BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,011
[h=3]Tanesco yakata tamaa [/h]
*Yasema hali tete, ratiba ya mgawo yatupwa
Na Benjamin Masese
Majira
SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema kuwa hali ya mgawo wa umeme nchini kwa sasa ni tete kutokana na uzalishaji wa nishati hiyo kuzidi kupungua na kufikia hatua za mwisho za kuzimwa kwa mitambo.
Vile vile limesema kwamba halitaweza kufuata ratiba iliyotolewa awali ya mgawo wa umeme na hivyo kuwataka wananchi kukubaliana na hali iliyopo sasa hadi serikali itakapofanikisha mipango yake kuhusu suala hilo.
Hayo yalisemwa na Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Badra Masoud wakati wa mahojiano na gazeti hili kwa njia ya simu kuhusu kutofuatwa kwa ratiba ya mgawo wa umeme iliyotolewa awali ambayo imesababisha malalamiko kwa wananchi.
Bi. Masoud alisema kuwa ratiba hiyo imeshindikana kufuatwa kutokana na kiwango kidogo cha umeme kinachozalishwa ambacho kwa muda mwingine kipanda na kushuka, hivyo kuwapa wakati mgumu wa kuwahudumia wateja wake.
Alisema kuwa hakuna njia mbadala ya kuepusha tatizo hilo, kwa kuwa tayari limeshakuwa kubwa.
Kinachotakiwa sasa, alisema ni uvumilivu na subira wakati serikali ikiwa katika mchakato wa kuepusha nchi isiingie katika giza.
"...kwa hilo ni kweli hatuwezi kufuata ratiba tuliyoitoa awali kwa sababu ya kiwango cha uzalishaji kupungua kila wakati, yaani kinapanda na kushuka...sasa ukisema unafuata ratiba utasababisha migogoro, naomba wananchi watambue kwamba hali ni tete na tukubaliane na hali hii," alisema.
Hivi karibuni, vyombo vya habari vilisema makali ya mgawo wa umeme yameongezeka kutoka saa nane hadi 18 kwa siku katika mikoa mbalimbali ikiwemo Tabora, Kilimanjaro, Arusha na Dar es Salaam.
*Yasema hali tete, ratiba ya mgawo yatupwa
Na Benjamin Masese
Majira
SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema kuwa hali ya mgawo wa umeme nchini kwa sasa ni tete kutokana na uzalishaji wa nishati hiyo kuzidi kupungua na kufikia hatua za mwisho za kuzimwa kwa mitambo.
Vile vile limesema kwamba halitaweza kufuata ratiba iliyotolewa awali ya mgawo wa umeme na hivyo kuwataka wananchi kukubaliana na hali iliyopo sasa hadi serikali itakapofanikisha mipango yake kuhusu suala hilo.
Hayo yalisemwa na Meneja Uhusiano wa TANESCO, Bi. Badra Masoud wakati wa mahojiano na gazeti hili kwa njia ya simu kuhusu kutofuatwa kwa ratiba ya mgawo wa umeme iliyotolewa awali ambayo imesababisha malalamiko kwa wananchi.
Bi. Masoud alisema kuwa ratiba hiyo imeshindikana kufuatwa kutokana na kiwango kidogo cha umeme kinachozalishwa ambacho kwa muda mwingine kipanda na kushuka, hivyo kuwapa wakati mgumu wa kuwahudumia wateja wake.
Alisema kuwa hakuna njia mbadala ya kuepusha tatizo hilo, kwa kuwa tayari limeshakuwa kubwa.
Kinachotakiwa sasa, alisema ni uvumilivu na subira wakati serikali ikiwa katika mchakato wa kuepusha nchi isiingie katika giza.
"...kwa hilo ni kweli hatuwezi kufuata ratiba tuliyoitoa awali kwa sababu ya kiwango cha uzalishaji kupungua kila wakati, yaani kinapanda na kushuka...sasa ukisema unafuata ratiba utasababisha migogoro, naomba wananchi watambue kwamba hali ni tete na tukubaliane na hali hii," alisema.
Hivi karibuni, vyombo vya habari vilisema makali ya mgawo wa umeme yameongezeka kutoka saa nane hadi 18 kwa siku katika mikoa mbalimbali ikiwemo Tabora, Kilimanjaro, Arusha na Dar es Salaam.