuachana na vyama vyao (crossing the floor) ili wajiunge na vyama vingine au kubaki wabunge binafsi, ni uwoga wa CCM kuondoka madarakani. Kwa hiyo wabunge wanawekewa mkwara wa kupoteza ubunge wao.

Kuwalazimisha wabunge watetee vyama vyao badala ya wananchi waliowachagua kutoka majimbo yao ya uchaguzi ni ushahidi mwingine wa uwoga wa CCM kuondoka madarakani.

Napenda kuitumia fursa hii kumpongeza huyu mwanamama kwa kazi nzuri aifanyayo bungeni kwa kushirikiana na wabunge wenzake wa upinzani katika kuidabisha serikali na CCM. Hata kama lolote la maana halitafanyika. lakini ujumbe utakuwa umefika.
 
Back
Top Bottom