HALI YA MZEE MALECELA: Ninawashukuru Sana JF

Status
Not open for further replies.
I am also the victim kuandika chochote kwenye hii thread, let's continue with out movement to rescue our country. Hakuna benefits zozote zile kuendelea kuandika na kujibishana na familia ya malecela. They are done na sisi wananchi tunakazi kubwa kudiscuss issues zinazolenga kutafuta solutions za nchi.
 
Mpe pole sana Mzee Malecela pamoja na Bi Mkubwa! Tupo pamoja
chatu dume imebidi nikubandikie avatar yako

..................................
avatar38162_22.gif
 
huyu mzee alipenda sana madaraka, yani vyeo vyoote alivyopitia bado aligombea tena ubunge, watoto wadogo wakamgalagaza, yani hata huyo aliyeshindana nae si chochote lakini watu wakaona bula yale kuliko babu huyu, ametoka kwa aibu kubwaaaa! Na ccm wakagoma kurudisha jina lake!
Sasa kama mnakataa hajaenda huko US hospital, basi nyinyi watoto ni machizi kumruhusu mzee kusafiri akiwa na afya dhaifu, na je kama si mgonjwa, kwa nini Anne akose vikao muhim vya bunge kwa kutembelea watoto wa kambo mda huu! Kwahiyo watoto wa kambo ni muhim kuliko wapiga kura wake kule kili?
 
Poleni sana kwa kazi nzito ya kumuuguza Mzee wetu, Mungu ampe Nguvu, Tumshukuru Mungu kwa kila Jambo
Get well soon Mzee
 
William mwambie maza tunamisi sana ile sauti yake kali mjengoni. Afanye haraka arudi bana, watu wa same wanamuhitaji awe mujengoni bana kuwawakilisha.
Hivi huwa unaliona bunge letu huko uliko? yaani mijadala inaendeleshwa na watu wachache kuliko nilivowahi kuona. Mwambie arudi chap chap basi.

Usitukumbeshe mateso watu wa Same. Kwani sauti yake inatusaidia nini sisi wapiga kura. Tunalishwa kasa kila mwaka. na huu ni muda wa mwisho wa CCM Same.
 
Aisee pole sana mkuu msalimie mzee ila mwambie akirudi huku amwambie live kikwete kuwa CCM ni lazima in'goke ili angalau tufikie robo ya USA, then salamu toka kwa kijana aliyemwangusha Livingstone Lusinde na imani anamwombea apone ila mbona kijana kapwaya sana bungeni? au mdomo umejaa barafu? why kwanini?
 
Poleni sn mkuu kwa kuuguza,ila akipona na hali yke ikitengemaa hebu mshauri atumie influence yko kuishauri serikal ijenge hospital ya kueleweka ili kuwaokoa maskin weng wanaozikwa wazma kwa kukosa pesa za kusaka uzma huko ughaibun.othr wise 2memmis sn mama K pale mjengoni.i wish huyo awe rais wa kwanza mwanamke aftr handsome boy.polen sn
 
Swala la watawala kusahau kuimarisha huduma za afya huku wakitegemea kodi zetu ziwapeleke nje wakituacha tukifa kwa magonjwa wanayotibika ni jambo la kulaani sana. Rufaa lazima iwe ni ya msingi hasa pale inapotumia kodi zetu walala hoi. Haingii akilini hata tiba ya kawaida hawa watu wanakimbilia nje. Umefika wakati kujua zaidi ya watanzania 97% hawana uwezo wa kwenda nje kutubiwa wala serikali haina uwezo wa kuwapeleka nje. Hivi nini kinashindakana kuimarisha hospitali moja kuwa ya rufaa kiukweli ili kuweza kupamabana na magonjwa makubwa na upasuaji mkubwa kwa kuajiri madaktari bingwa na vifaa vya kisasa?? hakuna jipya wanalolifuata nje zaidi ya huduma bora. tuwalipe madaktari bingwa mishahara mizuri na kuimarisha hosipitali walau mbili au tatu Tanzania nzima.

Kama kweli hawa viongozi wanajazana nje ya Tanzania kutibiwa ndio sababu ya huduma zetu za jamii kuzorota siwezi kuwaombea mema. kwani wameaacha watanzania kibao wanakufa kwa magonjwa marahisi kwa kujilimbikizia mali za wizi wa kodi zetu. wakumbuke tu wao watapona ila kuna wajukuu, shangazi, mjomba binamu, majirani wanaokufa kwa malaria tu.

Mzee malecella nakuombea upone haraka, na uende ukawaambie watawala wako kuwa unapenda watanzania wapate huduma kama uliyopata kwa kuimarisha walau huduma za Muhimbili kwani uwezo tunao.
 
Mzee Malecela amekuwa kimya muda mrefu sana, anaona maovu yanaendelea nchini yeye anayaweka rohoni! Kwa vile yamejaa rohoni bila kuyatoa hadharani sasa yamamsababishia matatizo. Asipo yatapika maovu ya CCM yatamendelea kumuumiza kiafya!

Mwanasiasa yeyote wa ukweli lazima akemee maovu yanayotendwa kwa wananchi hata kama alikwishatoka kwenye system. Mwambieni atoe dukuduku zake kuhusu sarakasi zinazoendelezwa na serikali ya kisanii naye atapona!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom