Hali ya serikali ni tete? Mpaka sasa mishahara kitendawili

Hata mimi sijasema kwa miezi miwili lakini dalili zimeanza kujionyesha hasa miezi hii miwili. Hivyo ina maana serikali ilianza zamani sana kuyumba kiuchumi lakini hatuwahi kunotes dalili mapema.
Ok, nashukuru mkuu kwa kuongeza mawe ya ukweli kabisa katika tetesi hizi tunazozijadili.
Ukweli ni kwamba hali itaendelea kuwa mbaya kwa sababu mali zetu ambazo zingetusaidia kujitegemea kiuchumi zimeshamilikishwa kwa wawekezaji ambao wameingia mikataba ya kijinga na kuondoka na mali zote!!!

Na hili ndiyo kilio cha upinzani kilichowapa umaarufu kwa wananchi.
Mwisho, ubarikiwe kwa hoja iliyoenda shule.

Kuna watumishi wa umma wameshiriki mafunzo Botiswana. Wanasema kule mtumishi wa umma wa chini anapata tsh. 1,800,000/- Na hapo ana uhakika wa mkopo wa kujenga nyumba ya kisasa ambapo serikali haikupi mkopo mpaka uoneshe nyumbani kwenu ambako ni sharti ujenge nyumba ya maana.

Wana maslahi mazuri kwa kuwa, gold na diamond yao wamewakabidhi wawekezaji kwa kugawana 50% wakati mwekezaji anatakiwa kufuata matakwa mengine kama kulipa kodi, kulipia lesseni ya biashara na sheria nyingine. Waliowekeza pale ni makaburu wa SA, watu wanakula bata kiivyo.

Sasa kama watumishi wa umma wanaolalamika leo, waungane kwa pamoja wapinge unyanyasaji unaofanywa na serikali haiwezekani? Polisi na JWTZ ndo wajinga kabisa, sitaki hata kuwaona. Walimu na maisha yo duni nao bado hawajabadilika. Eti mtu anajivunia kupewa tsh. 200,000/= atumie mwezi mzima? kwa vijijini inawezekana, kwa hawa wanoishi mijini tena nyumba za kupanga, si wanaishia kuwa wajasiria mali na kuwatelekeza watoto ili watafute hela ya kula na kulipia pango la nyumba?

Ama kweli we are controlled by false Consciousness.

 


Itanisaidia sana kumjibu. Serikali inapata nguvu ya kuuza rasilimali kinyemeala kwa kuwa niliowabold wanashiriki kwa kiasi kikubwa ndo jeuri ya serikali. Kuna dogo alishawahi kuniambia kuwa, huwa kuna magari ya serikali yanapelekwa kwenye mining site, wanapewa tofali za dhahabu, cha kushangaza, kwanza gari hizo zinaondolewa namba za usajili halafu pili, zinakuwa na escort ya polisi.

kuwajibu hawa wa majeshini, nawaambia ndiyo serikali mnayoilinda, kwani kama mngekuwa pamoja na wananchi tungehakikisha tunawaondosha na kuanza kusimamia rasilimali zetu kwa manufaa ya watanzania.

Majeshi wengui ni wajinga, wapuuzi, washenzi, kwani wanawalinda mafisadi wakiwa na bunduki, wanapelekwa mahala kuiba na bunduki lakini hawachukui hatua yoyote tena bila wao kunufaika kwa tija kwani wananishiwa kupewa 10,000-50,000, basi askari anaona kaukata. Hivyo, wanavuna wanachokipalilia.

Mwisho nitawashauri washituke, walinde wananchi wanaodai uhuru wao siyo kuwalinda mafisadi wanaotuingiza mkenge kila uchwao


Sasa nimekupata vyema. Uko sahihi lakini naomba nikujuze kitu fulani kuwa hao askari viongozi wao wengi hawana shida kabisa kwa sababu ya marupurupu na ufisadi wanaoufanya.
Kazi yao ni kukilinda chama tawala kwa gharama yoyoye ile!!!!! Askari walio chini wengi ni form 4 hivyo hata vimshahara wanavyopewa wanaona vinakidhi haja lakini wanashindwa kujiuliza kwa nini hawalipwi stahiki zao kwa wakati, mathalani mtu akihama,likizo n.k
Majuzi nilikuwa nasikia Nahodha Shamsi Vwai akisema serikali imelipa 14bill madeni ya Polisi na Magereza ambayi ni mwaka 2007-2009 June. Kwa hiyo ina maana mpaka sasa serikali bado inadaiwa madeni ya 2009 July - 2011 na bado wanaichekea serikali kwa kupiga wananchi na kuzuia maandamano kila kukicha halafu wananchi hao hao ndiyo wanaorudia kwa kuwaomba rushwa na kuwabambikia makosa ya uongo!!!
Inasikitisha sana, naomba siku wakose kabisa mishahara ili viti visikalike huko maofisini.
 
nchi hii tumeifilisi wenyewe kwa kuwaruhusu viongozi kuitwala na kuiuza kwa wezi wanavyotaka, lazima ile kwetu sote si kwa watumishi wa umma tu, bali kwa kila mtanzania, kwani mtumishi wa umma akikosa pesa ya kununua mazao, hata mkulima shambani atahaha kutafuta soko la mazao yake.

Ndiyo maana tunahitaji kuungana kupinga unyonyaji
 
DazNaz nashukuru kwa uchambuzi yakinifu kwa kadri ya uelewa wako. Lakini bado nipo pale pale, kwa nini wacheleweshe mishahara wakati awali kwa watumishi wa serikali hasa majeshi hali hiyo ilikuwa nadra sana?
Kuhusu idara nyingine kama walimu na wafanyakazi wa halmashauri hao ni kama kawaida yao kucheleweshewa mishahara na wameshazoea yaani wamejitune hivyo.
Tuachane na hilo la mishahara tuje kwenye dalili za serikali iliyo na hali mbaya kiuchumi ni zipi sasa ili tuzifitishe kwenye serikali yetu tuone kama zinafiti au zinakaribia kufit.

Hilo la majeshi kutolipwa mishahara nimegundua sio kweli. kabla sijaandika post hii, niliongea na askari polisi wawili ambao wamesema wameshalipwa. Aidha nimeongea na ofisa mmoja wa JWTZ, nae anasema wamelipwa isipokuwa kuna wengine ambao ni kweli hawajalipwa lakini anasema tatizo sio serikali, bali ni NMB. Huyu mheshimiwa anasema cheki NMB imeenda mapema sana lakini tatizo ikawa kwao. Ukumbuke kwamba, hivi karibuni NMB wamefanya mabadiliko katka mfumo wao wa kibenki uliosababisha hata namba za wateja kubadilika. Anaamini, hiyo ndiyo iliyochangia wanaolipwa kupitia NMB wawe bado hawajapa mishahara yao. Hata hivyo, nakubaliana na wewe kwamba, inapotokea serikali ikashindwa hata kulipa majeshi, basi kweli hali ni mbaya, lakini imethabitika kwamba wanajeshi (polisi na JWTZ) wameshalipwa!


1.0 Matumizi kuwa makubwa kuliko mapato yake ya ndani. Hii ina maana ni lazima serikali itafute misaada, mikopo ili kufinance matumizi yake ya kawaida ambayo ni recurrent expenditure. Ikitokea kutokukopesheka ndani na nje ya nchi basi serikali haina jinsi bali kubana matumizi ili iweze ku meet crucial exp. hasa mishahara ya watumishi wake.

Bado hadi sasa hakuna matumizi makubwa ya kutisha ambayo hayakutarajiwa. Matumizi kama hayo huwa yanakuja na matukio ambayo hayakutarajiwa kama vile uvamizi kutoka nje(vita), majanga ya asili (kama ilivyotokea Japan) na mambo mengine kama hayo. Lakini matumizi makubwa yaliyopo, tangu zamani yalikuwapo, sana sana yamepunguzwa. Bajeti miaka ya miaka ya nyuma, ilikuwa inategemea ufadhili kwa over 40% na sasa ni chini ya 30%....kwahiyo, kama kuna kipindi ambacho mapato ya ndani hayatoshelezi zaidi basi sio kipindi hiki. Kwahiyo, hapo hoja uyangu ni kwamba, ikiwa tiulishindwa kufilisika wakati mapato yapo below 300bn hatuwezi kufilisika sasa wakati mapato yapo above 400bn wakati mambo mengine yapo sawa with exception of inflation. naamini wewe si mmoja wa watu wanaochukuwa mapato na ku-convert into USD na ku-conclude instead of adjusting inflation.


2.0 Deni lake la kitaifa (ndani na nje) kuongezeka kwa kasi huku rate ya ulipaji ikiwa ndogo. Hii ina maana baada ya muda mfupi itashindwa kukopesheka na kufa kifo cha mende.

Takwimu za mwisho zinaonesha kwamba deni la taifa ni 30% ya GDP na hata kama limeongezeka bado haliwezi kufika 35% of GDP.Aidha, kiwango cha kutokukopesheka ni 60% of GDP, therefore, bado sana kufika huko!

3.0 Baada ya njia nilizokutajia hapo juu kushindwa basi serikali huamua kuprint new money na kuingiza kwenye mzunguko kinyemela na hii direct huongeza mfumuko wa bei. Hili limeshafanyika na serikali ya JK lakini usinihoji nimepata wapi information hizo.

Lazima nikuhoji kwavile nafahamu Money Printing as the source of government revenue ni very serious issue ambayo ni kweli inaashiria hali mbaya kabisa ya kiuchumi. Na mara nyingi, njia hii inatumika pale serikali inapokuwa haina option kabisa; haikopesheki na wala haina source ya kueleweka ya mapato. Bado TZ hali hiyo haipo kabisa kwani pamoja na ufisadi uliopo bado mapato yanakusanywa. Ni kweli, inapokuja money printing na kuzimwaga kwenye mzunguko, hapo inachochea kwa kiasi kikubwa inflation. Hata hivyo, inflation hiyo sio hii tunayoishuhudia sasa ambayo ukitoa inflation inayotokana na nishati na chakula, tunabaki kwenye single digit inflation. Inflation kwa TZ ni ndogo kuliko Kenya na Uganda(though not justification). Terible inflation inayotokana na uchapishaji wa noti inaonekana hata na mtoto mdoogo na huwa ina-affect hadi financial industry! Na hapo ndipo utakapokuta interest rates on savings accounts inafika zaidi ya 30% !!

Mkuu ni mengi lakini nimalizie kama unaamini serikali haipo dhofu li hali kiuchumi, nijibu kwa nini imeshindwa kupeleka Warrant of Funds katika idara zake kwa karibu miezi miwili sasa, na hili nalo usiniulize nimepata wapi.

Ni hayo, lakini amini hali ni mbaya serikalini. Chukua hizo changanya na uelewa wako utaanza kupata majibu.[/QUOTE]
 
nchi hii tumeifilisi wenyewe kwa kuwaruhusu viongozi kuitwala na kuiuza kwa wezi wanavyotaka, lazima ile kwetu sote si kwa watumishi wa umma tu, bali kwa kila mtanzania, kwani mtumishi wa umma akikosa pesa ya kununua mazao, hata mkulima shambani atahaha kutafuta soko la mazao yake.

Ndiyo maana tunahitaji kuungana kupinga unyonyaji
Kutokana na hali ya kisiasa inavyoonekana bado serikali haijagundua na inaamini katika nguvu ya dola. Kuna mtu mmoja alishawahi kusema ukiona serikali inatumia nguvu kubwa sana ya dola katika kuzima wapinzani ni dalili ya kushindwa kuongoza nchi.
Hali ndipo ilipofikia hapo.
Sumaye alishawahi kuongea kitu kuwa mpaka system nayo ikubalu uingie ikulu!!!
Ni ukweli usio na mashaka watu wa system hawapo tayari kuona nchi inashikwa na upinzani licha ya maovu na kadhia zote tunazopitia. Nashindwa kuelewa ni kwa nini wanataka kuwaamulia wananchi. Hofu yao sijui ni vibarua au nini!!!
 
Kiukweli hakuna tena consistency ya ulipaji mishahara nowadays, nakumbuka waraka wa karibuni ulitoka karibu na uchaguzi ukiagiza mishahara ilipwe si zaidi ya tarehe 25, nadhani ilikuwa ni kucapture kura za wafanyakazi then, maana baada tu ya uchaguzi things have gone twisting. mishahara haisomeki kabisa..last month imekuja imekatwa ovyo ovyo,Sitaki kuamini kwamba imefiliisika rather haitoi umuhimu kwenye hili, maana ebu ona effort na resources zinavyotumika kutangaza miaka hamsini ya uhuru...its boring maana watu hatma yao haieleweki nalafu unawaambia umethubutu,umeweza..in what?si bora tungeitangaza kilimanjaro kwenye new 7 wonders.
 
Mkuu naomba nikusahihishe, huyo Kameruni hakusema mwenye shida apige goti... alisema Nchi ikitaka msaada ishike ukuta na Tanzania haijasema lolote lenye kuonyesha msimamo mzito. Membe alibwata-bwata hapa kutuzuga kisha siku chache baadaye wakampokea Prince Charles kwa heshima zote, tunazijua haki za binadamu lakini kitendo cha kuliweka hili la ushoga kama sharti la misaada kwa nchi maskini ni matusi makubwa mno. Binafsi nalipinga kwa nguvu zote.
Nakumbuka niliona mahali hapa JF, member mmoja kaandika Kameruni alimwambia JK... "umezidi kuomba-omba, ukitaka msaada sasa shika ukuta..."

Mmmm...mimi simo!
 
Sasa nimekupata vyema. Uko sahihi lakini naomba nikujuze kitu fulani kuwa hao askari viongozi wao wengi hawana shida kabisa kwa sababu ya marupurupu na ufisadi wanaoufanya.
Kazi yao ni kukilinda chama tawala kwa gharama yoyoye ile!!!!! Askari walio chini wengi ni form 4 hivyo hata vimshahara wanavyopewa wanaona vinakidhi haja lakini wanashindwa kujiuliza kwa nini hawalipwi stahiki zao kwa wakati, mathalani mtu akihama,likizo n.k
Majuzi nilikuwa nasikia Nahodha Shamsi Vwai akisema serikali imelipa 14bill madeni ya Polisi na Magereza ambayi ni mwaka 2007-2009 June. Kwa hiyo ina maana mpaka sasa serikali bado inadaiwa madeni ya 2009 July - 2011 na bado wanaichekea serikali kwa kupiga wananchi na kuzuia maandamano kila kukicha halafu wananchi hao hao ndiyo wanaorudia kwa kuwaomba rushwa na kuwabambikia makosa ya uongo!!!
Inasikitisha sana, naomba siku wakose kabisa mishahara ili viti visikalike huko maofisini.

kazi ipo mkuu
 
Hivi TCRA si ndo ile Mamlaka ya Mawasiliano na kufanya nini cjui ambao wameshindwa kabisa kusimamia zoezi la usajili wa namba za simu?! anyway, habari za namba za simu sio issue; my interest ni kujua biashara inayofanywa na TCRA hata wawe na fedha za kulipa wafanyakazi wa serikali!!!

Kwa ufupi, kwa siku unatumia sh. Ngapi kwenye simu yako ya mkononi? Au kama unaenda internet cafe, kiasi unachotumia kule asilimia 18 inapelekwa TCRA kama VAT. Upo?
 
Kiukweli hakuna tena consistency ya ulipaji mishahara nowadays, nakumbuka waraka wa karibuni ulitoka karibu na uchaguzi ukiagiza mishahara ilipwe si zaidi ya tarehe 25, nadhani ilikuwa ni kucapture kura za wafanyakazi then, maana baada tu ya uchaguzi things have gone twisting. mishahara haisomeki kabisa..last month imekuja imekatwa ovyo ovyo,Sitaki kuamini kwamba imefiliisika rather haitoi umuhimu kwenye hili, maana ebu ona effort na resources zinavyotumika kutangaza miaka hamsini ya uhuru...its boring maana watu hatma yao haieleweki nalafu unawaambia umethubutu,umeweza..in what?si bora tungeitangaza kilimanjaro kwenye new 7 wonders.

Nakubaliana kabisa na wewe kwamba hivi sasa hakuna tena consistency ya ulipaji mishahara!!! Na hili ndilo tatizo la msingi na sio kufilisika. Tatizo ambalo linaweza kuchangiwa na mambo mengi ikiwa na pamoja na suala la utendaji, hususani wa hazina!!!
 
Kwa ufupi, kwa siku unatumia sh. Ngapi kwenye simu yako ya mkononi? Au kama unaenda internet cafe, kiasi unachotumia kule asilimia 18 inapelekwa TCRA kama VAT. Upo?

Kwahiyo unataka kuniambia kampuni za simu zinalipa kodi karibu 40%?! Na bila shaka unataka kuniambia kampuni za usafiri nazo pamoja na kulipa VAT bado wanalipa 18% kwenda SUMATRA?! Aidha, kampuni za nishati nazo zinafanya hivyo hivyo kwa EWURA?! By the way, mapato ya VAT yaende TCRA kufanya nini?! acha uwongo wako mkuu!! taasisi kama TCRA huwa wanaishia kupewa ruzuku tu na sio vinginevyo.h
hebu tuwasikilize wenyewe TCRA wanasemaje:

About TCRA:
The Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA), established by the TCRA Act no. 12 of 2003 is an independent Authority for the Postal, Broadcasting and Electronic communications industries in the United Republic of Tanzania. It merged the former Tanzania Communications Commission and the Tanzania Broadcasting Commission. Its role include licensing and regulating the Postal services, Broadcasting services and Electronic Communications sectors in the United Republic of Tanzania.
TCRA became operational on 1 st November, 2003 and has effectively taken over the functions of the two defunct commissions.
Specifically the Authority is responsible for enhancing the welfare of Tanzanians through:

****Promotion of effective competition and economic efficiency;
****Protecting the interests of consumers;
****Licensing and enforcing licence conditions of broadcasting, postal and Telecommunications operators

****Establishing standards for regulated goods and services
****Regulating rates and charges (tariffs);
****Managing the radio frequency spectrum;
****Monitoring the performance of the regulated sectors.
****Monitoring the implementation of ICT applications.

Sasa hiyo kazi ya u-TRA wameanza lini na amewapa nani?!
 
Ni kweli bandugu kuna jamaa moja ambia mimi salary slip iko pelekwa kwa benki tangia alhamisi lakini napata benki haiko na kitu hata kwa masaa haya..alafu hii jamaa ingine ambia sisi mshahara tarehe 30 kwani kama jana napata 24 alafu leo napata 30 kweli hyo ni mwezi moja au napata mwezi na masiku 6?sasa serekari nalipa sisi kwa masiku 30 ama masiku 36?mimi iko naona bantu leo balipwa baada kwa masiku over 30 days
 
Jamani, hata mliyebahatika kuajiriwa mnalalamika mshahara kuchelewa? Je, wale wanafunzi waliotoka vyuo vya UALIMU tangu mwezi wa sita mpaka leo hawaajiliwa, wao wanahali gani mpaka sasa? Maana matarajiyo yao yalikuwa "tukimaliza tu mafunzo ya ualimu na matokeo kutoka basi, sisi walimu na serikali yetu sikiivu itatuajili" lakini hadi leo ... Hapa naona kuja jambo "Serikali ime...."
 
Kwahiyo unataka kuniambia kampuni za simu zinalipa kodi karibu 40%?! Na bila shaka unataka kuniambia kampuni za usafiri nazo pamoja na kulipa VAT bado wanalipa 18% kwenda SUMATRA?! Aidha, kampuni za nishati nazo zinafanya hivyo hivyo kwa EWURA?! By the way, mapato ya VAT yaende TCRA kufanya nini?! acha uwongo wako mkuu!! taasisi kama TCRA huwa wanaishia kupewa ruzuku tu na sio vinginevyo.h
hebu tuwasikilize wenyewe TCRA wanasemaje:

About TCRA:
The Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA), established by the TCRA Act no. 12 of 2003 is an independent Authority for the Postal, Broadcasting and Electronic communications industries in the United Republic of Tanzania. It merged the former Tanzania Communications Commission and the Tanzania Broadcasting Commission. Its role include licensing and regulating the Postal services, Broadcasting services and Electronic Communications sectors in the United Republic of Tanzania.
TCRA became operational on 1 st November, 2003 and has effectively taken over the functions of the two defunct commissions.
Specifically the Authority is responsible for enhancing the welfare of Tanzanians through:

****Promotion of effective competition and economic efficiency;
****Protecting the interests of consumers;
****Licensing and enforcing licence conditions of broadcasting, postal and Telecommunications operators

****Establishing standards for regulated goods and services
****Regulating rates and charges (tariffs);
****Managing the radio frequency spectrum;
****Monitoring the performance of the regulated sectors.
****Monitoring the implementation of ICT applications.

Sasa hiyo kazi ya u-TRA wameanza lini na amewapa nani?!

Kwa mawazo uliyo nayo, kamwe hutaweza kuona kitu kizima hivi ambacho ndicho serikali. TRA ni kama TCRA. Je TRA pia inapokea ruzuku kutoka serikalini? Kwa taarifa yako ukusanyaji mapato kwenye kampuni za simu siyo kitu rahisi kama vile kulipa kodi ya pango TRA. Kunahitajika utaalamu wa hali ya juu na watu wenye wataalamu na vyombo vya kudhibiti mianya ya kukwepa kodi ni TCRA. Upo?
 
wanajf salaam!
hivi ni kweli kwamba hali ya serikali ni tete kiasi cha kuchelewesha mishahara ya wafanyakazi mpaka sasa?
nikiwa miongoni mwa wafanyakazi wa umma,nimepata salary slip yapata 4 days now ila hundi ya mshahara haijapelekwa bank,nimemuuliza mhusika w kwa hapa ofisini kwetu anasema serikali haijaleta pesa wao wametoa slip in advance tu.

mwezi uliopita kuna mjumbe wa jf alitoa mada hii mimi sikutilia maanani kwa kuwa mwezi ulopita sisi tulipata mishahara mapema ila sasa nadhani ndio zamu yetu....

duuu napata hofu na muelekeo wa serikali yetu.au ndo ule msemo kuwa 'nchi imeshauzwa?'

nawasilisha.

Serikali kwa mwezi inakusanya Tshs zaidi ya 500 billion , na mishahara ni Tshs 240 bn tu . Sio kwamba hakuna pesa za mishahara ila ni urasimu wa wachache tu kwenye ku process mishahara kule hazina

 
Fanyeni kazi acheni kupiga umbeya mwisho wa mwezi bado tayari mshaanza kulalama hela ya mwisho wa mwezi. Je mngelikuwa mnafanya kazi katika kampuni binafsi ambapo mshahara hutoka tarehe 30 si mngelia nyie vp!!!!

Mkuu, ebu tupe tafsiri yako ya mwisho wa mwezi. Mshahara wako wa mwezi ni makubaliano yako wewe na mwajiri wako kwamba atakuwa anakulipa tarehe ngapi ya kila mwezi. Sasa mwajiri SERIKALI alitangaza kwamba watumishi wake watakuwa wanapata mishahara yao kabla ya tarehe 24 ya kila mwezi. Kwao huo ndiyo mwisho wa mwezi wao. Tarehe hiyo inapopita bila kupata mshahara lazima ilete maswali, kwa nini hivyo?
 
Hapa ndipo ninapopata taste ya ile wanayoilalamikia CDM...."CCM wasijifanye wasemaji wa vyama vingine!" Je, nikuletee mkataba wangu wa kazi ili uone kama sijaajiriwa?! salary yangu ya October 2011 nilipata November 03; na hii ni kwa wenzangu wote na hakuna kibarua hapo!

Hiyo itakuwa kampuni ya kimjini mjini! Mkuu sekta binafsi mishahara inaingizwa kwenye account kuanzia tarehe 20 japo salary slip inasemapay date tarehe 25 na nikitu cha kawaida kabisa mbona.Poleni sana mlioko serikalini.
 
Amani na itawale mioyoni mwenu,subira yavuta heri hesabuni haya kama ni mapito tu kuelekea kwenye ukombozi kamili wa taifa letu toka kwenye makucha ya ukoloni mambo leo wa ccm.
 
jamani wakati mwingine wafanyakazi muwe na tumiradi,unaona sasa boss wenu kafulia mtafanyaje?njooni mtaani tuandamane
 
Back
Top Bottom